Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hongera mkuu kutubu ni indicator ya ushujaa na wala sio udhaifu
 
Inasemekana Man city wako karibu kabisa kumsaini Bruno Fernandez toka Sporting Lisbon kwa £42m + two players kwenda sporting kwa mkopo au permanent na mmoja wa Wachezaj hao ni Marlos Moreno waliomsaini mwaka 2016 ila ameshindwa kutoboa city.

Lakin Sporting Lisbon wamegoma wao wana demand €70m ambayo ni sawa na £60m. Na Kama kutakuwa na wachezaj wanaokwenda upande wao basi wawe separated from Bruno Fernandez deal.
 
Not only Mou, even Van Gaal.

We didn't know whos behind the failure of these managers.

Sitashangaa kituko atakachofanyiwa Ole.
 
Kinachoniogopesha ni kwamba Ole yupo desperate sana ku manage United

Kwa hiyo ni powerless kwa Ed na Tajiri, nahisi atakuwa Yes Man
Nikimwangalia tu vizuri hata kwenye press zake naona ni Yes man..mpaka sasa ingetakiwa awe anawaacha nyumbani wale wachezaji ambao anaona wanazingua au hawapaswi kuwa united,na awape madogo nafasi na next season tujipange..sasa yeye bado anaimani na hawa wazinguaji..

Hawa ndo atleast inabidi wabaki kama backborne


√De Gea

√Dalot

√Shaw

√Lindelof

√McTominay

√Lukaku

√Pogba(if he want to leave,no problem)

√Fred (Lets give him next season)
 
  • Ole Gunnar Solskjaer in December: "Football is easy if you've got good players! They are a great bunch of players and their quality is unbelievable."
  • Ole Gunnar Solskjaer now: "There's a chance you've seen the last of some players today."
kwa nini damushin nisiwe kama kinyonga?

bila ya kusahau endapo wattford watabeba ubingwa wa FA tutapaswa kugombania EUROPE kuanzia mwezi July
 
Bruno Fernandes scores his 31st goal this season (hattrick), making him the midfielder with most goals scored in a season.
nimeona taarifa majirani zetu tayari wameshaanza harakati za kumsajili huyu mwanadamu, nyakati hizi tunazojiandaa kuishi bila ya herrera tunapaswa tuingize ingizo jiipya kama hili.
kwa heri premier league karibu transfer rumours league
 
Kuna dalili za wazi kabisa kuwa kuna kundi la watu wanaondoshwa united, kijanja sana, na kwa kugeuziwa kibao, Ikumbukwe de gea na pogba wamegoma kuongeza mikataba mipya, de gea akitaka 300,000 na pogba anataka 500,000 kwa wiki, ili kufidia panga la mishahara la msimu ujao sababu united haijafuzu ucl, na united imegoma kuongeza mshahara wanaotaka wachezaji hawa, hata herrera kumpa 150,000 imegoma kabisa, sasa hivi de gea anapewa ultimatum ya wiki moja ya kusaini mkataba bila maboresho anayotaka, maana yake nini?? Pengine kuna salary re-structuring ambayo ilikua ni lazima itokeee kustabilise timu, woodward alivurunda sana hapo awali, pengine anataka kurekebisha makosa, sio mbaya, tusubiri tuone.
 
Mpaka sasa united kama kuna mchezaji Mzuri atakubali kuja ujue atakuwa analipwa mshahara mkubwa sana maana hivi sasa kila mtu anataka kupiga hela za kijinga za man u.

Kwenye transfer kila top talent haina mwelekeo wa kuja united na hata kama ikihitajika extra energy itahitajika hata kupambana na team kama Chelsea au arsenal tu hii ni hatari.

Wachezaji pekee wanaoweza kwenda united ni wale ambao huenda wanaelekea kuzeeka au hawahitajiwi na team nyingine kubwa tofauti na united tumekosea wapi ?

Hao watoto wa benfica na Porto au borrussia kuwamchomoa siyo chini ya mia napo kwa mbinde kweli kweli labda kama tukiamua kufanya vinginevyo tujipe two to three years kwajili ya kujipanga tusajili wachezaji vijana lakini wenye uchu wa mafanikio tunaweza kutoboa.

Hivi scouting department ya man u si tunaambiwa ni kubwa kuliko team nyingine yoyote duniani huwa inafanya kazi gani kuviona vipaji vya maana mpaka inafikia man u kuanzia kupigana vikumbo sokoni wakati inajicho la ziada la kuona vipaji ?

Hawakumuona.
Kylian Mbappe mpaka akanyakuliwa na Psg, hawakumuona mapema Harry Maguire mpaka amefikia pound 70+ hivi hiyo department haijaona replacement ya Phil Jones chris Smalling na Ashley Young mpaka sasa inawaongezea mikataba in their early thirties?

Hivi Ben chilewell hawezi kuwa replacement ya young japo kwa muda tu maana ndiye beki aliyekimbia kilomita nyingi kuliko mwingine EPL!?

Hivi man u ya Leo ni ya kuumizwa kutoingia top four jamani au tuko karne nyingine kama na uelekeo wetu ni kuwa Leeds united nyingine EPL ?
 
mkuu unapaswa unywe maji baadae urudi nyumbani (umemaliza kila kitu), nimebaki najiuliza hivi paundi million 200 zitatosha kweli kwenye usajili au ndio mwendo wa kuuziwa mbuzi wengine waliochoka
 
Kuna uwezekano wa kutokusajili wachezaji wa maana kwa jinsi hali ilivyo.

Labda tukubali kupoteza miaka mingine miwili tukifanya restructuring ya team kwa kusajili wachezaji vijana zaidi na kuresort kwenye academy yetu.

Lakini kinachoniumiza academy ya man recently haijatoa mchezaji akadumu na kiwango chake consistently hata kwa two seasons wengi huja na kupotea tu kama moshi
Yuko wapi Bothwick Jackson, Timoth Fosu mensah, Paul Keane , james Wilson, Joshua Tuanzebe, Adnan Januzaj, etc
mkuu unapaswa unywe maji baadae urudi nyumbani (umemaliza kila kitu), nimebaki najiuliza hivi paundi million 200 zitatosha kweli kwenye usajili au ndio mwendo wa kuuziwa mbuzi wengine waliochoka
 
Ni msimamo mzuri ili kuweka stability ya salary scale kwenye timu

Lakini huu mjadala kuhusu Pogba kuongezewa sijui unatoka wapi

Pogba kuanzia mwezi wa saba, 2019 anakuwa amebakiza miaka 2 ili mkataba wake uishe, na bado klabu ina option ya kuongeza mwaka mmoja ikitaka

Sasa swali la kujiuliza ni kwamba klabu ina presha gani ya kufanya nae mazungumzo ya kumuongeza mkataba
 
mkuu sakata la pogba linaonyesha dhahiri klabu inafaidika zaidi na uwepo wa jamaa nje ya uwanja kimapato ndio maana hawataki kumpoteza kizembe na si kwamba eti hakuna viungo wanaomzidi pogba ambao wanapatikana sokoni kwa wastani wa paundi millioni 60.
si ajabu klabu ikamuongezea mkataba muda huu na mshahara wa paundi laki tano na wakati huo huo wakaendelea kukataa kumpa kandarasi mpya ander herrera.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…