Manchester United (Red Devils) | Special Thread

sielewi mantiki ya kufanya mazungumzo ya kumpa mkataba mpya lee grant haliyakuwa muda huo huo tunavumishiwa kusajili kipa mwengine (tom heaton), Ina maana sergio romero ataondoka na mwenzake (de gea au henderson)?
Nathan Bishop Dean Henderson, David De Gea na Sergio Romero.

Huyo Tom Heaton wa nini ?
 
Nathan Bishop Dean Henderson, David De Gea na Sergio Romero.

Huyo Tom Heaton wa nini ?
mkataba wa sergio unaelekea ukingoni na anatazamiwa kuondoka bure, hapo ndipo unapouona udhaifu wa kiuongozi ndani ya klabu kama ulivyozungumza hapo nyuma, huyu sergio alitakiwa na everton pamoja na aston villa kwa nyakati tofauti lakini klabu ikaweka kizingiti kirefu cha fedha kilichosababisha vilabu viwili hivyo kushindwa kuchupa na kufikia makubaliano ya kulipa.
Msimu huu tumemdhalilisha kwa kumuondoa kikosi cha kwanza na hatimaye ataondoka bure (hapa namlaumu ole kwa aliyomtendea huyu jamaa)

Tom heaton anatarajiwa kuwa kipa wa hakiba namba 3, mwanzoni nilidhani lee grant ataondoka ndipo nafasi yake izibwe na heaton lakini taarifa za leo zinasema grant anafanya mazungumzo ya mkataba, Pengine klabu imeshanusa harufu mbaya ya kuondokewa kipa maarufu kati ya wawili wanaogombea namba ndio maana grant lee amerudishwa kwenye kundi.

ngoja tuone hii sinema itaishia wapi lakini tukumbuke tu hakuna timu kubwa inayohitaji goalkeeper kwa sasa labda pafanyike mapinduzi ya kihuni (PSG au Juventus).

jengine huyu tom heaton ni mtoto wa manchester united (alicheza pamoja na Ole)
 
Hata kama kuna golikipa anaondoka mkubwa kuna haja ya kumsajili Heaton wakati Nathan Bishop yupo
 
Hata kama kuna golikipa anaondoka mkubwa kuna haja ya kumsajili Heaton wakati Nathan Bishop yupo
tunajificha kwenye hoja ya uzoefu huku tukisahau huyo keeper anayekuja atakuwa chaguo la tatu, kmuajiri mchezaji mkongwe kwenye nafasi ambayo inaweza kusimamiwa na kijana anayechipukia ni matumizi mabaya ya madaraka.
Hapo ndipo unapozaliwa ugonjwa wa msongo wa mawazo kwa hawa vijana kwa sababu ya kutishiwa kwa fursa zitakazowawezesha kusonga mbele na kujitengenezea careers nzuri.

kwa miaka hii ya karibuni ni henderson pekee ndiye aliyefanikiwa kusonga mbele, wengineo wameishiwa kuhama ndani ya klabu.
  1. pierluigi gollini = ameishia atlanta baada ya kushindwa kuingia kikosi cha kwanza (afadhali huyu ana career nzuri)
  2. robert zieler = mjerumani aliyerudi kwao miaka 10 iliopita, kuna nyakati aliwahi kuitwa timu ya taifa ya germany
  3. ben amos = ameishia charlton
  4. joel perreira = amekuwa mtangaji wa vilabu, kwa ufupi huyu dogo hawezi kurudi man utd
 
Probably tunahitaji mabadiliko ya mfumo pia
hayawezi kuja mpaka tumuondoe mwalimu, mpira huu tunaocheza umerithiwa kutoka kwa sir alex (hatukucheza total football wala soka la kijerumani miaka yake yote)
bielsa ameupa jina la simple football, sasa sijui kama alikuwa anatusifia au kutudhihaki kabla ya mechi ya marudiano.

 
mjadala wa Ole gunnar solskjaer na mwanawe rashford utabaki kuwa ni mgumu sana, ukitumia jicho la kawaida hao watu huwezi kuwaweka katika kundi la ubora hata kwa dakika moja lakini ukiweka takwimu zao wanaweza kukuumbua hadharani.

