ruralofficer
JF-Expert Member
- Apr 4, 2014
- 2,499
- 3,635
Amesema sawa ni vizuri: Kwanini anasema muda huu ambao yeye mwenyewe hafanyi vizuri kwa nafasi yake?Man u ina matatizo na watu hawataki kuambiwa ukweli
Mwisho wa cku CR7 kasema ukweli ili timu ipone matokeo yake watu wanamshambulia CR 7
Cjui vichwan mwa watu kuna nn? Mtu anajifanya kuijua man u kuliko CR7 mwenyewe
Unadhan kuna mtu anaweza kutoboa jipu kama alivyofanya yeye??? Hana cha kupoteza na mwalimu amuheshim C7 mwalimu wa daraja la chiniAmesema sawa ni vizuri: Kwanini anasema muda huu ambao yeye mwenyewe hafanyi vizuri kwa nafasi yake?
Ameonesha tabia mbaya zisizofaa kwa wachezaji wenzake hususani kumsema namna ile mwalimu wa timu.
Ronaldo yupo sahihi, toka alipoondoka Ferguson timu haileweki inataka nini, walishayasema Van gaal na Mourinho alichofanya CR7 ni kukazia tu. Timu inahitaji mabadiliko makubwa sana.Nilitaka kwenda Man City lakini Sir Alex Ferguson alinipigia na kuniambia sipaswi kwenda City nami sikutaka kumkatalia, nikaufuata moyo wangu na nikarejea Old Trafford.
Nilidhani nitaona vitu tofauti ndani ya United lakini nimeshangaa mambo mengi ni yale yale tangu nilipokuwa nina miaka 20,21,22 teknolojia imebadilika ila United tupo pale pale.
Nahisi kusalitiwa na Man United, kuna baadhi ya watu hawataki niwepo hapa na sio msimu huu tu ni tangu msimu uliopita wanataka niondoke, mimi naiheshimu sana klabu hii na Mashabiki wake.
Sina heshima yoyote kwa Erik Ten Haag kwakuwa yeye haniheshimu, kama wanataka kufanya mabadiliko ikiwemo kuniondosha ni sawa ila wanapaswa kubadili vitu vingi sana ndani ya United.
Sijui kwanini Wayne Rooney ananikosoa sana, pengine kwakuwa bado nacheza muda mrefu tena kwenye ushindani mkubwa kuliko yeye, hilo sifahamu.
- Sehemu ya Interview ya Ronaldo na Piers Morgan ambayo itaanza kuruka Jumanne na Jumatano.
Sidhani kama kuna timu yo yote itakayokuwa kumchukua mtu anayejiona wa maana kuliko wenzake wote, na hata kuliko kocha.Mtu analipwa £500k p/w..summer hii pia meneja wake alikuwa anapiga simu kwa kila sporting director anayemjua ili amtoe Ronaldo United..Yet Ronaldo anasema anahisi kusalitiwa ..
Achilia mbali drama nyingine alizotufanyia..
I hope ameshapata timu ya kwenda January hii.
Mkuu shida ya United ipo ndani wewe ukimuangalia Ronaldo huhisi kwamba anareact kutokana na anavyotreatiwa United?Ni kwel kwenye uongozi kuna shida , hakuna asiejua,,,,
Ronaldo kaongea upupu Sana eti hamueshimu mwalimu,,,,
Alafu amevizia hakuna match hivi karibuni watu wanaenda world cup ndo akaongea ,,,,
Kingine anataka kutafuta huruma na support kwa Mashabiki waone kwamba ameonewa, mchezaji mkubwa wa caliber yake anakuwaje na vituko Namna hii,,, watoto/vijana Kama kina Alejandro/Anthony wanajifunza Nini toka kwake ?
