Takribani yamebaki masaa 2 kabla kipute kuanza kupigwa pale Godsonpark, moja kati ya mechi ngumu kwa United lakini pia mechi muhimu sana
Kikosi kikichosafiri kimekwenda bila Ashley Young na Ander Herrera lakini sehemu kubwa ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wamesafiri
Mechi ya leo itakuwa ngumu sana kwetu kwa sababu kadhaa. Kwanza, kwa sababu tupo ugenini, toffees wameonesha wana uwezo wanapokutana na wakubwa, juzi juzi tu Chelsea kisha Arsenal wametolewa kamasi pale Godsonpark.
Kingine kinachiweza kuifanya mechi kuwa ngumu, ni kama OGS hajawaandaa vizuri kisaikolojia wqchezaji, maana siku kadhaa zilizopita tumetoka kupigwa na Barca, hivyo hii inaweza kupunguza confidence yetu, lakini ukweli utabaki kuwa Everton is no where near Barca, ability wise.
Kwa upande wetu tuna uwezo wa kupata matokeo, yaani ushindi. Tukumbuke hii United ndio ile ile iliyoshinda mechi 12 kati ya 14 baada ya OGS kuwasili pale OT. Hivyo hatuna haja ya kuwa na wasiwasi sana.
Pia, fomu yetu nje ya OT sio mbaya kwa hiyo hatuna sababu ya kuihofia Everton (hapa nieleweke haimaanishi OT hatupati ushindi)
Tumalizie na stats
Everton Vs Manchester United
Michezo waliyoshinda 69, Waliyopoteza 88, Waliyodroo 43
Everton nyumbani, kwa miaka 10 iliyopita
Wameshinda 6, Wamepoteza 12, Wamedroo 4
Everton nyumbani, kwa miaka 5 iliyopita
Wameshinda 2, Wamepoteza 7, Wamedroo 2
Tangu Oktoba, 2015 Everton wamepoteza mara 6 na kutoa droo mara 2, hawakupata ushindi wowote
Line up ninayoipendelea (kwa mujibu wa waliosafiri)
Degea, Dalot, Darmian, Smalling, Lindelof,
Fred, Scot, Pogba
Rashford, Lukaku, Martial