Ushaanza kumpamba sasa OGS Bado ana muda wakujipanga Kurejesha Furaha ilopotea pale OT katuangusha Mechi ngapi mpaka unaanza kumpa sifa kama hizo.
mechi 10 zilizopita OLE na benchi lake la ufundi wamejirekebisha sana kutokana na makosa waliokuwa wakiyafanya mara kwa mara hususani kwenye mechi ndogo.
wakati ligi kuu ya uingereza inaanza (mechi dhidi ya chelsea) eneo la kiungo alikuwepo
nemanja matic pamoja na
juan mata lakini hao wote walianzia benchi ili kutoa nafasi kwa mmoja wao (kati ya
jesse lingard au
andreas perreira)
mechi nne za mwanzo Ole alikuwa analazimisha paul pogba acheze chini (namba 8) zaidi pamoja na
scott mctominay nafasi ambayo ulikuwepo uwezekano wa kumtumia nemanja matic then paul pogba acheze namba 10 au juan mata, kinyume chake alikuwa anamtumia andreas perreira au jesse lingard.
baadae paul pogba akapata majeruhi, kuumia kwa pogba pia ndio ulikuwa mwanzo wa fred kurudi kwenye kikosi baada ya harusi na ishu nyenginezo (match fitness) na ilikuwa ni mechi ya 5 kama nitakuwa nipo sahihi, cha ajabu ole akaendeleza tabia ile ile ya kumbeba perreira na lingard na hatimaye fred akaendelea kukaa benchi.
mechi ya arsenal paul pogba akarudi tena kwenye kikosi cha kwanza baada ya kupona majeruhi, OLE na benchi lake la ufundi wakaendelea kulazimisha
jesse lingard na
andreas wawemo kwenye kikosi cha kwanza huku benchi letu wakiwepo
juan mata, fred na
nemanja matic ambao hao wote wana ubora mkubwa kuliko wawili hao
mechi iliofuata tunapoteza dhidi ya newcastle united na kwa mara nyengine tena andres perreira anacheza mbele ya nemanja matic, kwa ufupi mpaka tunafika mwezi oktoba hakuna hata mechi moja ambayo OLE na benchi lake la ufundi waliacha kuwatumia andreas perreira au jesse lingard kwenye kikosi cha kwanza, baadae matic na paul pogba wakapata injury.
nilichojifunza ni kwamba tokea mwanzo (dirisha kubwa la usajili) bwana ole alishaweka akili yake kwa wachezaji wawili (andreas perreira na jesse lingard) waongoze jahazi la kiungo mshambuliaji ndio maana paul pogba akashushwa chini zaidi, ila baada ya kuona wachezaji hao wameshindwa kufikia matarajio makubwa aliyoyaweka kupitia wachezaji hao na paul pogba kuendelea kuwa majeruhi ndipo alipoamua dirisha dogo la usajili amrudie
bruno fernandez.
sasa jiulize tokea bruno fernandez asajiliwe hao wahuni wawili wameanza mechi ngapi?
bado naamini zile mechi tulizopoteza point kizembe dhidi ya timu ndogo kama tungelianza na midfield ya pogba, mata, scott na matic/ fred tungelipata ushindi.