Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Fitness ikiwa regained mtapata ushindi mfululizo.

Hii imani ni yenye nguvu si mchezo. Mkuu kocha wenu tu anahangaika na formation ili Donny apate pa kucheza timu yenu haina uwezo wa kuanzisha shambulizi from scratch, kocha anataka RW sasa uahindi mfululizo utawezekana kweli?
 
Ni kweli wachezaji man u hawapofit lkn je nani anayepaswa kuhakikisha fitness ya kikosi?
Kinacholeta fitness ni mazoezi na muda, hatukuwa na muda wa kufanya mazoezi ndio maana hatuna fitness. Europa Imechelewa kuisha hivyo wachezaji wakachelewa kupewa likizo na sababu wamechelewa kupewa likizo wakachelewa kurudi kambini na kusababisha kuanza ligi bila fitness
 
Hahaha tumekosa visingizio mimi na nani? Swali la kawaida hilo unataka ugeuke ugomvi.
 
Mpaka leo tuna Record toka mwezi wa kwanza mwishoni hatujapoteza mechi yoyote ugenini, kama tuliweza kumaintain winning streak mpaka tukashika nafasi ya 3 kwanini tushindwe sasa hivi?
 
Mkuu unadhani baada ya muda gani man u itakua na fitness ya kuanza kushinda mfululizo?
 
Mpaka leo tuna Record toka mwezi wa kwanza mwishoni hatujapoteza mechi yoyote ugenini, kama tuliweza kumaintain winning streak mpaka tukashika nafasi ya 3 kwanini tushindwe sasa hivi?
Notis kwamba nimeongelea timu kushindwa kutengeneza build up ya goli. Hiyo rekodi ya kutofungwa mbona haijibu swali?
 
Hivi upo serious kusema Fernandes ni mkali and he is second to Kevin? Bernardo Silva anacheza cricket?

Huyu jamaa siyo mbaya ila kazidiwa na wachezaji wengine isipokua anachokifanya hakijaonwa na mashabiki wa man u kwa muda mkubwa so anatukuzwa kama lulu.

Formation ya 4 2 3 1 ambayo imeanza kutumika ili kumpa nafasi Donny ikiendelea kutumika Bruno ataanza kuonekana miyeyusho. Mpaka mje kuizoea ushindi mfululizo unaousema utakua outta window.
 
★Acha tuone ulicho kisema Mkuu★
 
Hizi stats muhimu za kiungo mshambuliaji

1. Magoli
Bruno nusu msimu 8
Bernado msimu mzima 6

2. Assist
Bruno nusu msimu 7
Silva msimu mzima 7

3. Key passes
Bruno average 2.1
Silva Aveeage 1.5

4. Mashuti golini
Bruno average 3.5
Silva ni 1.5 tu

5. Dribble
Bruno average 1.8
Silva ni 1.2

Stats zote zinazohusu ushambuliaji Bruno by far ni zaidi ya Bernado.

Ukija ukabaji
1.tackle
Bruno 1.6 average
Silva ni 1.1

2. Interception
Bruno ni 0.8
Silva 0.7

3. Clearence
Bruno 1
Silva 0.1

Hata kwenye ukabaji by far bruno ni mchezaji mzuri.

Tumalizie na usambazaji upendo
1. Idadi ya pasi kwa mechi average
Bruno 55
Silva 40

2. Pass accuracy
Bruno 75%
Silva 90%

3. Crosses
Bruno 1
Silva 0.5

Katika vigezo 11 hapo juu bruno kashinda 10 na silva kimoja tu, bado tu unaaamini silva ni zaidi ya fernandez?

Naweka na source usije ukadhani nimetoa kichwani
https://www.whoscored.com/Players/123761/History/Bruno-Fernandes

https://www.whoscored.com/Players/136741/History/Bernardo-Silva
 
'WAZZA' ALIWASHA JUA, SIKU DUNIA INASUBIRI MVUA.
.
Ni mzunguko wa 24 wa ligi, Arsenal wamezigeuza timu zote za epl jaa, kila mtu anatupa taka zake anavojisikia. Wanajipigia tu wanavotaka. Si Manchester United, Chelsea wala Liverpool zilizofua dafu mbele yao. Walienda hadi michezo 30 ya ligi bila kufungwa. Utawaambia nini wakati wana Patrice Vierra katikati, Thierry Henry na Denis Berkgamp dimbani. Utawaambia nini Arsenal?
.
Siku hiyo Arsenal wapo Goodison Park, Everton wamekomaa. Wamegoma kufungua njia. Wanaomba Mungu wapate sare tu mbele ya Arsenal hii inayoitetemesha dunia. Kumbuka hapo ni October 2002, Arsenal hawakumbuki mara ya mwisho waliyopoteza mechi. Hawakumbuki!
.
Siku hiyo wakati wanafikiria kufikia mchezo wa 31, 'mswedish' Freddie Ljunberg aliwatanguliza Arsenal mapema tu kabla hawajaenda mapumziko. Mashabiki wa Arsenal jukwaani hata hawakushangilia, kwao ilikuwa kawaida tu. Kuongoza dhidi ya Everton? Kawaida tu yaani.
.
Walirejea kipindi cha pili Tomasz Radzinski kimiujiza aliwasawazishia Everton. Bado mashabiki wa Arsenal hawakushtuka. Walijua ni suala la muda tu kabla hawajashinda. Hata wangepata sare isingewaumiza. Walichojua ni kuwa, hawawezi kupoteza.
.
Zikiwa zimesalia dakika 10 mchezo kumalizika, David Moyes alimnyanyua Wayne Rooney na kumuambia "twende ukatupe bao la ushindi." Rooney hakumjibu, alikuwa amenuna sana. Alishaanza mechi za nyuma, isitoshe alifanya vizuri sana. Kwanini leo alimchelewesha hivi?
.
Alishamuambia Moyes kuwa anataka kufunga bao lake la kwanza la epl kabla hajatimiza miaka 17. Kufikia hii mechi ya leo alikuwa amebakiza siku tano kabla ya kufikisha miaka 17. Kwanini leo hakumuanzisha ili atimize ndoto zake?
.
Wakati anaingia kaka yake wa mpira, David Unsworth alimuambia "usiogope mdogo wangu, utakuwa mchezaji mkubwa sana duniani hata kama hutafunga kabla ya 17 kama ulivotaka". HAKUJUA kama bwana mdogo alikuwa na mawazo tofauti.
.
Wakati mechi inaisha, ipo magharibi ya roho Rooney aliitangazia dunia ujio wake kama unavoona hapo juu. 'WAYNE ROONEY REMEMBER THE NAME" Ilikuwa sauti ya mtangazaji akiitaka dunia ilikumbuke jina la huyu mtoto. Kilichofuata? Tunakijua.
 
Huyo anajua ila ana troll tu.
 
I am very optimistic,I agree with you.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…