Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hii kusema wanatafuta interim coach mpaka mwisho wa msimu Kama nimewaelewa hivi! Yani huenda Kuna kocha pahala wanamvizia na wanaijua contract situation yake,,,,

Tutulize mtori nyama ziko chini ,,,,,
Kwaio kombe tusahau msimu huu sio!?
 
List yangu ni hii

1, Conte
2,, ten Hag
3,, gasperin
4,, Enrique


Khs walio na mikataba sio tatizo , mikataba huwa inanunulika,,, football means business,,,, ! Mfano mdogo refer kwa Mr Ancellot, alikuwa na mkataba mzuri Sana pale gudsonpark, Tena inaaminika Ni kocha alikuwa among ya list wanaopokea mpunga mrefu EPL , lakini Madrid walivyokuja hakufikiria mara mbili,,,!!!!!
 
Man management is one thing, techniques & tactics ni vitu vingine kabisa.
kuwa na technue & tactics bila man management skills ni sawa na kumlazimisha ng'ombe kunywa maji,
with man management skills, then ndo unaweza waambia wachezaji yale Guardiola aliwaombia siku wanaingia kucheza na man u.

when you have both, then you become the likes of sir Alex.
 
You're extremely wrong mkuu. Ukweli ni kwamba Zidane hayupo available kiasi hiko unachosema.
Ndiye kocha pekee asiye na kazi ulaya kwa sasa. Wengine wote ni lazima ununue sehemu ya mikataba yao.
Moja, yeye anataka France NT
Kumbuka hii sio self-appointment job.
Mbili, anataka kumaliza mwaka mmoja wa likizo yake.
Hayupo likizo. Yupo ktk frictional unemployment, kumbuka alifutwa kazi Real Madrid hakuondoka kwa kupenda. Toka amefukuzwa kazi hakuna timu iliyowahi kutuma maombi rasmi ya kumhitaji. Vyombo vya habari ndio vimekuwa vikizusha kuhitajika kwake. Sio kweli kwamba yupo likizo.
Tatu, hayupo tayari kuchukua team yoyote katikati ya msimu.
Hakuna timu iliyomuhitaji rasmi Jombaa.
Nne, mke wake hataki weather ya mji wa Manchester (kiafrica tunaichukulia poa ila wenzetu huko wanaskilizana kwenye maamuzi)
Mpaka hapa hafai kuongoza kundi la wanaume.
Kabla Mou hajaenda Inter alikua ameshaamua kuchukua kazi ya England NT mke wake akakataa.
Hahaaa are you sure? Weka uthibitisho hapa wa Jose Mourinho kupewa kazi ya kufundisha timu ya taifa ya Uingereza.
Talking about cheap, u cheap wake ni kwamba tu hana release clause yoyote. Ila package-wise jamaa sio the cheapest
Hapa umejijibu mwenyewe. Niliposema yeye ni cheap nilimaanisha huhitaji gharama za ziada nje ya mshahara wake.
 
Yeah mkuu. Mourinho, Carlo, Benitezi wote combined hawakuweza kufanya alichofanya Zizzou. Hili linaniaminisha ana kitu
Mkuu Real Madridi ilikuwa kwenye crisis uwanjani toka mwaka 2003, walipita makocha sita bila mafanikio.
1. Fabio Capello
2. Ben Schuster
3. Juan De Ramos
4. Manuel Pellegrin
5. Jose Mourinho

Wakati Mourinho anaenda Real Madrid alikuta haijachukua ubingwa mfululizo mara nne kwenye laliga ni katika kipindi hicho Mourinho alisajili wachezaji wengi sana ambao walikuja kuipa real Madrid mafanikio makubwa mfululizo miaka 6 baada ya Mourinho kuondoka alikuja Carlo Ancelloti ambaye usajili pekee aliofanya ni kumsajili James Rodriguez ambaye hakuwa na matumizi nae wakati huo Mourinho aliwasajili
1. Nuri Sahin
2. Sami Khedira
3. Mesut Ozil
4. Dani Caravajal
5 Fabio Coentrao
6. Angel Di Maria
7. Cavalho
8. Luca Modric
9.Xabi Alonso
10 Toni Kroos
11. Christiano Ronaldo
12. Karim Benzema

Wakati huo Manuel Pellegrin aliwaacha wachezaji wengine wengi
1. Marcelo
2. Klas Jan Huntellar
3. Gonzalo Higuain
4. Sergio Ramos
5.Rafael Van de Vart


Unaweza kuona squad iliyompa Matokeo Zidane alikuta ikiwa ndiyo iko kwenye peak hasa baada ya kuchukua UEFA chini ya Ancelloti.

