Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

timu yetu haiheshimiwi tena na vilabu vyengine ndio maana si ajabu tunateseka kwenye biashara ya kuuza na kununua mchezaji.

west ham wanaelekea kukamilisha usajili wa paundi millioni 25 kwa kurt zouma, kiupande wa pili wanaweka ngumu kulipa paundi millioni 25 kwa jesse lingard
Hili swali la kwanini hatuuzi wachezaji umewahi kuuliza mara mbili humu jukwaani na majibu ya wengi kama yalivyo yangu ni over rated english players pamoja na aina ya mishahara wanayolipwa waki renew mikataba yao pale united.
Au mkuu umeishapata majibu tofauti na hayo?
 
timu yetu haiheshimiwi tena na vilabu vyengine ndio maana si ajabu tunateseka kwenye biashara ya kuuza na kununua mchezaji.

west ham wanaelekea kukamilisha usajili wa paundi millioni 25 kwa kurt zouma, kiupande wa pili wanaweka ngumu kulipa paundi millioni 25 kwa jesse lingard
Naona uelekeo ilionao united kwenye dirisha hili la usajili ni kutoa wachezaji kwa mkopo tu.
nashindwa kujua kama biashara ya moja kwa moja imegoma au bado wana matumaini ya kupevuka zaidi kama alivyotuonyesha bwana Jesse pale westham.

Lakini dhana ya pili inaweza kuwa uelekeo wa timu kiuchezaji/wachezaji kukosa muda wa kutosha uwanjani inaweza kuwa sababu ya bidhaa zetu kukwama sokoni?
. Brando Williams ....Norwich
.Andreas Perreira...Corinthians
Amad Diallo... inaonekana anaenda championship kwa mkopo
.Tuanzebe...Aston Villa
.Facundo Pellistri....Alaves (kama niko sahihi hapa)
.Daniel James...inakisiwa anatakiwa na Leeds kwa mkopo
 
Hili swali la kwanini hatuuzi wachezaji umewahi kuuliza mara mbili humu jukwaani na majibu ya wengi kama yalivyo yangu ni over rated english players pamoja na aina ya mishahara wanayolipwa waki renew mikataba yao pale united.
Au mkuu umeishapata majibu tofauti na hayo?
bado sijapata jawabu rasmi ila hiyo ishu ya mishahara mikubwa inaweza kuwa ni sababu, kiupande wangu nadhani hizi pia ni sababu
  1. wachezaji wetu hatuwapi heshima inayostahili, sisi mashabiki tunaongoza kwa kuwadharau kwenye media tofauti na vilabu vyengine
  2. tunachelewa kufanya maamuzi:
  3. tunapenda kujiwekea imani isiyowezekana, kwa mfano tunaamini wachezaji wengi wanaotoka academy wana uwezo wa kuingia kikosi cha kwanza, fikiria mchezaji kama tuanzebe laiti kama tungelimbakisha kwa mkopo miaka miwili iliopita pale aston villa baada ya kuisaidia kupanda daraja tungelikwishapata fedha, hatimaye tukaamua kumrudisha na kuozea benchi
  4. wachezaji wengi vijana tena wenye uwezo wa kupigania namba tunawatoa kwa mkopo kwenye vilabu visivyo na ushawishi wa kifedha na hata kimvuto, mara nottingham forest, derby country, dundee united, hull city.
  5. Tariq lamptey ameingia kikosi cha kwanza cha brighton akiwa na miaka 18 akitoka chelsea, kwa nini hannibal, levitt, shoretire, mengi, garner na wengineo wasiweze kama kweli wana uwezo. Tunajificha kwenye hoja ya game time huku tukiwapotezea wachezaji fursa sahihi za kuonyesha vipaji vyao kwenye ligi kubwa
1629983873938.png
 
