Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Watu wanaongelea uwezo binafsi wewe unaleta mafanikio, unajua Man. Utd tukiongelea mafanikio ya timu huwa tunasemwa tunakimbilia historia na hivyo timu yetu mnai-consider kama timu ndogo at the same time kupitia uwezo wake wa sasa ila imekuja ishu ya Bruno na Luka umekimbilia kuwalinganisha kwa mafanikio na kuacha uwezo ambao ndiyo kipimo chenu pendwa cha ubora ila nashangaa hapa umebadili direction ili tu upate conclusion kuwa Luka ni bora kuliko Bruno. 😂

Jaribu kuifanya nyeusi iwe nyeusi na nyeupe iwe nyeupe.
 
Hahahaaa duuhh, kweli kila mtu na muono wake
 
Amenishangaza sn, hzo tunzo binafsi wakati mwingine huwa zinaendana na bahati, Iniesta na ufundi wake wote hajawahi kupata ballon dor lkn Michael Owen anayo.
 
Bruno labda kupiga penaty ila hafiki kwa Fei toto
Huwa nashindwa kuelewa kwanini mashabiki wengi wa soka huwa wana chuki binafsi na wachezaji wa timu pinzani. Mnajichelewesha sana kufurahia mchezo wa soka. Huyuhuyu Bruno akija kwenye timu yako utaimba siku nzima ubora wake. Mashabiki wengine eti wanafurahia hadi wachezaji wa timu fulani kuumia. Acheni huo ushamba, kama hujui unachotaka kuongea kaa kimya!
 
Hii list sikubaliani nayo kwakuwa iko based on statistics, performance ya mchezaji inaweza kuwa chini kutokana na factor nyingi: kikosi, mfumo wa uchezaji na aina ya wachezaji.

Imagine Bruno awe na front-line ya;

SANE, LEWANDOWSKI, GNABRY
au
REUS, HAALAND, SANCHO

Can you imagine atatoa pasi ngapi za mwisho!?
 
Pumba
 
Bruno hamfikii ata Mukoko Teacher
 
Kwa nini useme Modric wa sasa na unajua anaelekea kustaafu soka.

Unapomrank mtu na mtu usimkate katikati mlinganishe kwa Uwezo wake wote toka umeanza kumfahamu.
 
Kwa nini useme Modric wa sasa na unajua anaelekea kustaafu soka.

Unapomrank mtu na mtu usimkate katikati mlinganishe kwa Uwezo wake wote toka umeanza kumfahamu.
Mkuu fuatilia mtiririko wa mada ilipotoka utaelewa kwanini nasema Modric wa ss.
 
Sioni sababu ya kuwalinganisha hawa watu..

Modric sio kamzidi Bruno tu bali hakuna kiungo ambae anamkaribia kwa hawa wanaocheza kwa sasa.

Tuache kuficha akili.
Umeona ss, ilikupasa ufuatilie mtiririko ulikotokea.
 
Martial na Rashford kuna muda unawaangalia unasema hawa ni world class..ila mechi nne mbele wanacheza kama watoto wa League 2 ya England..Pia sijui wanadekezwa kimtindo..
Tatizo la kwanza hatuna depth, wachezaji hao hao wanacheza wakiwa kwenye form ama hata wasipokuwa kwenye form, pia ukosefu wa winga wa kulia unachangia hao jamaa kuwa predictable.

Hata Neymar angekua united asingekuwa na utofauti sana na rashford.
 
Tatizo la kwanza hatuna depth, wachezaji hao hao wanacheza wakiwa kwenye form ama hata wasipokuwa kwenye form, pia ukosefu wa winga wa kulia unachangia hao jamaa kuwa predictable.

Hata Neymar angekua united asingekuwa na utofauti sana na rashford.
Kwahiyo mkuu kisababishi cha hawa madogo kuwa na long runs za inconsistency ni squad depth? au ni mimi sijakuelewa vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…