Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Yaani united ya wakina Cr7, Rooney 10, Berb09 , n.k
Leo tunahusishwa na Zaha ???
Eeeh mungu tusaidie
United yetu inasikitisha sana.. Yaani hadi Arsenal inatuzidi upepo kwenye soko la ulajili.
 
Kwahy alishinikizwa? Dadavua
Hakushinikizwa ila alisoma mambo yanavyoendeshwa akaamua aondoke asuharibu heshima yake.

Maana baada ya SAF kuondoka hata Moyes alisuasua sana kwenye issue ya usajili.

Na juzi kati alisema hakumuhitaji Fellaini ila aliletewa na Ed kilazima.
 
Huyo Zlatani (35) unayemponda, ndio striker aliyefunga Magoli mengi pale United kuliko striker yoyote kwa msimu tangu aondoke Van Persie (29). Na hapo aliumia kabla ya msimu haujaisha

Embu nitajie ni wachezaji wangapi kwenye ligi ya Uingereza waliofunga magoli zaidi ya 29

Zlatan ameondoka, amewaachia vijana nafasi akina Lukaku, Rashford, Martial, wamefunga Magoli mangapi kwa msimu huu, au uliopita. Hakuna cha maana. Angalau hata Lukaku anajitutumua.

Ukiondoa Matic, Sanchez niambie hao wengine wenye umri unaoupendekeza wewe, wameifanyia nini United? Niambie aliyekuwa na 27 alifanya nini, niambie Bailly aliyekuwa na 22 amefanya nini? Vipi kuhusu Pogba (24), Dalot na wengine?

Kwa kigezo chako cha umri, mazingira yakiruhusu usajili Messi (32), Ronaldo (33), Griezeman (28), Aguero n.k utakataa kuwasajili na badala yake utamchukua Odoi, Rashford eti kwa sababu wao ni wadogo? Magoli watakayofunga hao jamaa "wazee" ndani ya misimu 3, itawachukuwa hawa "watoto" pengine carrier yao yote
 
Arsenal wako mbele kumhitaji Zaha.. kuna tetesi wako tayari kutoa wachezaji wawili + pesa ili wamchukue.
Hakim Ziyech pia amesema anapenda kucheza Arsenal na yuko tayari kuondoka pale ajax.
Ziyech aliyasema hayo mwaka 2017, leo ni mwaka 2019

Mick aliwahi kusema anapenda Arsenal, akaanzia United
 
Zlatan msimu wa pili ni kama hakucheza (sidhani kama alianza hata mechi 5)

Kwa hiyo huwezi kum judge kupitia msimu wa 2 ambapo ndio alikuwa ametoka kwenye majeruhi mabaya sana
 
Sijui hapa umetumia kigezo gani

Ila kama usajili wa Van Gaal unasema angalau wachezaji 4 walionesha makeke, usajili wa Jose unamuachaje Pogba, Matic msimu wa kwanza, Zlatan pia
 
Ziyech aliyasema hayo mwaka 2017, leo ni mwaka 2019
Mick aliwahi kusema anapenda Arsenal, akaanzia United
Sawa.. Arsenal wako bize na Zaha lakini ikishindikana wanaweza kumvuta Ziyech sisi tumezubaa mno.
 
Utamuuza Rashford + Lingard hukosi £100M unaongeza £60M unamleta Mbappe.
Man United hawezi kosa hela ya kumleta Mbape, maana kitita pekee atakachokabidhiwa ni kati ya £200m na £250m

Ameambiwa mchezaji akiuzwa hiyo hela itaongezewa kwenye kitita cha manunuzi

Swali ni kwamba, je hao Mbape wapo tayari kuja OT?
 
So far Ole anatupa mashaka, lakini ni mapema sana kum judge kwamba hana uwezo, hana wisdom na blaa blaa nyingine

Tunampa benefit of doupt kwanza
 
Upo sahihi

Unaambiwa Sanchez usajili wake ambao ulifanyika majira ya baridi (msimu usio maarufu kwenye usajili kama summer) uliongelewa zaidi kwenye social media kuliko usajili wa Neyamar wa £199m kwenda PSG

Hivi ndio VITU ambavyo Ed akikaa na ma investors anaviongelea, STUPID
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…