Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kuna mahali nimeona wamepiga kura nani aondoke kati ya Mou au Pogba. Asilimia 60 wanataka Pogba afurumushwe.
Ona watu wanavyocharuka mkuu

Screenshot_20181002-082129.jpeg
Screenshot_20181002-082142.jpeg
Screenshot_20181002-082157.jpeg
Screenshot_20181002-082210.jpeg
Screenshot_20181002-082227.jpeg
 
Wakuu nanyinyi kabisa mnaamini Pogba ndo chanzo cha kufungwa na kuwa na hali mbaya hahahahhaha ngoja twende tutajua tu time will tell
 
Huyu bwana pogba kwa kweli yeye ndiyo chanzo, maana anawafanya hata wachezaji wengine wakose molari na pia hata kufanya wamchukie mourinho
Pogba ni kiongozi tu mkuu ila wengi wao wanamanung'uniko ya ndani kwandani,

ni kama hapa tuchukulie pogba ni Mange alf mtukufu ni Mourinho.....nadhani umeona Mange ni kiongozi wa watu waoga wasiojitokeza hadharani
 
Pogba ni kiongozi tu mkuu ila wengi wao wanamanung'uniko ya ndani kwandani,

ni kama hapa tuchukulie pogba ni Mange alf mtukufu ni Mourinho.....nadhani umeona Mange ni kiongozi wa watu waoga wasiojitokeza hadharani
Mkuu najua umeangalia gemu za man u nyingi alzocheza pogba na u hezaji wake umeuona kijana hachezi jihad ana ubishoo mwingi utoto mwingi yuko slow kwa hili tusikatae tuukubali ukweli
 
*English Premier League officials have drafted some rules to protect Manchester united to survive the relegation*
.
1) Mourinho.. will be allowed to field 15 players at once and 6 substitutes.

2) Man United will be awarded a free penalty at every match.

3)The super sport technicians are cautioned to avoid highlighting any man united goal as this will be regarded as scores.

4) Man united will be awarded 1 point for a lose, 3points for a draw and 6 points for win.

5) Any attempt to tackle lukaku,rashford and pogba will result to a straight red card +penalty regardless of the place the tackle took place.

6) Teams like Chelsea, Tottenham, Man City, arsenal, Liverpool will be only allowed to field 8 players with no substitutes when playing against man u

7) Hazard, ozil, Sallah, aguero, kane Kante, firmino,Mane morata,aubameyang, jesus, willian, Zaha are banned to play against man united until further notice.

