Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Jose Mourinho at Man Utd:

- Win percentage: 58.3%

Mauricio Pochettino at Spurs:

- Win percentage: 56.4%

Jurgen Klopp at Liverpool:

- Win percentage: 54.7%
Kilichomuondoa Mourinho MUFC siyo performance ya kushinda. Kilichomuondoa kwanza kabisa ni kwenda kinyume cha culture ya MUFC attacking football siyo kupaki basi. Pili morali ya wachezaji haipo hivyo ameshindwa kucontrol timu. Tatu form ya uchezaji ni ya ovyo kupindukia na hakuna dalili za mabadiliko.
 
Bonge la point.
 
Hata klopp aliichukua liverpool mwez wa 12 nakumbuka sana
 
Sasa ndio ana suggest aje Bruce au Hughes?

Is he serious? Na wewe mkuu upo serious kweli

Na kwa sasa hivi, katikati ya msimu utampata wapi kocha wa kuipeleka United mbele? Usimtaje Zidane, maana alikuwepo at a right place, at a right time, with right players. Na isitoshe Zidane naye ni wale makocha ambao mechi ngumu wanazi approach kama Mourinho (defensive)
 
Zizou hawezi pewa timu

Ndio maana anatafutwa kocha wa mpito mpaka summer

Zizou ni free agent, ingekuwa wanamtaka yeye, kusingekuwa na haja ya kutafuta kocha wa mpito
 

Am I serious?

Are you serious?

Umesoma nilichoandika?

Hao kina Hughes umeona nimewataja wapi?

Ninaungana na yeye kwa kile tu nilichoandika.
 
Manchester United imemtangaza aliyekuwa mshambuliaji wake wa zamani raia wa Norway, Ole Gunnar Solskjaer kuwa kaimu kocha mkuu wa klabu hiyo kumrithi Jose Mourinho.

Klabu hiyo jana asubuhi ilimfukuza kazi Mourinho baada ya kuiongoza kwa karibu miaka miwili ambapo alianza vizuri lakini baadaye mambo yalibadilika na msimu huu alikuwa katika kipindi kigumu akipata.

Taarifa za kuteuliwa kwa Solskjaer, zilithibitishwa na tovuti ya klabu hiyo yenye maskani yake Old Trafford lakini hakukuwa na maelezo yoyote zaidi ya ufafanuzi.

Solskjaer mwenye miaka 45, aliifungia Man United mabao 126 katika misimu 11 aliyoitumikia chini ya kocha Sir Alex Ferguson.

Kabla ya kuteuliwa kuinoa Man United, Solskjaer alikuwa akiinoa klabu ya Molde ya nchini Norway kuanzia mwaka 2015 hadi Machi mwaka huu alipojiweka kando lakini akaombwa na kuridhia kusaini mkataba mpya mwanzoni mwa mwezi huu.

Waziri Mkuu wa Norway, Erna Solberg, amempongeza nguli huyo wa soka akisema uteuzi wake kuinoa klabu hiyo maarufu duniani kote ni heshima kwa Taifa.

Solskjaer mfungaji wa bao lililoipa Man United taji la Ligi Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich mwaka 1999, mechi yake ya kwanza akiwa kocha itakuwa Jumamosi hii dhidi ya Cardiff City.

Iwapo atafanikiwa kufanya vizuri katika mechi atakazoiongoza Man United, pengine akathibitishwa kuwa kocha wa kudumu wa timu hiyo ambayo imepanga kumtangaza kocha wa kudumu baada ya kumalizika kwa msimu huu.

Akiwa mchezaji wa Man United, alitwaa mataji sita ya Ligi Kuu England, mawili ya FA na lile la Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Anatwaa mikoba hiyo wakati Man United ipo nafasi ya sita katika msimamo ikiwa na pointi 26, ambazo ni 19 nyuma ya vinara Liverpool ambayo Jumapili iliyopita iliwalaza kwa mabao 3-1 ambayo yalichangia kwa kiasi kikubwa kutimuliwa kwa Mourinho.
 
Kitu ulichokisema na alicho kiandika yeye nimebakia nacheka tu
Yeye ameandika hicho alichoandika, amechagua baadhi ya maneno ya Fletcher aliyoongea kwenye hiyo hoja ya kocha wa mpito

Lakini Fletcher hakuishia kuongea hayo, alisema pia anaona watu gani ni sahihi kuoewa timu ambapo alimtaja Hughes au Steve Bruce ndio wapewe timu

Sasa sijui cha kuchekesha hapo ni kitu gani

Unaposema inabidi ateuliwe kocha wa moja kwa moja, kwa sasa ni kocha gani bora ambaye yupo sokoni/hayupo kibaruani? Mwisho wa siku timu itateua tena kocha ilimradi halafu baada ya miezi 10 watu waanze kusema afukuzwe
 
"HATA MAJIVU YA MWILI WA BILL SHANKLY YALIKUSANYIKA TENA"

Usiku mmoja wa saa 00.30 Usiku wa tarehe 29.09.1981 kwenye hospitali ya Broadgreen iliyopo Jiji la Liverpool ilitoka taarifa Baba wa klabu ya Liverpool FC amefariki dunia.
Siyo mwingine ni Bill Shankly.. Liverpool ni Bill Shankly na Shankly ni Liverpool FC. Ndani ya miaka 15 aliyofanya kazi Kama mkufunzi mkuu wa timu ya Liverpool FC aliitengenezea misingi migumu na imara ambayo hata sasaivi bado inaishi.

Ndani ya uwanja wa Anfield hairuhusiwi mechi yeyote kuanza mpaka walevi wao watakapomaliza sala yao takatifu ya wimbo wa "U Will Never Walk Alone ",Ndani ya Anflied Kuna jukwaa maalumu linaitwa "The Kop End" ambalo linanuka marashi ya majivu ya mwili wa marehemu Bill Shankly.

