Liverpool mechi nyingi wamesaidiwa kushinda na idara zingine katika timu siyo striker tu.
1 game na Leceister walishinda kwa msaada wa midfield
2 kuna game walishinda magoli yote yakifungwa na Van Dijk
3 Mechi na Aston villa walishinda kwa magoli ya kutoka kwa Robertson na Sadio Mane.
4 Mechi na Man united walisawazisha kwa goli la Lallana Midfielder
Ukiangalia timu yetu idara ya ulinzi kama imefunga goli katika mechi zote tulizocheza hayazidi mawili goli la William's na Lindelof
Idara ya kiungo naangalia naona goli la Pereira na Mctominay, tofauti na hapo magoli yote yamefungwa na strikers wetu.
Siyo mechi zote striker anaweza kufunga kuna mechi zingine hautakuwa form hivyo idara zingine zinafill hilo gape.
Mpaka sasa striking force yetu imejitahidi sana kwanza kulingana na nafasi chache za kufunga magoli tunazotengeneza.
Mechi yetu na Everton tulitengeneza nafasi chache za kufunga lakini hatukuweza kuzitumia, lakini nafasi hizo nyingi walizipata ni midfielders na defenders baada ya strikers wetu kuwa marked sana.
Tusiligeuza jukumu la kufunga uwanjani kama ni la kwao pekee wachezaji wetu wa idara zingine lazima watambue wajibu wao wakufunga zinapopatikana nafasi pia.
Sent using
Jamii Forums mobile app