Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ushindi mapema sana au sio, NYUMBU bana mnajua kujifariji sana
Ipo vzr..lakini lazima tuweke double attacking midifilders hapo mbele acheze na Bruno,,inapaswa kati ya rashford,, au martial mmoja aanzie bench,,kulia akae mata..au VDB..
tutashinda mapema sn
 
Hiyo fluidity unayoiongelea mbona siioni? Au wewe unaangalia mpira upi tofauti na ninaouangalia mimi?
 
Hiyo fluidity unayoiongelea mbona siioni? Au wewe unaangalia mpira upi tofauti na ninaouangalia mimi?
Kama umeangalia mechi ya West brom, kwa dakika Chache ambazo martial alienda Kushoto, rashford akaenda Kulia na cavani katikati, tulikuwa fluid sana.

Unapozungumzia fluid Attacking kwenye mpira unamaanisha ule uwezo wa wale wachezaji pale mbele kucheza nafasi zaidi ya moja. Wanaposhambulia wanaweza kubadilishana nafasi haraka haraka kutengeneza movement na kuwatoa defenders kwenye nafasi.

Kwa Timu yetu fluid ipo kushoto tu baina ya Martial na Rashford, hawa wapo comfortable kucheza striker ama ku cut in toka kushoto, na ni jambo la kawaida martial kumkuta kushoto japo anachezeshwa kati ama kumkuta Rashford kati japo yeye ni wa kushoto.

Mata alicheza Kulia mechi na WBA, Mata hawezi ku echange na wenzake, hawezi kudrible past player na muda mwingi anakuja katikati hivyo fluid inaharibika kulia.

Ndio maana mshabiki yoyote wa Man Utd anaefahamu hata basics za Formation utaona anataka winga wa kulia na makocha wote kuanzia LVG, mou mpaka Ole wanataka winga Lakini Bwana Mkubwa Woodward anajua zaidi.
 
Ole alikosea sana kumuondoa Diogo Dalot hiyo ilikuwa ni best option ya right wing basi tu.
 
 
Hii inakuwa 4 3 3 au or 4 2 1 3 ?
 
Mkuu umeeleza vizuri kuhusu martial na rashford na cavani..
Naomba niweke nyama kidogo kwenye comment yako,,
Ni kwamba mata analazimika kuingia katikati kwa maelezo ya Mwalimu kufuatana na kucheza double defensive medifilder..
Fred na tommy.

Pale mbele mchezaji creative ni Bruno peke yake,,
Kwahyo mata anacheza kati na kuua winger ni ktk kuongeza nguvu eneo la kiungo wa juu..
Ndy maana watu wengi wanazungumzia mfumo wa ole kuchezesha double defensive midifilder..

Siku man u wakipata beki imara hawatachezesha tena double defensive midifilder,,
Na hapo kila mchezaji atacheza kwa mfumo uliozoeleka wa man u kutegemea winger..

Nakuhakikishia hata Sancho akiwasili man u,,still watatumia double defensive medifilder sababu beki ni mbovu..
Ni sawa na bati linavuja sasa tunaweka nylone juu yake ili kupunguza bati kuvuja..

Ole anapaswa anunuwe beki imara,,na winger imara,,
Hapo utaiona man u ile ya Ferguson
 
Mechi tunazocheza na Holding wawili ni chache kuliko ambazo tunacheza na mmoja.

Kuanzia Post corona tunacheza na holding mmoja tu (matic) mpaka mwanzo wa msimu huu.

Tunacheza na holding wawili baada ya Pogba kuwa out of form na baadae akaumia. Wakati form ya mctominay na Fred ipo juu, na hata hawa wawili sio holding kivile ni Central midfielder, useme wana creativity ndogo.
 
Inakuwa kama hivyo..hapo mbele attacking midifilder ni Bruno na Marta,,

Defensive midifilder ni Fred na tommy.View attachment 1633675
Kuna mfumo fulani unaitwa 4-1-4-1 tulicheza wakati wa LVG, ule unacheza na attacking wawili ila unahitaji Dm anaejielewa, Si fred wala Mc tominay mwenye uwezo wa kucheza mwenyewe, tumeshajaribu mara kibao, ni disaster.
 
Kuna mfumo fulani unaitwa 4-1-4-1 tulicheza wakati wa LVG, ule unacheza na attacking wawili ila unahitaji Dm anaejielewa, Si fred wala Mc tominay mwenye uwezo wa kucheza mwenyewe, tumeshajaribu mara kibao, ni disaster.
Ili ucheze hivyo unahitaji DM world class kabisa kama alivyokuwa Fernandinho au Ndidi kwa kiasi fulani
 
Kuna mfumo fulani unaitwa 4-1-4-1 tulicheza wakati wa LVG, ule unacheza na attacking wawili ila unahitaji Dm anaejielewa, Si fred wala Mc tominay mwenye uwezo wa kucheza mwenyewe, tumeshajaribu mara kibao, ni disaster.
Tangu carik astaafu man u hatujapata kiungo wa chini mwenye akili timamu,,

Wote machizi watupu,,,inategemea na mwezi mchanga..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…