Ni muendawazimu pekee ndiye atakaekuwa upande wake na kumtetea ,,,
Alianzia ujinga wake pre season, akaja Kuna match moja sikumbuki alitoka kabla muda , akaja ya Spurs, juzi aaambiwa match na Fulham hatoanza lakini atakuwa sehemu ya kikosi, yeye akadanganya anajisikia vibaya kwa hio hakusafiri na wenzie kwenda London,,,
Umri umemtupa, hawezi kufanya alichokuwa anafanya akiwa 20's ama early 30's ,!
Mwisho wa siku hakuna mchezaji aliemkubwa kuliko club never,,,, ! Watakuja wengi na wataondoka, that's all
Timu ipo Salama na kwenye right direction chini ya ETH, apewe muda aweke ideas zake pia apate players anaowahitaji, sio kitu Cha siku moja ,,,msimu huu hatuna Cha kupigania tushinde,,, sana sana tunahitaji kushiriki UEFA mwakani
Chief-Mkwawa Anahesabika Kama legend ? Kwangu Ni Big No, kaiexpose Sana club na dharau kwa mwalimu
Naona wahuni mmeamua kuanzisha memes juu ya Ronaldo.GlazerOUT
Ronaldo IN
MAGUIRE IN
BRING BACK POGBA
BRING BACK TUANZEBE
Hata kama aliyo yaongea ni sawa ila alichoboronga ni hapo kwenye kumlalamikia kocha wake kua hamuheshimu na yeye pia hawezi kumheshimu.Man u ina matatizo na watu hawataki kuambiwa ukweli
Mwisho wa cku CR7 kasema ukweli ili timu ipone matokeo yake watu wanamshambulia CR 7
Cjui vichwan mwa watu kuna nn? Mtu anajifanya kuijua man u kuliko CR7 mwenyewe
ETH Anapongezwa kwa sasa ila najua muda si mrefu utamgeuka.umeshaambiwa tatizo la united sio Ronaldo wala ETH tatizo ni viongozi wa hii club hawataki kuwajibu kwa ajili ya future ya club tangu aondoke sir Alex Ferguson mpk leo hakina transformation ndo maana timu inafanya vibaya wamekuja akina pogba, van gal, mourinho,lukaku wote wameondoka wanasema uongozi wa club ni tatizo ndo maana timu haiendi top level leo ameongea Ronaldo tena bado mnabisha mtaendelea kusindikiza watu wanabeba mataji miaka na miaka ndo maana mnaitwa united fans hili swala mlibebe msiweke chuki tu dhidi ya Ronaldo ameongea ukweli hata kama hakutakiwa kuongea
Mpumbavu huyu, dirisha kubwa alitaka kuondoka ila management ikamkazia ndio maana ameamua kuisagia kunguni kipindi hiki ili dirisha dogo likifunguliwa tu aruhusiwe asepe.Nimempongeza EtH kwa kuhakikisha nidhamu inakuwepo kwenye timu na timu inakuwa moja bila kujali ukubwa wa mchezaji. Ronaldo alitaka awe mkubwa kuliko Kocha na hilo sio sahihi.
Tatizo la uongozi wa club lipo na linajulikana lakini halihalalishi mchezaji kutokuwa na nidhamu kwa Kocha,wachezaji na timu nzima.
Ronaldo ana mkataba pale kama mchezaji, angetimiza wajibu wake kwanza ndio aanze kiherehere.
Yani kocha yupo huko anajenga nidhamu na roho ya kujituma kwa wachezaji, yeye anahaha kwenye media kumvunja kocha moyo pamoja na wachezaji wenzake? Halafu unasema tatizo la club?
Ronaldo ni mbinafsi, anaangalia Records zake binafsi, hizo ni hasira za kuwekwa bench. Yeye hata kama anajua ni mzigo kwa timu hajali, anataka apangwe tu Records zake zitimie.
Mtu analalamika hata aibu hana, amekuja Cavan anajituma kuliko yeye ila kwa heshìma akavuliwa jezi aķapewa yeye, anataka heshima gani tena?