Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Unajua tunacho tofautiana ni kitu kimoja. Mourinho ni binadamu na ana mapungufu kama walivyo binadamu wengine. Ila unacho sahau ni kwamba kila kocha ana hitaji watu wa aina Fulani ili kuweza kufiti kwenye mfumo wake. Usipo mpa watu wanao fiti kwenye huo mfumo basi usitegemee kupata Matokeo mazuri.Kama bodi ya utd ingekuwa inaangalia mpira wa Pasi nyingi (mpira mnao ita ni wa kisasa) LVG asinge fukuzwa. Shida ya Manchester haikuwa kucheza mpira mzuri shida KUBWA ni makombe. Na hii task aliyeonekana(binafsi naamnini anayeweza kufanya mpaka saiz) ni Mourinho.

Kwa mtazamo wangu ukiniuliza kuhusu Rojo kutaka kuuzwa naona wameangalia udhaifu wa Rojo. Rojo ni beki mzuri na anatufaa kabisaa ila shida ni MTU ambaye huna uhakika wa yeye kucheza mechi tano mfululizo(injuries). Na ukimuweka sokoni anauzika Kwa bei mzuri, sasa kwanini usichukue hela hiyo halafu ukatafuta beki ambaye sio injury prone??

Tangu Fergie ameondoka basi msimu uliopita ndio msimu bora kwa Man utd kwenye ligi ila kilicho tuangusha ni kwamba Man City alikuwa bora zaidi yetu.
BODI IMPE MOU WANAJESHI ANAO WATAKA, BAADA YA HAPO NDIO TUTOE HUKUMU.
 
Mkuu top players wa aina gani Man United inayowakosa?

Wakina Sanchez,Pogba,Matic,Herrera,Lukaku,Bailly,Martial,De Gea sio top players?
Hawa wote wana uwezo wa kuchezea Madrid vizuri tu.
Timu nzima haiwezi Kuwa na top players namba zote.

Je Liverpool ina top players gani? Mbona ilifika fainali UEFA?
 
Ukiangalia chanzo cha hiyo post uliyo quote utagundua aliye mention majina ni tofauti na aliye sema kuwa Man utd ina wachezaji wabovu.
Mkuu ni kweli Man utd ina baadhi ya wachezaji wazuri ila tatizo pia ina wachezaji wengi zaidi ambao sio wazuri(kwa mtazamo wangu). Ili kujipima kama una timu nzuri au mbovu inabidi pia uangalie na wapinzani wako wapo vipi?
Kwa upande wangu wachezaji wa kikosi cha kwanza waliokuwepo msimu uliopita wenye hadhi ya kuchezea man utd ni Degea,Matic,Herrera,Pogba,Sanchez(kaja January nadhani msimu huu ata improve),Mata na Lukaku.
Rojo&Baily msimu uliopita karibu wote wameumalizia benchi.
Valencia &Young wanajituma kweli lakini kwa age yao walitakiwa wawe backup players.
Martial na Rashford walikosa consistency.
(najua watu watasema wali badilishwa badilishwa namba lakini nacho jua mchezaji mzuri anajithidi kutumia vizuri kila dk anayo pewa ili aweze Ku prove kuwa yeye ni mchezaji mzuri)
Linderlof bado hakuwa amezoea na alipo pewa nafasi wote tuliona makosa aliyo kuwa ana yafanya.

Na tatizo linaloonekana wazi kwenye timu ya Manchester ni udhaifu wa upande wa kulia pamoja na back line(japo hili lilifichwa na Degea). Naamini yakifanyiwa kazi hayo hapo tutakuwa kwenye position nzuri kuanza kumjudge kocha.

Kwa Pogba hata mashabiki wa man utd na malegend wengi wamekuwa wanamsema kuhusu attitude yake. Na mou alilizungumzia hilo ila sikumbuki kama amewahi kusema Pogba ni mbovu au hana kiwango.
 
Huyo Jamaa ni mbishi sijapata ona

Mbona Ni Mambo Ya Kawaida Kwenye Majukwaa Kama Haya Kutofautiana Mitazamo.