*Source #skysportsnews*
 
  1. sitomlaumu jose mourinho kwa sababu ya kuwa na mbinu mbovu na za kizamani za ufundishaji ila nitamlaumu jose mourinho kwa matokeo mabovu anayoyapata uwanjani msimu huu, mourinho si muumini wa mpira wenye kuvutia na hatokuwa muumini wa mpira wenye kuvutia mpaka kufa kwake kisoka.
  2. wakati huyu jamaa anapewa mkataba wa kuifundisha manchester united tunapaswa tujiulize ina maana bodi walikuwa hawafahamu ya kwamba mourinho hafundishi na hatofundisha mpira wa kuvutia akiwa kwenye majukumu yake?
  3. muheshimiwa paul pogba a.k.a mzee wa attack attack style wakati anatia saini manchester united kwa dau lililovunja rekodi miaka mitatu iliopita kutoka juventus alikuwa hafahamu ya kwamba anakwenda kufanya kazi na jose mourinho asiyeamini soka la kuvutia?
  4. sakata la paul pogba halina tofauti na sakata la wayne rooney mnamo mwaka 2010, rooney alidai ya kwamba manchester united imepoteza nguvu na ushawishi kwenye soko la usajili na pia ina wachezaji wa kawaida hivyo basi anataka kuondoka, bado naikumbuka sura yenye hasira ya sir alex ferguson kwenye mahojiano akizungumzia ishu ya rooney. kumbe kelele zote za rooney ishu kubwa alitaka aongezewe mshahara ili awe mchezaji anayelipwa zaidi nchini uingereza. Tukirudi kwa pogba na yeye naamini kelele zote hizi zinachangiwa na ishu ya maslahi yake binafsi na si maslahi ya klabu kama anavyotudanganya
  5. kitendo cha mtumshi hewa anayeitwa alex sanchez kulipwa mshahara mkubwa ndani ya klabu na uingereza kwa ujumla ndicho kinachomuumiza paul pogba na wakala wake mino raiola, ubovu wa sanchez uwanjani ndio mdomo wa paul pogba nje ya uwanja, vijembe vya pogba vinamuhusu mourinho na alex sanchez.pogba alivutiwa zaidi na maslahi aliyoahidiwa na mancheter united kupitia account yake ya benki kuliko maslahi aliyoahidiwa kupitia ndani ya uwanja, inasemekana dili la pogba muheshimiwa mino raiola alivuna wastani wa paundi millioni 15 kama wakala, kama pogba alitaka mpira wa kuvutia na mafanikio kwa nini alikataa ofa ya real madrid?
  6. kwa hali iliofikia siamini ya kwamba jose mourinho atarudisha heshima ya manchester united kwa sababu na yeye pia amehusika kwenye upoteaji wa heshima ya klabu,inasikitisha sana kuona jamaa unapofika msimu wake wa tatu anafukuzwa kwa sababu kubwa mbili zisizobadilika nazo ni matokeo mabovu na kushindwa kuwa na mahusiano mazuri na wachezaji.Hata kama itatokezea upepo ukabadilika na kupata matokeo mazuri basi ningependa mwisho wa msimu mourinho aondolewe kwenye klabu.
  7. bodi ya manchester united wasipokuwa makini watajikuta wanarithi nafasi ya liverpool kwa kusifia historia ya mafanikio yao,miezi hii iliobakia wanapaswa wafanye tathmini ya kutosha kwa ajili ya kutafuta mrithi wa jose mourinho anayeendana na utamaduni wa klabu na mwenye fikra pana kuhusiana na soka la sasa, kinyume chake wataishia kubadili makocha kila msimu kama mzinifu anavyobadili paketi za kondomu kila mechi.
  8. kwa mpira wa sasa ulivyo na ushindani mkubwa sana tunahitaji mwalimu mwenye uwezo wa kutupa mafanikio ndani ya msimu mmoja, tusidanganyane jamani kwa hadhi yetu manchester united hakuna mshabiki, mpenzi na mpiga kelele anayeweza kuvumilia ujengwaji wa timu kwa miaka 3 kipindi hiki, na kwa ushahidi wa hilo klabu ilimfukuza van gaal baada ya kufanya vibaya licha ya kucheza soka la kuvutia.Hivyo basi kitakachomuondoa mourinho ni kufanya kwake vibaya na si kutokucheza soka la kuvutia.
Manchester United news: Paul Pogba admits to Real Madrid snub ahead of £89m return to Old Trafford | Goal.com
 
1/ Sema morinho anagombana na wachezaji sana sio pogba tu angalia Bailly,shaw,Sanchez, na Leo nimesoma sehemu kashagombana na valencia na teammates wamechukia sasa unaweza kuta ata mchezaji anacheza kwa kinyongo sasa atachezaje vizuri

2/ Mchezaji akikosea basi media zote zitajua ataongea kwa kumponda kwenye media hyo haitakiw mwite mtu mwambie sasa hata ungekuwa ww upondewe mbele ya watu cdhani kama utafrahi

3/ mou ana mbinu mbovu sana za mpira we angalia mechi ya westham kama sikosei mc tominey kacheza no 2 wakati ni kiungo nzuri tu.

4/ Yani cha kufanya mou aondoke tu mana sa iv ana ugomvi na wachezaji karibu 7 au 9 je akipewa pesa ndo anunue wote hapo jibu ni hapana anatakiwa atafute wa kuongezea kikosi na sio kununua timu nzima
 
Back
Top Bottom