Yapo mengi Achana na uwepo wa kibao cha "THIS IS ANFIELD, Achana na uwepo wa kiwanja cha MELWOOD ambacho Shankly mwenyewe alikuwa anaamini hapo ndipo mahali maalumu kwa ajili ya "Askofu" mkuu kuandalia muongozo wa ibada.

Kwanini hata majivu ya Bill Shankly yalikusanyika tena?

Jibu ni Kiwango kitakatifu kilichooneshwa na Liverpool FC siku ya jumapili ya tarehe 16.12.2018 kwenye ardhi takatifu ya Anfield.
Niliingalia jinsi timu ya Manchester united ilivyonyanyasika chini ya mikono ya mjerumani Jurgen Klopp ,nikaangalia kwenye jukwaa flani la V.I.P nikaiona sura ya Sir Alex Ferguson imekuwa nyekundu huku akitingisha kichwa kwa ishara ya kusikitika .
Nikasafiri mpaka kwenye jukwaa wanaokaa watu maalumu waliokulia Liverpool FC na kukutana na sura ya Sir King Kenny Daglish Nikaona jinsi anavyotabasamu kwa furaha baada ya mechi kuisha.

Hiyo Ndiyo Liverpool FC ambayo marehemu Bill Shankly aliijenga na kuagiza siku akifa mwili wake uchomwe moto na majivu yake kusambazwa kwenye jukwaa la The Kop End, hiyo Ndiyo Liverpool ambayo Steven Gerrard ameagiza siku akifa mwili wake usipelekwe mortuary bali ukawekwe katikati ya kiwanja cha Anfield.

Siku zote kwenye maisha yake fundi Bill Shankly alikuwa anaamini ni laana kubwa Sana Liverpool FC kuwa chini ya Manchester United au Evarton na Ndiyo maana akaja na usemi usemao "In Liverpool city there only two best teams and those teams are Liverpool FC and Liverpool Reserves "

Anachofanya saivi Jurgen Klopp ni kurudi kwenye misingi ya Bill Shankly ambapo alikuwa akiamini katika mambo makuu mawili ambayo ni umuhimu wa mchezaji kufahamu kwanini kavaa jezi ya Liverpool FC na mchezaji anatakiwa kufahamu Melwood ni uwanja wa vita wa wajerumani.

Yapo mengi ya kuwasimulia wadogo zangu ambao hawaijui Liverpool FC zaidi ya kuijua kwenye makundi ya Whatsap na kwenye Odds za kubet, lakini ninachoamini siku ya Jumapili majivu ya mwili wa Bill Shankly yalikusanyika kwa furaha kutokana na mateso waliyopitia Manchester United kwa dakika 90.

Ni Nadra Sana kwa Mtukutu Kama Jose Morinho kwenda kwenye "Post Match Press Conference " na kukiri mbele ya vyombo vya habari kuwa alipitia mateso makubwa Sana kwenye ardhi ya adui.. Ila jumapili Morinho alikiri kupitia mateso makubwa sana na kukiri kuwa ilikuwa ni mechi ya mbingu na ardhi.

Kwa heshima ya jumapili naamini Billy Shankly kabakiza deni moja kwa Jurgen Kloop ambalo ni kuwapa Kombe Liverpool FC.
Hiyo Ndiyo Liverpool FC ambayo watoto wasioijua Liverpool FC wakawa wanakesha mitandaoni wakipiga porojo kuwa Napoli anaenda kuwatoa Liverpool FC kwenye UEFA Champion League , hiyo ndiyo Liverpool ambayo Pep Gurdiola anasema anapenda kusoma vitabu lakini kila akiiwaza anaacha kusoma kitabu, hiyo ndiyo Liverpool ambayo mwaka 1997 kuliwekwa Jukwaa la Bill Shankly nje ya jukwaa la the Kop End kuwakumbusha wachezaji shujaa huyo.

Wanaoweza kujua vizuri kuwa majivu ya Bill Shankly yalikusanyika tena Anfield kwa furaha ni Marehemu Bob Paisley, Joe Fagan na Renben Bennett.

Hiyo Ndiyo Liverpool ambayo iliamua kutoa misa takatifu kwa Manchester United na Kunikumbusha Liverpool ya akina Phil Neal, Alan Hansen na Ian Rush.

Kilichotokea Jumapili ni Liverpool FC kuipa Manchester United PENZI la Ghetto ambalo Kanye West anampa Kim Kardashian.. Kama Hujui Penzi la ghetto tafuta video ya Kanye West na Kim Kardashian wakiwa Ikulu ya Uganda kwa Yoweri Kaguta Museven.

Ashante Jurgen Kloop kwa kusababisha majivu ya Bill William Obe Shankly kukusanyika kwa Mara nyingine ndani ya ardhi tukufu ya Anfield

Montelo 10

Kapumzike Mourinho nenda Inter Milan ukamalizie ufalme wako ulioshindwa kusimama OT, najua team pinzani hazitamani kukutana na Liverpool kwa sasa duh noma sana
 
Kuna uwezako mkubwa Bwana Baby Face akafanikiwa kwa kiasi chake, kwasababu anauzoefu mkumbwa na baadhi ya wachezaji tangu wakiwa wadogo, haswa huyo Paul Pogba, na taticts zake hazina utofauti na zile za Babu Fergie,Kutakuwa na mabadiliko makubwa katika chumba cha kubadilishia nguo.
 
MTU yuleyule ID tofauti ,


Nina Uhakika huyu ni yule Pro Mourinho mkuu katika Uzi huu.



Hahaha nasubiri jiwe limzabe mtu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…