Mentor
JF-Expert Member
- Oct 14, 2008
- 20,334
- 23,940
Chifu, upo ngazi ama unanusanusa maji machafu? Maana ni kama huelewi ninachokisema na unachokiandika.Anyway, ngoja nikueleweshe.Wewe ulianza kwa kukejeli kichwa cha uzi kwamba, siku Man United sio tena hatushikiki bali tunashikika sana.Mimi nikakwambia, pamoja na hilo ulilolisema, United ndiyo tunaenda kuwa mabingwa wa EPL kwa mara ya 20.Wewe ukaja na stori kwamba,ubingwa siyo ishu, kinachoangalia ni rekodi ya game to game (kumbuka chanzo ni matokeo ya juzi dhidi ya City). Na baadaye ukaja na kusema kwamba kwa rekodi hiyo, Chelsea na City waliifanya United vibaya na hivyo kupelekea Uingereza nzima kuwa bluu.Mimi nikakuuliza, kwani umesahau matokeo ya awali ya msimu huu? Nikianza na City, nikasema: City tuliwapiga kwao 3-2 kwa RvP kufunga bao ushindi kwa freekick katika dakika za mwisho mwisho. Hivyo tukienda kwa mtazamo wa game to game, United tunaibuka kidedea kwa goli la ugenini, kwao wao City walitufunga 2-1 pale OT. Sasa hapo ubluu unatokea wapi? Kumbuka na bado tunaongoza ligi kwa pointi 12 zaidi ya City!!Nikaenda kwenye upande wa Chelsea, nikasema: Chelsea tuliwafunga 3-2 pale darajani (tarehe 28 Oktoba 2012) katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi, na goli la Chicharito katika dakika ya 75. Na game ya mzunguko wa pili ndiyo inapigwa tarehe 4 ya Mei pale OT. Sasa huo ubluu unatokea wapi?Kwa maana ukija na mtazamo wa game to game, bado Chelsea na City kwa United ni nyanya msimu huu. Pia ukija na mtazamo wa historia, bado timu hizo ni nyanya kwa United.Ukija kwa mtazamo wa wingi wa mashabiki na wapenzi, timu hizo zinaendelea kuwa nyanya.Hata kwa mtazamo wa utajiri wa klabu, bado mnaendelea kuwa nyanya.Hata kwa rekodi katika EPL, UCL, FA, World Clubs etc. bado timu hizo ni nyanya kwa United.Vile vile hata kwa ubora wa timu katika Ulaya (United ni ya 4 baada ya Barcelona, Real Madrid na Bayern Munchen), bado timu hizo ni nyanya.Sasa huo ubluu katika Uingereza nzima unatokea wapi? Chifu, hizo timu zenu huwezi kuziweka daraja moja na United; hizo bado ni timu ndogo sana - wee clubs - katika kila kitu kwenye soka.
Mkuu, You do not respond to a mosquito bite with a hammer man!!!
I was referring to your current run of games...between nyie na sisi na man city!!!
Umeenda mbaaali..ni kweli nyie ndo mabingwa wa EPL kwa mara nyingine ya 20 msimu huu ila haitoshi kuacha kukutania mkifungwa maana ni aibu kwa timu uisemayo siyo ya level yetu kufungwa na timu ya level yako!!! khe khe kheeee...
Again...bila kuangalia ligi gani mmecheza..basi kwa msimu huu mmekuwa 'nyanya' wetu zaidi maana it can easily be concluded kwamba ile first round was a simple fluke!!!