Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu, issue ya nani acheze na nani asicheze Ina sababu nyingi zaidi ya ambavyo huwa tunafikiri.
Chache kati ya sababu hizo ni ;
1. Mkataba wa mchezaji & role yake, ambapo mkataba una kiwango cha chini/minimum amount of matches he has to play in a season.

2. Falsafa ya team/league husika. Pale United falsafa yake imejikita zaidi katika kupromote homegrown players (wachezaji waliokulia kwenye academy za pale kwao). Hivyo fanya ufanyalo, m-british pale falsafa inamlinda zaidi ya maelezo.

Kuhusu issue ya kutumia academy players kama ulivyosema hapo nimeliongelea tayari. Wachezaji ambao tayari wapo kwenye locker room wana impact hasi au chanya kwa wale wanaokuja/kuchipukia. Hivyo mazingira yaliyopo United sasa hivi yanakuwa sio friendly sana kwa wachezaji wachanga. i.e mifano ya kuigwa iliyopo pale kwa asilimia kubwa haina United spirit.

Kwa kumalizia, role ya kocha kwenye generation ya mpira wa sasa imebadilika sana.
Maamuzi ya kuhusu team yanayofanyika yanakua sio 100% matakwa ya kocha, Bali kuna sababu kadha wa kadha ikiwemo hizo nilizoanisha hapo juu.
Sasa hivi ndo maana role Ile sio Football Manager entirely, ila is just a coach ndo maana unaskia kuna technical director sijui, na vyeo vyeo kama hivyo.

Kama unakumbuka vizuri, hii ni moja ya sababu zilizofanya Mourinho anashindwana na United. Sababu kubwa ni structure ya club haimruhusu yeye kufanya maamuzi ya moja kwa moja kwa utashi wake binafsi, ila kuishi katika misingi ya club.
Things change with time, na United bado haitaki kubali katika hilo. Ndio maana team ina-struggle sana.
Nimelielezea vizuri nyuzi za juu kidogo. The problem is way deeper than a coach pale. Don't be surprised hata aje mtu kama Pep hivi af still akaishindwa Ile team. Maana kujinasua kutoka kwenye shida inayoikumba United it's way beyond inavyoonekana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe una mahaba na Ronaldo,Ata avatar Yako inaonesha wazi.

Swala la Ronaldo hata Allegri alilizungumzia,Wewe unaongea Nini???
Issue ya Ronaldo, japo I have nothing against him ila ilikua a matter of time tu kunasa kwenye tuta.
United already had issues za kudeal nazo, na kwa mazingira yale ukiangalia kuja kwa Ronaldo lazima kungeongeza matatizo zaidi ya kuyapunguza.

Hamna mazingira rafiki ya mchezaji caliber ya Ronaldo kuweza kukipiga pale United kwa sasa.
Ndio maana aki-underperfom lazima #TeamCr7 wake na lawama kwamba hajapata service za kutosha. United kwa sasa haina mazingira hayo ya kum-guarantee mchezaji kama yule kupata service, lile chama la wana... Ni kupambana tu ili kusonga mbele
.

Purchase ya Ronaldo huwa naiona katika picha tatu sana sana.

1. Amenunuliwa kwa sababu za kibiashara. Cr7 brand hata haiitaji maelezo. Na kumbuka wenye Ile team sahivi wamejikita zaidi kwenye biashara.

2. Kuzuia Man City kumsajili. Hapakua na plan yeyote na hapakua na haja yeyote kwa United kuforce deal ya Ronaldo, ila tu kuwazuia City kumnasa. Hiyo case sahivi ishatokea kama mara 3 hivi... Ilianza na Alexis Sanchez, ikaja Maguire, na sasa Cr7. Kama ni mfatiliaji mzuri mchongo hapa ni kumzuia rival kupata kilicho bora, mwisho wa siku mbuzi kwenye gunia ndo United anaambulia.

3. Mahaba ya Ronaldo
. Ni ukweli usiopingika United alkua hajapona na trauma ya kumpozea Cr7 kwa hiyo miaka 12 (tangu 2009) alipoenda Madrid.
Ukipitia pages za United Twitter etc, Ronaldo kabla hajarejea United kwa mara ya pili, alikua ni mchezaji (Ex player) anayeongozwa kwa kuwa posted na United, mara kwa mara, kwa sababu tofauti tofauti.
So Influence ya SAF, na mahaba binafsi ya United kwa Ronaldo yakapelekea deal kuwa materialized.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida ya kocha huyu..hawapangi madogo wa akademy Tena anao kwenye timu ya wakubwa....

 
Kuna clip nimeiona inaelezea makosa yaliofanya na magwaya, lindelof, tominay

Mnakila sababu ya kuitwa NYUMBU
 
Tatizo la United ni Board.

Hakuna kocha anaepewa nguvu ya kuamua anataka nini bila kuingiliwa na board.

Na mbaya zaidi board haina watu wanaojua mpira.

Na mbaya zaidi wachezaji wameshakuwa miungu watu, wanalipwa mishahara mikubwa isiyolingana na viwango vyao. Wachezaji wananunuliwa based on uraia wa Uingereza na hawana viwango.

