Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wale waliompitishia David Moyes ndege na Banner ya Moyes Out walikuwa ni mashabiki Wa simba au???



Hivi nyie mbona mnalazimisha vitu vilivyo hadharani au mnadhani sisi ni vichaa. Mpira ni tukio la hadharani. Jana Vs Bayern Team haijapiga shout hata moja langoni unakuja na porojo zako za Plastic fan.



Hivi wewe mtanzania ukute hata membership card ya team huna unakuwa na Guts za kumuita English Fan kindakindaki Wa united kuwa sio real fan.


Yani wewe mlugulu uiepende Manchester saaaaaaana kuliko Mtoto Wa kiingereza kama Gary Neville au Gigs eti unashupaza domo kuwa hao ni wachumia tumbo.






Kingine mbona mnatumia nguvu kubwa kumtafutia mou ushawishi??? Acheni matokeo yatulize ghasia za mashabiki na sio kuita watu majina ya kipuuzi.


Hakuna shabiki anaependa team ya hovyo ,hakuna. Huyo furguson Mwenye almanusura atimuliwe kabla ya kuuwasha moto kuanzia miaka ya 90, Kinyume na hapo alikuwa anaenda na maji.
 
Ed woordward asimpe tena hela huyu mhuni ya kireno ya kusajili wazee wake pale OT ambao hawatatusaidia kitu..sack him at the end of this upcoming season,then leta kocha atakayefundisha mpira wa kisasa na kutengeneza hamasa ndani na nje ya uwanja,,sio huyu bwatukaji wa kireno
 
1. Kipindi cha moyes tayari ED ameshakuja
2. Kipindi cha moyes kinahesabika kama miaka ya karibuni kama nilivyosema.
Hoja yako sijaielewa hapo.

Si kweli mshabiki wa ukweli anaipenda for better and for worse team yake, timu ikifanya vibaya sio yako na timu ikifanya vizuri ni yako huo sio ushabiki bali una jina maarufu kama Glory Hunter.

Fergie alipewa muda wa kutimuliwa mwaka wa 4 na sio alipokuja tu akawa anazomewa na kutolewa maneno machafu. Na matokeo ya mou Ndani ya miaka 2 ni mazuri kushinda ya fergie ndani ya miaka 4 ambayo alichukua FA tu.

LvG alipewa Task timu iende UEFA akafeli msimu wa pili. Same kwa moyes.

MOU nae amepewa same task msimu kwa kwanza timu iende UEFa na Pia tu compete league, Yote ameyakamilisha Timu ipo Uefa na tumepata point 81 ambazo tungekuwa msimu Leicester anachukua Ubingwa sasa hivi tungekuwa mabingwa watetezi. Hivyo ni kocha aliefanikiwa, ndio maana yupo pale, atafukuzwa asipoleta matokeo, ila kwa sasa ni kocha wetu na ana deliver ni jukumu letu kama mashabiki kuwa nyuma ya kocha wetu.

Pia usijidanganye Man u sio kama Simba na Yanga na kadi za Uananchama ile ni kampuni ina wamiliki na Hisa.
 
Mino Raiola is in England to attempt to force negotiations for the departure of Manchester United midfielder Paul Pogba, according to Mundo Deportivo.
 
Upo sahihi kabisa wakati nyie mnapambana na kocha ambae anawachezaji wa kawaida ambao mnawakuza kama top player vi timu vidogo vinaboresha timu zao subir wapambane na wakina darmian mle mkono.
 
Mino Raiola is in England to attempt to force negotiations for the departure of Manchester United midfielder Paul Pogba, according to Mundo Deportivo.
Huyo agent alimmsumbua sana hata sir alex si mtu mzur mtu na hilo atakwambia ni kocha.
 
Pep anataka kiungo mwingine wakat ceo wa united anaamini wakina lingard ni sawa na silva.
 
Pep anataka kiungo mwingine wakat ceo wa united anaamini wakina lingard ni sawa na silva.
Nilichokiona huyu mreno msimu ujao hatakuwepo na ed hataki kumpa pesa za ovyo ovyo tu,,atumie kikosi hiki kutubakiza top 4,,akishindwa sawa tu..ila msimu huu ni wa mwisho lazima atumuliwe..
 
Kuanza upya si ujinga,ila anahitajika kocha anayekuja kutengeneza timu walau ndani ya miaka 2 uelekeo uanze kuonekana. Usajili wa JM hautoi taswira rahisi kutafsirika. Tunaaminishwa timu inapaki bus lakini makombe tubebe ila sidhani kama itatokea hivi karibuni,europa na qarabao ile ndio mwisho wetu chini ya huyu mhuni wa kireno.
 
Tetesi

Martial njian kwenda Chelsea kwa kubadilishana na willian

Pogba njian kwenda Barcelona
 
nimeiangalia iyo video aiseeee yani humu kuna mashoga walipaswa kuwepo kuleeeee kwenye bango la manchester is my heaven halafu wachache wabaki hapa mwanzo kwa wahuni mwanzo mwisho wao kushangilia
 


Eti Mlugulu 😀😀😀
 
Ndo nilichokisema mkuu,kwamba mourinho anaonekana dhahiri anataka kupata kombe bila ya kutengeneza timu itakayokuwa na ubora kwa miaka miwili au mitatu mbeleni..Ndo maana nasema asipewe pesa tena,,bajeti aje apewe kocha atakayeijenga united mpya
 
Tetesi

Martial njian kwenda Chelsea kwa kubadilishana na willian

Pogba njian kwenda Barcelona
Kuna muda iwe hivyo rooney alilazimishwa kucheza kila namba kwa mapenz ya timu na kukubali majukumu mapya martial kaomba kusepa kwa nini akataliwe hapa ndo linapokija suala la kutengeneza wachezaj wa academy ni nadra kusikia wana ka mgomo au kaomba kusepa watapambana kwa ajili ya timu haijalishi yupo ktk mazingira yapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…