Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu narudia tena hii mechi ilikuwa nyepesi kwetu isipokuwa kocha ndiyo kautia ugumu mchezo wa jana, hayo yote uliyoyaandika ni kweli kwamba walikabia juu na walitupa presha lkn hayo yote kayataka kocha kwa kuwapa wachezaji presha zisizokuwa na msingi wowote, ww una pogba una Matic una Bruno zen unawaruhusu vp watoto wadogo wautawale mchezo? Kamshusha Matic chini akawa km beki 5 pogba kamshusha namba 6 icyopanda, mda wote pogba alikuwa nyuma havuki mstari wa kati hapo unategemea kumuona Greenwood? Mipira haifiki mbele utamuona vp Bruno, ofcz jana hata bissaka hakuwa vzr kivile mda mwingi alikuwa anakosea kosea lkn hyo yote alitaka kocha kwa approach yake ya kukaba, mbinu nzr ya kukaba ni kumiliki mpira ss yeye kawatia presha wachezaji mapema unategemea nini hapo? Alipaswa kuwaambia chezeni mpira bila kuangalia historia cz man u ni tm kubwa kuliko Soton, hapo lazima wachezaji wange relax mpira wangeucheza lkn yy kaanza kuwatia hofu matokeo yake wachezaji wakawa wanawaza top 3 kuliko mechi yenyewe.
 
Watu wanapigiwa pira lile home ground utasema wao ndio midtable team dah,,,
kuna haja next season mupewe jezi za njano,









Hii United hii ?au UTOPOLO ...UJINGA HUU BWANA
 
Hapa Palace wanahitaji miujiza kuiharibia United kwenye mbio zake za top 3

Hawa Palace wamepigwa mfululizo na Liver, Burnley, Leicester, Chelsea, Villa (ndio ni Villa ya Samata, tena 2-0), kwa hiyo current form ya Palace United wakiruhusu kuvurugiwa nao itakuwa wamedhihirisha mbio za top 4 ni mbio za wanyonge.

Mechi ngumu kwa mtazamo wangu bado ni Leicester, na hii watu hawaitaji. Pamoja na kwamba current form yao ni mbaya, lakini watakapokutana na United watakuwa motivated zaidi, maana United kwao ni direct rival on top 4 spot.

Kwangu kama shabiki wa United kitu kinachonipa kiburi kuhusu Leicester ni kiwango chao duni walichoonesha hivi karibuni na kitendo cha kutokuwa na huduma ya James Madison na Soyuncu (mechi ya Villa alikula umeme) vinginevyo, wao wana timu nzuri na kocha mzuri kuliko Palace na Westham.

Kwa mtazamo wangu, win percentage ya Man Utd kwenye game zilizobaki, Man Utd vs Palace (70% kwa 30%), Man Utd vs Westham (70% kwa 30%) na Man Utd vs Leicester (60% kwa 40%)

Ila game yenu dhidi ya Crystal Palace ndiye mwamuzi mkubwa, mkishinda hiyo nina uhakika top 4 mnaingia.

Maana mna game na Leicester ambao kwa sasa wanafungika.

Leicester ana game na Sheffield, Tottenham and then Man United.

Hatoboi.
 
Wale Southampton wanaitwa "The Saints" maana yake Watakatifu wa Bwana"
Na nyie mnaitwa "Red Devils" maana yake Mashetani wekundu
Tatizo ni mashetani walicheza na watakatifu
Tangu lini Shetani akamshinda Mtakatifu wa Bwana?
 
Mmepewa nafasi nyingine, wenzetu wanaitwa second chance, ya ku screenshot msimamo, tumia nafasi hiyo vizuri mkuu

Ukichelewa mpaka ifike Julai 22 utakuwa umechelewa mazima
Mkuu hiyo imeisha sahauni nafasi ya tatu labda mbadilishe mawazo muanze kufikiri nafasi ya 4
 
Kabisa Mason jana hakuwa mchezoni kabisa na mwenzake Pogba, ila OG aliamua kubet Fred nae kaingia akapotezwa hakuwa na msaada. Pongezi ziende kwa Saints walitu outsmart , walikuwa bora sana kipindi cha pili.



Ggmu
 
Sotton walicheza vizuri zaidi yetu kwenye umiliki wa mpira, lakini sisi tulicheza vizuri kwenye kutengeneza nafasi, kosa kubwa tulilofanya ni kushindwa kutumia nafasi tulizopata.

Pressing ya Sotton ilitufanya tuwe suffocated, lakini pia Mungu alikuwa upande wao, kwa namna walivyo press walicheza rafu nyingi sana ambazo wangemaliza mechi wakiwa pungufu kwa red card nisingeshangaa

Greenwood kutoonekana. Kitu walichofanya ni bullying kwake, kila alipo pata mpira alizungukwa na wachezaji wa Sotton 3 hadi 4, pia walifika sana miguuni make, Romeu ana bahati sana, alipaswa kupigwa red card kwa rafu mbaya aliyomchezea Greenwood.

OGS ana mapungufu yake, hapa ndipo huwa nina mu admire Jose katika kupata matokeo. Timu inaongoza goli 2 - 1, Greenwood amebanwa sana, kwani usimtoe yeye halafu ukamwingiza Tominay, ili Tominay au Fernandez mmoja acheze namba 7 lakini tunapokuwa hatuna mpira acheze katikati ambapo Sotton walitawala? Ukiwa na Fred, Tominay na Fernandez kwenye kulinda ushindi wako ni bora kuliko ukiwa na James, Fred na Tominay.

 
Kushindwa kuhandle pressure na poor management of the game from Ole ndo kilichofanya kupoteze zile point mbili

✓Matic kucheza kama centre half huku Pogba akicheza nyuma sana lilikuwa kosa

✓Angetoka Greenwood na kuingia kiungo (Scot au Fred) tungeendelea poa tu naamini..Pogba na Bruno wangeendelea atleast tungefanya kitu,japo kuwa walikuwa wamechoka kimtindo

✓Kwanini hakufanya Sub ya Brandon?..angeingia ata Bailly

AWB kuna namna ubora wako umecompromise..Anacheza vibaya sana

Martial hizi mechi mbili amepambana sana..That's what we want to see from him..Pure talent


Top four race bado haijaisha na tuendelea kushinda game zilizobaki
 
Baada ya Brandon kuumia, hakuingia mtu sub ziliisha nadhani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…