Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 21,697
- 32,447
Huyu jamaa kanichekesha sanahivi vyeo unavyonipa ni vikubwa kuliko cv ya vyeo aliokuwa nayo iddi amini dada, nahofia hivi vyeo vitanigeuza tabia zangu na kuwa shetani muandika upumbavu humu ndani.
kama tuna mpango wa kumpa ajira ya moja kwa moja OGS basi si vibaya kuchelewesha upatikanaji wa DOF kwa sababu OGS na benchi lake la ufundi wanaweza kuifanya kazi ipasavyo ya kufanya tathmini ya kikosi chetu huku wakimsubiri DOF achaguliwe mwanzoni mwa msimu, kama OGS ni kocha wa kupita halafu kocha ajaye ndiye mwenye mikakati yote ya usajili basi huu ni muda muafaka wa kumtangaza DOF ili apate kufanya kazi yake ya kufanya tathimini ya kina kwa timu na kuandaa mikakati ya usajili ili kocha ajaye ajuwe wapi pakuanzia.
kama tunamsubiri kocha mpya na DOF wafanye kazi kwa pamoja pindi watakapotangazwa ifikapo mwezi July basi tutakuwa tumepoteza muda wetu bure, ukiziangalia timu kama barcelona, juventus na bayern munich tayari wameshaanza kufanya maandalizi ya msimu ujao kwa kutafuta target zao muhimu wanazozihitaji kwa ajili ya kuimarisha vikosi vyao lakini kiupande wetu bado tunasukumuwa zaidi na ishu ya kocha, tetesi za DOF na tetesi nyingi za wachezaji.
ndivyo ninavyojiaminisha kiupande wangu sijui wewe una mtazamo upi.
kuhusu tetesi za DOF kila siku wagombeaji nafasi wanazidi kumiminika kwa mujibu wa magazeti ya uingereza na hii ni kwa sababu magazeti wameshaona fursa ya kupiga hela ila mwenye maamuzi ya mwisho ni ed woodward na mabosi wake.
wapo wengi lakini nimempenda Sven Mislintat kwa jicho lake kali akifanya kazi kama recruitment pale dortmund akiwa pamoja na director michael zorc na hata arsenal pia alifanya kazi nzuri kabla ya kuondoka miezi michache iliopita.
- Jordi Cruyff = ana ukaribu sana na OGS
- Tony Whelan, John Murtagh, Matt Judge : wote wamefanya kazi manchester united.
- eric cantona
- Sven Mislintat
- monchi
mara nyingi nafuatilia thread hii kwa ajili ya kufuatilia hii ishu na kupata kusoma michango ya wadau mbali mbali.
Man Utd set to appoint Director of Football | Expected before next manager hired
Manchester United Forum
View attachment 1023396
Sent using Jamii Forums mobile app