Hebu nipe mambo makuu matano ambayo ameyafanya Hazard na team ya Chelsea iko vibaya.
Halafu naomba uniwekee orodha ya mashabiki wa Chelsea wanaohitaji hazard auzwe. Labda watakuwa mashabiki wa ileje huko ila shabiki anaetumia medula yake vizuri hawezi thubutu kuinua mdomo wake na kusema kiumbe huyo kutoka Belgium auzwe. Labda akili za Mpuuzi Mou ndio zinaweza kufanya maamuzi hayo ya kipuuzi.
Hebu cheki hizo takwimu za hazard halafu usikie kuna mpuuzi anataka kumuuza kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu.
Niliwahi sema humu kuwa Njia pekee ya kiburi cha kocha yoyote kufanya maamuzi kama ya kumuweka mtu kama Pogba benchi ni KUSHINDA TU. Maamuzi yako yataoneka ya maana kama ukiwa unashinda Baaaaaasi, ila ukiwa na maamuzi ya hovyo na matokeo hupati lazima utimuliwe.
Hivi unamkumbuka Haya Toure unadhani Man city wangekuwa wanafungwa kama Manchester , wale Die hard fans wa City wangekuwa wanamuonaje Gurdiola kwa maamuzi yake Magumu ya Kumuuza Nguli hili la soka kutoka Ivory Coast. Lazima angepigwa chini ila matokeo ya uwanjani yamembeba Guardiola. Same situation anayopitia Sergio Aguero. Hivi ni vitu anavyokosa mou; ana mabifu na wachezaji halafu hana lolote kimbinu na team inaishia kuwa na Goal difference 0 yaani sifuri. Halafu MTU mzima Kama wewe huoni ni Jambo la Kishetani team yenye hadhi kama united mpaka msimu wa xmass kuwa na 0 goal difference.
Halafu acheni kukaririshwa, Amini nakwambia Ferguson kama angekuwa mpaka Leo asingekuwa na jeuri ile ya kuuza watu hovyo. Zamani ulikuwa ukiangalia duniani unakutana na lundo la washambuliaji. Leo pitia pitia ligi zote uone natural namba 9 ni wangapi??... Hapo Manchester tu asilimia 50 ya mabeki sio natural defenders unadhani kipi kimefanya hivyo na usajiri ulikuwa unafanywa kama kawaida.
Ashely Young ni namba tatu ila kiasili ni winger. Valencia kiasili ni namba 7 ila Leo ni namba 2. Unajua sababu ni nini????
View attachment 974531