Mambo vipi wadau?
Kitambo sijachungulia humu, hii inatokana na pilika za kimaisha ukizingatia kazi zenyewe ni ngumu na usipofanya hakuna kula wala pesa ya bando utaisikia kwenye bomba.
Duh, sio poa mwenzenu nishakata tamaa ya kutwaa upingwa wa EPL, sikutegemea kama Palace angetushika shati mara ya pili.
Sijui tatizo liko wapi? Nani wa kumuangushia jumba bovu, wachezaji ama benchi la ufundi.
Ila ninacho weza sema "kutesa kwa zamu" wenda zamu yetu ilisha pita hivyo tusubilie awamu nyingine sijui ni mwaka gani?