Mourinho ndiye kocha bora duniani. Ni aibu kubwa sana watu kama Bout na Ed Woodward wanamfundisha Mourinho namna ya kucheza na kusajili. Mourinho mpeleke hata PSV atabeba ubingwa. Mou ameikuta United nafasi ya 6. Msimu wa kwanza kabeba
Yuropa, Ngao ya Jamii, Carling Cup
Tuambieni basi ni kocha gani msimu wa 2017 ambaye alivaa medali tatu hata kama ni za mbuzi?
Msimu wa pili kamaliza na alama nyingi kuliko klabu yeyote ispokuwa Man City. Yaani ndani ya miaka miwili amecheza fainali 5 tofauti, CARLINGA, CA, YUROPA, FA na UEFA super cup ni kocha yupi England basi mwenye ubavu huo?? Mbona Ferguson alikaa misimu mitatu bila ubingwa tena akimaliza nafasi ya 3 mara mbili mfululizo akiwa na kikosi bora kabisa duniani kuanzia 2003 mpaka 2006 kwanini wa Mou imekuwa nongwa? Au kisa sio Muingereza mwenzao?
ED alimfukuza Van Gaal chini kwa chini leo nasikia wamepanga ujinga wao sebuleni wameshtukiwa wameanza kukanusha... ED ndo anapaswa kuondoka sio MOU. UNAFIKI UACHWE NAWAAMBIA. MOU NTAMKUBALI POPOTE ATAPOENDA KUFUNDSHA SOKA. FULLSTOP.