Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Upo sahihi kabisa ila Fernandes muache.
 
Nilivyoona tu kikosi nilijua kitachotokea sijui kwanini kocha kamuacha fred nje dhidi ya DVB.

Ok next game aston villa wanakuja OT Alhamis tutajua wametuotea au mbinu hatuna.
Wawaotee mmechaniwa packet ya dume kabisa, mlishalainika nyie
 
Yaani unaongea tu! Watu wameajiliwa ofisini mwao we unasema waondoke, kama we ndo muajiri

Hii nchi ngumu sana
Sasa we jamaa unadhani mimi kusema waondoke hapa watanisikiliza huko Ulaya


Acha makasiriko ndugu huu mchezo wakongoman wanakuambia malembe...yaan pole pole...hauhitaji hasira

Hapa ni maoni tu kama mashabiki...na mashabiki wote wana maoni yao.


Mtaalam Ralf Rangnik alishasema hayo wakamfukuza...ila ngoja tuone Carabao wataingiaje
 
Mimi maoni yangu.

Ronaldo sasa ni muda wa kuanzia benchi, hamna anachooffer.

Zile kelele ilitakiwa Ten Haag akaze, hakuna kumpa minutes za kuboroga.

Sasa hivi mentality ya Ronaldo ni afunge approve wrong watu.

Duh! Hamna cha team work tena


Lindelof *****, shenzi sana. Yaani unasindikiza mtu mpaka boksi hata hujaribu kumsukuma au kumfanyia tackle ili apoteze balance?


Lindelof sio beki bora apelekwe CDM awe analisha mipira mirefu mbele.

Kocha nae aache ukuda, awe anaweka watu hitajika siku ya mechi, kina Fred, ikiwa gemu ngumu


Kingine wakuu, nadhani nyie hamkuona ila DE GEA katuchoma leo.

Goli la kwanza, na Freekick, si ni juzi hapa alifanya impressive saves.

Alafu kipa awe anafanyiwa hata rotation kutoa challenges bana
 
Poleni sana Kwa yaliyowakuta mjikazage sio kulia lia sana
 
Sijui kwa nini kipa habadiliki...

Ronaldo akipewa service nzuri anaeza kifunga goli mbili tatu...changamoto hatengenezewi clear chances...hakuna crosses wala pass za mwisho nzuri

VDB asicheze tena kashachoka mda mrefu ndo maana kina Ole na RR hawakumkubali jamaa anazingua sana

Erikcsen apumzike..jamaa kachoka asee
 
Yani leo timu za ugenini zote zimeshinda kasoro nyie tu nyumbugile.
 
Improvements gani zipo? Hakuna kitu ushindi tunapata wa ndondokera hamna lolote, mpira tunaocheZa hauna malengo yoyote yaani tunapooza tu mpira wapinzani wakipata mpira ni presha tu hata tukifungwa sawa kitu tunataka kuona ni mpira unachezwa wa kueleweka kama hatuchezi mpira nzuri hata ushindi hauna maana kwetu, naanza kupoteza imani na ETH
 

Utakuwa umeshiba mihogo inakulevya
 
Ya
Muache kocha ajenge team, kwanza huu msimu sina cha kumdai kocha wala hao wachezaji kwenye EPL labda ueroper huko angalau wafike nusu au fainali.
Yah ni kweli...lakin kinachojengwa ni kipi na huku mambo ni yale yale yanajirudia mechi hadi mechi...ukiangalia mechi za hivi karibuni utd wanastrago sana kufunga

Ukifatilia utajua kocha washambuliaji ni Ben Mcarthy msauzi labda shida ndo inaanzia apo!!
 
Siku Ronaldo akiondoka wengi mtakumbuka aina ya mchezaji tuliyekuwa naye. Striker, goalscorer, GOAT, goal machine. 'No service, no goals.' Old Trafford hata umlete Haaland utaishia kutukana tu tumepigwa.

Mchezaji kama Bruno mnamlaumu bure tu ila naamini influence ya mazingira aliyokutana nayo klabuni yameshusha kiwango chake.

EtH ni kocha atakayerudisha zama zetu, kitu kinachodhihirisha hilo ni kwasababu ameweza kuleta wachezaji wenye manufaa kwa timu yetu. Suala la kusema leo kazingua kufanya sub hiyo ni mitazamo yetu tu, hata yeye ni binadamu anafanya kitu anachoamini na kukosea kupo tu.

"In football you don't deserve, you win or lose."
 
Umeongea pointi sana...mechi tunazoshinda ni za kinaga ubaga. Kina shaw na dalot wanafika juu wanarudisha mpira kwa CB kisha unazunguka duara tu...hakuna penetration pass yoyote ya kuaminika hakuna chance zinazotengenezwa
Man utd bado sana


Cha kushangaza kila timu ikicheza na Utd inacheza vizuri sana..
Pass za haraka na wanatengeneza chamce nyingi sana...hata Omonia alitupelekesha sana


Anyway labda watabadilika baadhi yao wakiondoka
 


Ni kweli...akiwaondoa deadwoods wote labda timu itabadilika tusubiri msimu uishe


Huu bado sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…