sasa Itategemea na njia utakayoitumia kuwarate ubora wao, binafsi napendelea zaidi njia ya kutumia macho yangu dhaifu kwa sababu hunipa jawabu kwa mujibu wa mahitaji yangu

sijui wewe unatumia njia gani kuwarate hao jamaa ila nakuomba usitumie takwimu kwenye kuwapima ubora wao kwa sababu itakuwa ni rahisi kuadhibiwa.
Chief mkwawa hutumia takwimu kumrate mchezaji au kocha husika


Highest Goals Per Game ratio since Sir Alex retired, tatizo kubwa lililojitokeza ni GA

SeasonGamesGFGAGoals Per Game
20-2161121682.0
19-2061112511.8
18-195385701.6
17-1856101401.8
16-1764105461.6
15-165987541.5
14-154471441.6
13-145594571.7
12-1354114652.1
11-1254120562.2
 
United tayari wameshamrelease
 
Mimi huwatazama kwa jicho la kawaida tu na huwa nawatazama kwa takwimu ninapokuwa na sababu mahsusi.

Tatizo langu na Ole ni Laissez Faire attitude ambayo mara kwa mara tutashindwa kuwa serious kwenye mashindano tunayoshiriki.

Kitendo cha yeye kuwalea wachezaji wake kama ROOMMATES kimetugharimu mara nyingi sana maana wote hawaonyeshi nia ya ushindi as a team mpaka majini ya Bruno yapande na Cavani awe form wale vijana wake wao kazi yao ni kumaliza dakika 90 tu na kwenda kwenye Twitter kusema "not the result we wanted".

Kutobadilika kwa mwalimu kimbinu jambo la kushangaza msimu huu kuanzia mechi ya kwanza ya ligi mpaka tunamaliza msimu sisi ndiyo tumeanziwa kufungwa kila mechi kisha ndiyo tunaanza kujitafuta hii hali imetutengenezea sare nyingi sana ambazo tungeshinda tungeweza kutwaa ubingwa kwa gap kubwa tu dhidi ya Man city.

Mechi alizopoteza Man city na United hazikutofautiana sana isipokuwa tumetoka sare mara nyingi karibia mara tatu ya mechi alizotoka sare man city.
 
 
Timu yetu inasifikaga ina pesa kuliko zote duniani mara inaingiza oesa nyingi kuliko club zote, ila haijawahi onesha hilo hata siku moja......

Sijawahi ona msimu timu inasajili wachezaji wa paund mil 100 wawili waviwango vya juu na kuongeza beki wa paund mil 70 .....je tunajiita timu kubwa yenye hela kwa vigezo gani maana hata uwanja haujafanyiwa marekebisho muda mrefu imebaki historia tu pale OT......

Kwasasa ni dhahiri Manchester sio club kubwa bali ni club kongwe, hatuna maamuzi wala watu wazoefu wakuitwa experts wa timu kubwa kuanzia kocha hadi wachezaji baadhi.....

Hivi mchezaji kama Aguero anatolewa manchester tunaweza mtoa hata pogba umri ukifika.....Timu kubwa imejoficha kwenye kichaka cha rebuild kila msimu wanatumia paun mil 200 au 150 kwa wachezaji 4 au 5 alafu tunajiita timu kubwa how......

Timu yetu sio timu kubwa na yenye pesa.....kama tungekuwa timu kubwa na yenye pesa tungekuwa na wachezaji 4 au 5 wenye thamani ya mil 100 kwenye kikosi ila sidhan kama wanazidi 2......

Hapo unasikia timu imeshindwa msajili Dias kwa sababu wanaamini paund 25 ndio sahihi (refer msimu uliopita).....wanaamini Haaland sio mchezaji wa thamani ya paund mil 40 (plus add ons plus hela za wakala na blah blah nyngne) sasa ukubwa na utajiri wa timu uko wapi kama sio kuwekeza kwenye miundombinu ya uwanja na wachezaji wazuri....

Hatujawaji kumgombania kocha aliekwenyepick tukaweza kumleta OT ndio maana tumeridhika na Ole.....

Kweli man u ni ya kufungwa fainal na Villareal Kwa mechi ile?

Kuanzia kocha, wachezaji nusu yao, wamiliki na staff wengine wote ni watu wasiosahihi kuwepo klabuni.....

hivi unashindwa nini kumtoa Ole aliefeli na ukamleta Conte aliefree na ukampatia paund mil 300 akuletee ubingwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…