Wachezaji wengi vijana aliowaingiza kikosini pale Madrid wengi aliwafundisha akiwa kocha katika timu ya vijana.

Kilichomwangusha Benitez katika kikosi cha Madrid ni ubrazamen tu wa kutaka kuanza upya katika kikosi ambacho kilikuwa na kila kitu, Zidan aliona mtego huo akaukwepa.

Lakini pia katika makocha hao sita waliopita Madrid Zidan alikuwa katika club kwenye sehemu ya benchi la ufundi hivyo alikuwa anaijua Madrid kuliko hata makocha wenyewe.

Kumpa timu mpya inahitaji muda ili aweze kuweka falsafa yake
 
Kuna point alikuwa anaieleza PTER kwamba Ole kinachomuangusha ni laisserz fair policy yake. Yani hana kitu anachopambania ni ngumu kupata matokeo kwa kuwachekea tu unaowaongoza hata wakiharibu.
 
Kuna point alikuwa anaieleza PTER kwamba Ole kinachomuangusha ni laisserz fair policy yake. Yani hana kitu anachopambania ni ngumu kupata matokeo kwa kuwachekea tu unaowaongoza hata wakiharibu.
Hilo ndiyo lilikuwa tatizo kubwa la Ole angebadilika eneo hilo Ole angekuwa alishatwaa ubingwa siku nyingi tu.

Kwanza msimu uliopita United ilikuwa na uwezo wa kuchukua ubingwa kama Ole angeamua kuwa mwanaume na siyo mvulana.

Man city ilikuwa na crisis na Liverpool ilikuwa kwenye crisis chelsea ilikuwa kwenye crisis ni Man United pekee ambayo haikuwa na problems.

Pia msimu uliopita ni Man united pekee iliyomaliza msimu bila wachezaji wake wote kupata serious injury wakati huo Man City haikuwa na De Bruyne Liverpool hawakuwa na defence, chelsea were in total shambles badala ya kucapitalize na hizo weakness za wenzake akaanza kugawa point kwa vitimu visivyo na ambitions zozote kama Arsenal na vi Newcastle.

Hicho tu kilinifanya nimuondoe Ole kwenye List of Men.
 
Gasperin! Ataleta Man to man marking kama Bielsa, ukikutana na timu bora kwa transition zenye good runners unakufa tano hadi sita. Kama United inavyowafanya leeds/ Atalanta.
 
Gasperin! Ataleta Man to man marking kama Bielsa, ukikutana na timu bora kwa transition zenye good runners unakufa tano hadi sita. Kama United inavyowafanya leeds/ Atalanta.
Sasa Gasperini ndiyo kiboko ya mabitozi na wanaopenda kumpangia kocha maamuzi.

Ukileta komedi kukurushia ngumi haoni kazi. Papu Gomez aliondoka baada ya Gasperini kutishia kumshushia kichapo kwa kuona ana masihara uwanjani.
 
Sasa Gasperini ndiyo kiboko ya mabitozi na wanaopenda kumpangia kocha maamuzi.

Ukileta komedi kukurushia ngumi haoni kazi. Papu Gomez aliondoka baada ya Gasperini kutishia kumshushia kichapo kwa kuona ana masihara uwanjani.
Noma sana. Haaah
 
Unafahamu kama Zidane alibakiza miezi 12 ktk mkataba wake? Jaribu kuchukua hiyo official statement ya Real Madrid juu ya kuondoka kwake linganisha na ya Ole utanielewa naongea nini. Tofauti ni moja tu Zizzou alikubali kujiwahi kujiuzulu kabla maamuzi hayajafanyika. Kuna tofauti kubwa sana ya mtu anayesitisha mkataba wake kabla haujaisha na mtu anayeamua kutoongeza mkataba wake baada ya kumaliza.

Kauli yake ya mwisho ilikuwa hii hapa ilikuwa tarehe 31 mwezi wa 5 mwaka huu alipoongea na waandishi wa habari

'I am going because I feel that the club no longer gives me the trust I need and doesn’t offer me the support needed to build something in the mid and long term. Over the last few months, I would have liked my relationship with the club and the president to have been a bit different to that of other managers.”

“tell me to my face that you want to get rid of me, not behind my back”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…