Tutabadili makocha wote duniani, ila nakuhakikishia, kama board itakuwa ndo hii ya type za kina Ed Woodward, tutaendelea kufeli milele.

Ralf ni the best way forward kwa kuanzisha project mpya. Ila mashoga kama kina Neville, Paul Mesron wameshaanza kumkejeli. Labda wanataka mabwana zao waje pale.

Project mpya haitakiwi kumuangalia mtu usoni. Kinyume cha hapo, miaka 20 kama ya liverpool itatuhusu.
 
Sahivi imeshajulikana wachezaji ndo tatizo.

Ralf yupo bold kwenye hilo, na wenyewe wameshaanza onja joto la jiwe.

Naona pundits pekee ndo wanawatetea.

Ila wachezaji ni mizigo.
 
Bora Ole kuliko huyu motivational speaker.

Ole alikuwa na pressure tu
lakini ange endelea ange onesha changes.

ACHA KUJIFANYA HAUONI.
Acha kuongea upumbavu.

Ole was absolute failure.

Wachezaji walimpenda kwasababu hakuwa mkali.
 
Ole angekuta structure inayoeleweka, angeperform vizuri tu.
 
Mara zote, ucaptain hapewi mchezaji mwenye jina kubwa au star.

Timu zote duniani zipo hivyo.
 
Mkuu uliyosem nimeona ata baadhi ya mashabiki uko England wanademand board ivunjwe ila nionavyo mimi ili ni gumu maana hayo yanategemea zaidi maamuzi ya wamiliki ambao ni GLAZERS FAMILY...na kwakuwa hao jamaa upande wa marketing unaendelea kuingiza pesa za mauzo ya jezi na mikataba minono kutoka kwenye makampuni kibiashara pale united...hawawezi fanya hayo maamuzi maana yakwao yanawaendea kwahiyo hawana haja na furaha ya fans, members na supporters wa clubs...

Ilifika kipindi msimu uliopita kuna baadhi ya fans waliwakataa hao glazers kwenye mgomo wa #GlazersOut kwa malalamiko ya kuwa KUNA SEHEMU YA MAPAA YA UWANJA PALE OT YANAVUJA MAJIRA YA MVUA lakini kina glazers hawana habari na marekebisho uku wakiwa wanakusanya mapato mengi kutoka kwa club,

Kimsing ningekuwa na mamlaka pale OT yule RR alitakiw kuwa DOF kama alivyotumikia kwa kipind kirefu akiwa RedBull Football Group then bwana Erik Ten-hag aje akabidhiwe timu kama kocha mkuu apewe muda wa kusuka timu ata 2-3yrs...pia aletew watu wake anaowataka yeye bila kuingiliw na bodi kisha kusubiri impact yake. Siwashauri kumchukua Pochettino maana yule jamaa tactic zake sio za timu kubwa zenye njaa ya vikombe ijapokuwa anauwezo mzuri wa kuunganisha timu kama tulivyomuona spurz, pia yale mambo ya DNA yatupiliwe mbali na hao kina neville wasisikilizwe kabisa katika maamuzi ya bodi.
 
Mara zote, ucaptain hapewi mchezaji mwenye jina kubwa au star.

Timu zote duniani zipo hivyo.
Sasa mkuu ukisema ivyo didhani kama ishu ni Ustaa ama sio...kikubwa awe na sifa nilizosem apo awali sidhani kama ulivyosema apo ina msingi...kwa kuwa tumeshuhudia mastaa kama Messi, Ronaldo, lewandowsk, ata iniesta walishawai vaa armbands za ucaptain mara kadhaa tena wakutegemewa kabisa japo kuwa ni mastaa.
 
Poch ni kama tumemrudisha Ole tukambadilisha jina.
 
Arm bands zinavaliwa na hao wengine wakati captains hawapo uwanjani.

Kila timu ina kapteni mkuu na yule ambae anakuwa kapteni uwanjani kama kapteni mkuu hayupo.
 
Arm bands zinavaliwa na hao wengine wakati captains hawapo uwanjani.

Kila timu ina kapteni mkuu na yule ambae anakuwa kapteni uwanjani kama kapteni mkuu hayupo.
Ok!...lakini ata hivyo bado bwana magwaya licha ya kuwa yeye sio staa lakini hana sifa za kuwa CPT mtu anakabidhiw ucaptain hana ata mwaka pale OT. Ni bora ata wangemkabidhi DeGea bhasi maana jamaa anajituma na yupo pale kwa muda...unless hana ubavu wa kukoroma kwenye locker room.
 
Yani uwe ovyooo ufike fainali ya Europe, ufike nusu fainal kila kombe,Umalize nafasi ya pili.

Acha mahaba na Ronaldo Ww,Zama zake zake zishaisha.
Zama zake zimekuja kuisha utd au co? Pogba naye zama zake zimeisha, Fred zama zake zimeisha, Bruno zama zake zimeisha, Cavani, Rashfod, wote hao zama zao zimeisha. Lkn zimeishia utd.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…