bado sijapata jawabu rasmi ila hiyo ishu ya mishahara mikubwa inaweza kuwa ni sababu, kiupande wangu nadhani hizi pia ni sababu
  1. wachezaji wetu hatuwapi heshima inayostahili, sisi mashabiki tunaongoza kwa kuwadharau kwenye media tofauti na vilabu vyengine
  2. tunachelewa kufanya maamuzi:
  3. tunapenda kujiwekea imani isiyowezekana, kwa mfano tunaamini wachezaji wengi wanaotoka academy wana uwezo wa kuingia kikosi cha kwanza, fikiria mchezaji kama tuanzebe laiti kama tungelimbakisha kwa mkopo miaka miwili iliopita pale aston villa baada ya kuisaidia kupanda daraja tungelikwishapata fedha, hatimaye tukaamua kumrudisha na kuozea benchi
  4. wachezaji wengi vijana tena wenye uwezo wa kupigania namba tunawatoa kwa mkopo kwenye vilabu visivyo na ushawishi wa kifedha na hata kimvuto, mara nottingham forest, derby country, dundee united, hull city.
  5. Tariq lamptey ameingia kikosi cha kwanza cha brighton akiwa na miaka 18 akitoka chelsea, kwa nini hannibal, levitt, shoretire, mengi, garner na wengineo wasiweze kama kweli wana uwezo. Tunajificha kwenye hoja ya game time huku tukiwapotezea wachezaji fursa sahihi za kuonyesha vipaji vyao kwenye ligi kubwa
View attachment 1909491
1. Najaribu kuwaza kama kipindi tulichopo kinaweza kuwa kinatuponza kwenye soko kwa maana hatuko na nguvu ya majadiliano ukizingatia mwenendo wa timu uwanjani,hivyo wananunuzi wanaona kama tumeporomoka

2. Na vipi kama wanunuaji wanaangalia mchezaji ametoka kwenye mikono ya mlezi gani ili alinganishe ubora na bei?
 
Najaribu kuwaza kama kipindi tulichopo kinaweza kuwa kinatuponza kwenye soko kwa maana hatuko na nguvu ya majadiliano ukizingatia mwenendo wa timu uwanjani,hivyo wananunuzi wanaona kama tumeporomoka
hii pia inaweza kuwa ni sababu, wanunuzi wanaingiwa na woga wa kujaribu bahati ya kununua wachezaji wasiohitajika na timu inayofanya vibaya. imekuwa ni rahisi kumnunua mchezaji anayekaa benchi chelsea kuliko kumnunua mchezaji anayekaa benchi man utd au arsenal.
nakubaliana na wewe nguvu ya matokeo ya uwanjani inahusika kwenye biashara ya usajili ndio maana vilabu kama chelsea, liverpool na hata man city wanatengeneza hela ndefu sana kwa miaka hii ya karibuni
 
Na vipi kama wanunuaji wanaangalia mchezaji ametoka kwenye mikono ya mlezi gani ili alinganishe ubora na bei?
chelsea wasingelikuwa na nguvu ya kutengeneza mpaka paundi millioni 100 za mauzo kwa msimu, mimi nadhani ishu kuu ni timing ya kufanya maamuzi.
 
Daniel James...inakisiwa anatakiwa na Leeds kwa mkopo
taarifa zinadai brighton na leicester wapo tayari kutoa mpaka paundi millioni 20 hadi 25 kwa ajili ya james lakini klabu imegoma, sababu ni moja tu klabu bado ina imani daniel james anayo potential ya kuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi japokuwa mimi siioni dalili hiyo.

sasa hapo ndipo tunapofeli, kwani tukimuondoa daniel james asiyekuwa na nafasi ndani ya kikosi cha kwanza huku nafasi yake ukimpa amad au elanga utapoteza kitu gani?
liverpool wamemuondoa grujic ambaye kila mshabiki wa liverpool anamsifia, kama tuna khofu ya kiwango chake klabu inaweza kuweka kipengele cha buyout clause kama wafanyavyo real madrid

tunapenda kujipa imani isiyokuwepo kwa kuwalea wachezaji wasioonyesha potentials ya kuwa bora kwa muda mrefu
  1. ondoa brandon na mapema then mpandishe yule fundi wa kihispania
  2. ondoa tuanzebe na mapema then mbakishe taden mengi
  3. perreira na jones hawakustahili mkataba mpya na wa gharama
  4. pellistri bado ni kijana, kama ataonyesha kiwango kizuri tunaweza kumrudisha au kumuuza huko hispania
 
Kwann cr 7 anaitaka city kuliko man utd ...

CR7 analala na kuiota man city ,yebabaaaaaaaaa...........

Hamjioni kama ni matakataka ,hamjielewi,hamna project yeyote ....
 
Back
Top Bottom