Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu unajua maana ya full backs? Nitajie full backs wawili wa manchester united. Tuanzie hapo kwanza
 
Ndugu tatizo la MU ni la zamani tangu atoke Ferguson, Moyes, Van Gal na sasa Mo hawapewi wanachokitaka kama makocha, Just fukuza, lakini msipowasikiliza makocha you are and you will be the next Arsenal
Kwa Moyes ni kweli uongozi uliingia chaka kwa kumpa mkataba mrefu wa miaka 6 bila kumpima kwa mkataba wa muda mfupi. Matokeo yakawa mabaya sana na akafukuzwa kabla hata ya kumaliza mwaka.

Management ikajifunza kwamba kocha sahihi anaehitajika ni yule ambae anataka makombe "now" na siyo "in the future".

Akaja LVG na yeye akasajili wachezaji wake kama Di Maria, Blind, Rojo, Memphis, na Martial. Kidogo kulikuwa na improvement kulinganisha na Moyes, lakini at the end hakufanikiwa kufikia malengo.

Akaja Mourinho ambae inajulikana wazi ni aina ya makocha ambao hawana muda wa kujenga kikosi kwa ajili ya future, yeye anachotaka ni ubingwa fasta fasta. Na kweli timu inahitaji kombe angalau la premier league.

Msimu wa kwanza, pili, sasa wa tatu yeye anasajili tu. Mnapata wapi nguvu ya kusema hapewi anachotaka?

Kuna scenarios nyingi katika usajili, kuna mchezaji kukataa ofa, kuna timu kukataa ofa, na kuna mchezaji kuwekewa bei kubwa sana kiasi kwamba timu inayotaka kumsajili inapotezea hata kama anahitajika na kocha.

Haimaamishi kwamba mahitaji yote ya kocha yatakua satisfied 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakini ndio kocha wa klabu yako mpka sasa na hakuna dalili zozote zile na kuondoka kwake.

Hivyo wewe endelea kuumia tu
.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mourinho bado yupo yupo..

Kocha Jose Mourinho bado anaungwa mkono ndani ya Manchester United licha ya kichapo cha 3-2 dhidi ya Brighton.

Matokeo na kiwango cha timu kimeibua maneno mengi dhidi ya kocha huyo wa Kireno.

Mourinho anapewa nafasi kubwa ya kuwa kocha wa kwanza kufukuzwa msimu huu ndani ya EPL , ambapo kocha wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane anapewa nafasi ya kuchukua mikoba yake.

Chanzo kutoka United kimesema," Kwanini tumzungumzie Zidane huku hakuna kazi ya kumpa ? "

Huku Ed Woodward bado anaamini Mourinho ana uwezo na uzoefu wa kuweza kubadilisha matokeo ya Man United kuwa chanya.
 
Mtalaamu wa biashara anataka hadi vya uwanjani
 
Not big deal mkuu, nimechanganya na center back (beki wa kati). Ndo ilikua maana yangu na ahsante kwa kunishtua.

Baada ya hapo unasemaje maoni yako?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sioni kama center back ina tatizo sana kuliko full back. Mechi ya brighton kulikuwa na gape kubwa upande wa kulia kwa young (right back) na hicho ndicho kilisababisha kuonekana bailly kavuruga maana jamaa alikuwa anacover mpaka upande wa kulia anaacha gape katikati. Ukiangalia chanzo cha magoli yote matatu ni makosa yaliyofanyika upande wa kulia kwa young.
 
Kabisa mkuu kumbe tupo sahihi upande wa young ulikuwa na tatizo kubwa sana lakin bado bailly na lindelof walichanganyana sana hapakuonekana nani ana maliza 5
 
Na ukiangalia kwa makini, midfield na attacking ndo zina tatizo zaidi kuliko defence. Viungo wetu wazito hawapeleki mipira mbele kwa wakati, kule mbele ndo tatizo kabisa wamejaa kobe hawana plan, pasi wanapiga hovyo hovyo wanarudisha mipira nyuma hakuna pressing yoyote.
 
Tatizo la Man utd ni... Young,Smalling,Mata,Jones,Valencia,Sanchez,Fellain bila kumsahau Herrera.

Hao wote wakiumia msimu mzima,ndio kidogo tutacheza kama Man u ya Ferguson
GGMU


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi mpaka leo ukiniuliza tatizo kwa timu yetu lipo wapi ntakwambia midfield hasa pogba ni shida hawapeleki mipira mbele kwa wakati hawana speed hawako sharp, right wing nayo ni tatizo hakuna mtu kule huwezi kumtegemea mata/lingard. Lingard anacheza vizuri kama forward namba 10 na siyo winga wa kulia. Midfield hawapo sharp na winga wa kulia hatuna.
 
Sawa mkuu, sasa hizo beki za pembeni kuna beki yeyote ambae kocha alikua na plan za kumsajili? Maana kulia kuna Valencia ambae kocha anapenda sana kumtumia, na ndo captain. Addition aliyofanya kocha ni kumsajili Dallot (19 yrs). Imetokea wote hawapo ikabidi acheze Young ambaye mara zote kocha anamchezesha kushoto.

Na watu wengi wanalaumu kwa nini Mourinho hakupewa Toby Alderweireld na Harry Maguire ambao ni mabeki wa kati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah kiukweli Pogba nae ni tatizo.. He's overrated. Ukiangalia kwenye world cup alikua hafanyi dribbling hovyo hovyo, ila akiwa klabuni analazimisha mbwembwe nyingi halafu ananyang'anywa mpira au anatoa pasi haifiki kwa target.

Halafu baada ya ile mechi ya juzi anaanza ooh attitude this attitude that, kama vipi wamwache asepe kama kweli anataka kusepa, considering upupu ambao agent wake kaongea leo inawezekana lao moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi bado tupo,tutamwona huyo Mourinho wako..tuombe tu uhai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi bado tupo,tutamwona huyo Mourinho wako..tuombe tu uhai

Sent using Jamii Forums mobile app
Kujenga timu sio jambo dogo na si kwamba mourinho ni kocha mzuri hapana safari ni ndefu hata aje nani kuna ku RISE AND FALL cha msingi uvumilivu bodi kuvutana na kocha jambo baya sana hata kama alipoint wachezaj above 29 nani kaumia mashabik,bodi au kocha?

Pia kocha yoyote atakateuliwa na timu nitamsapot no matter what
 
Kukosa fullback ndio kunasababisha hadi dk ya 70 dhidi ya BHA tuwe na shot 'moja' on target??

Sababu hiyo hiyo ndio inafanya kila mtu acheze anavyojua yeye? Hivi mnaangalia mechi zipi za Utd??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pumba Tupu,


Samahani kwa kusema hilo, ila pumba zako hata Kuku hawali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…