Manchester United (Red Devils) | Special Thread

@KENGE 01
Kukusaidia tu tukujibu hivi;
1. Tunabeza kikosi cha ETH pale anapotuwekea mid field dhaifu (erickson,vande beek) na kuwaacha wagumu Fred na Tominay nje.
2. Timu haijacheza vizuri toka dakika 1-90 kama unavyosema. Baada ya sub (Van de Beek, Martial) mdio tumekimbiza sana mpaka wakatamani mpira uishe.
3. Kikosi cha Villa sio kile kile cha last game. Hao miamba wao uliowataja (Mings,Bailey,Cash,Digne...) wameingia kuanzia dakika ya 60. Walianza na watoto.
4. Umewapa bigup wachezaji wa Man U waliofanya vyema nimekubali lakini umefanya kosa moja HUKUMTAJA TOMINAY, amekiwasha kweli kweli.
 
Hahaha, Sancho amepoteza kujiamini nadhani, akipatiwa muda atakaa vizuri. Tulitarajia mambo anayofanya Garnacho ndio angeķuwa anayafanya Sancho,ila hali imekuwa tofauti.

Garnacho akitunzwa vizuri hapa tuna mchezaji hatari sana.
Last game commentator alisema kwa namna anavyocheza lazima atakuja kuvaa jezi no. 7 ya United.
 
Maguire amecheza vizuri sio..Okay.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…