Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Umevurugwa na avatar yako.
Ukweli ni kwamba EPL mnashinda game 1 kila mwezi ,sasa uniambie mwezi mlioshinda game 2 ,msema kweli mpenzi wa Mungu ,kwa kuwa mwezi huu game ziko saba mtashinda 2 ,moja tayari bado moja kwenye game Tano
 
Jibu swal langu,
Kwa mtazamo wako, Sosha n mtu sahihi ktk hiz jitiada za kuirudisha utd glory days au bodi itafute kocha mwingne?
 
Kumkosa Pogba imetu'cost sana, kiufupi timu haija'balance, tunaitaji left back, creative midfilder, striker no 9
Sometimes nashindwa mlaumu Sosha, apewe madirisha mawil zaid kujenga timu japo uchanga wake uwa unatugharimu baadh ya mechi
 
Jibu swal langu,
Kwa mtazamo wako, Sosha n mtu sahihi ktk hiz jitiada za kuirudisha utd glory days au bodi itafute kocha mwingne?
Ni sahahi tena sana,kitu usichojua ni kikosi ndiyo kina mtupa mkono ila angalia game na utaelewa,kazi iliyobakia ni usajili wa baadhi ya namba mfano 10 haipo pia 9 bado ni mchanga ukilinganisha na Firmino,Lacazet,Aguero/Jesus,Vardy na Jimenez pia tunaitaji kiungo mwenye uwezo binafsi na concistency ya kuwa bora angalau mechi 7/10 tofauti na akina Scotty ambao wanachezea kujituma na nguvu(though ndio dogo nnaemkubali Man UTD maana anajituma sana)
 
Tukipata midfielder namba 10 creative, tukapata na striker wawili mmoja awe na uwezo wa kucheza kama second striker kama Piatek wa Ac Milan timu itabalance.

Defence Midfielders wanaanza kuwa vizuri na tunao wawili kinachotakiwa ni kumbakiza Pogba kama box to box midfielder na kupata mwingine atakayekuwa back up ya Pogba.

Left backs kwa sasa tunao watatu hivyo sehemu ya kuongeza ni right back ili Bissaka apate back up hasa tukipata back mwenye uwezo wa kushambulia zaid ya Bissaka.

Sehemu nyingine ni central defenders akiondoka Jones itabidi aongezwe mwingine hasa versatile ili kupunguza workload kwa Maguire na Lindelof.
 
Jana nilikuwa na fraha sana kumuona Scott duh! Hata kama tungeshindwa ila jamaa namkubali hanaga ufala anapambana kupeleka timu mbele.


Maguire jamaa linazingua hapa pa kusubiri huruma za offside badala ya kuact fast linanyosha mkono ndio inaboaga.


Wan Bissaka asee! Jamaa anazingua timu ikiwa moto akipewa ball tunakuwa freezed. Inahitaji wamwambie apambane kwenda mbele tu.



Rashford, yuko poa tatizo la jamaa ubinafsi mwingi ile chance ya dakika ya mwisho hata kama angeona hataki kufunga wape wengine sio kuipoteza kizembe.


Young hua anatoa maboko ila hasahihishi bora Williams akizingua anajaribu kucorrect kwa kupeleka mbele mpira kwa kasi japo goli lipatikane.


All in All jana kipindi cha kwanza ilikuwa moto.
 
Kuna makocha sahihi zaidi ya OGS, hilo ndio ninaloweza kusema

Lakini ukweli unabaki kuwa hard time tunayopitia inasababishwa na mambo mengi na udhaifu wa kocha ni sehemu ndogo ya tatizo kubwa lililopo
Jibu swal langu,
Kwa mtazamo wako, Sosha n mtu sahihi ktk hiz jitiada za kuirudisha utd glory days au bodi itafute kocha mwingne?
 
Kuna makocha sahihi zaidi ya OGS, hilo ndio ninaloweza kusema

Lakini ukweli unabaki kuwa hard time tunayopitia inasababishwa na mambo mengi na udhaifu wa kocha ni sehemu ndogo ya tatizo kubwa lililopo
Umejibu kisiasa ila poa, my opinion OGS apewe madirisha mawil zaid ya kusafisha/new signout timu itarud, falsafa yake ya kuwamini vijana inanikosha na ndio falsafa za utd, hata new signing alizofanya maguire, bissaka n james ni typical utd DNA
LVG n Mou walituulia timu, wamesajir wachezaj wengi kw pesa ndefu wasio msaada ktk timu eg Martial, Sanchez, Bailly, Lukaku, Micktaryan, Depay etc
 
Mkuu sio kisiasa

Tatizo mjadala wa OGS kutosha kuvaa viatu vya u meneja pale tushaujadili sana humu, kwa hiyo sometimes ni ku avoid repeatition.

Pia kuhusu biashara kupewa kipaumbele kuliko mafanikio ya kisoka (hapa wamiliki wa timu na bodi wanahusika) tumeshakitaja sana humu kama chanzo cha kuyumbisha United

Pia structure mbovu ya uongozi inayosababisha watu wasio wa soka kufanya maamuzi ya soka au watu wa soka lakini wapita njia kufanya maamuzi ya soka (kimsingi hapa ni kukosa DoF) . Vyote hivi vimechangia kuyumbisha timu yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…