Hata Jukwaa letu sometimes unaweza Kutukutia Kama Bunge la Ukraine ambalo Nusu ya Wabunge wake ni Maboxer Muda wowote Hutupiana Makonde.

Haiwezekani Washabiki Wote Wawe na Mtazamo mmoja.
 
Mkuu unataka kulinganisha wachezaji waliokuwepo Man utd na Real Madrid? Huo mzani hauja balance.
Hao liver walivyo fika fainali walifanyajee?

Na ukitaka uone faida ya kuwa na top players wengi refer hiyo hiyo hiyo mechi ya Madrid vs liver. Wakati kina cr7 wamebanwa anakuja bale from benchi na anakiwasha. Liver alipo toka Salah akaingia Lalana
 
Last edited:
Mkuu umewahi kujiuliza kwa nini kipa anakuwa mchezaji bora wa timu misimu labda minne mfululizo hao hawakuwepo?wapiga kura wanakuwa na uoendeleo au?
 
Mkuu unataka kulinganisha wachezaji waliokuwepo Man utd na Real Madrid? Huo mzani hauja balance.
Hao liver walivyo fika fainali walifanyajee?
Mkuu labda muulize Aliumia salah ambae ana mchango mkubwa ndani ya liverpool bench alikuwa nani mbadala?

Liverpool wangekuwa na kikosi kipana na top players walah wangefanya jambo alibaki mane bado walikuwa mwiba madrid walishinda game kwa kuwa na wachezaj wengi wazuri na ukibwa wa kikosi chao leo sisi akiumia valencia sub ni darmian huu is utani
 
Fact.
 
Nimesha edit post tayri Mkuu.
Na hii ndio point ya msingi.
Wanasahau alipo umia Salah akaingia Lalana tofauti ya viwango vyao ni mbingu na ardhi.

Madrid walikuwa wanaweza kucheza mechi NNE kwa formations tofauti na zisijirudie kutokana na mahitaji ya mechi. Mchezaji A asipo perform anaingia Mchezaji B na unaona tofauti.
 
Tukiwa tunawaambia huyu kocha ni mbabaishaji muwe mnatuelewa wandugu.



Leo anasema sanchez ni poor hahaha h a .... Halafu anakuja mtu anasema apewe hela ya kusajili.
 
Wanashindwa kuona hata zile mechi tulizoshinda msimu uliopita zingeongezwa dakika tano katika hizo mechi tungeweza kutoka sare au kufungwa kabisa.

Timu inacheza hovyo sana.
Kuna muda najiuliza hivi zile mechi za Manchester huwa na hawa mashabiki wanaomtetea mou huwa wanaziangalia kweli??


Maana kama kweli last season mtu ulishuhudia game za United huwezi kumtetea Mou hata robo. Mpira hooooovyo
 
Tukiwa tunawaambia huyu kocha ni mbabaishaji muwe mnatuelewa wandugu.



Leo anasema sanchez ni poor hahaha h a .... Halafu anakuja mtu anasema apewe hela ya kusajili.View attachment 823464
Kwa nilivyo ielewa hiyo kauli ni kwamba alikuwa ana sikitika kuwa mpaka saiz mchezaji pekee wa kikosi cha kwanza kwenye nafasi ya ushambuliaji aliyerudi ni Alexis Sanchez.
Sijui wewe umetoka na tafsiri gani hapo.
 
Wewe utakuwa sio mzima , kwanza nimekusoma una udhaifu wa kusahau. Leo umesahau mambo mazito aliyofanya Rashford katika umri wake mdogo. Umesahau Van Gal alivyomuamini vs Arsenal Akawapiga 2 peke yake. Umesahau debut yake ya europa?? Umesahau leo hii???


Kwa hyo kipindi hicho rashford hakuwa mdogo??? Mbinu za mou ndio zimewaruin martial na Rashford.

Rashford huyu huyu ndio mlikuwa mnasema ni new mega player chini ya Van Gal. Martial kipindi cha Van Gal anatupia golini kama kichaa watu walisema ni new Dwight York. Baada ya kuja Mou mnakuja kusema ni weak players????



Jitafakarini
 
Kwa nilivyo ielewa hiyo kauli ni kwamba alikuwa ana sikitika kuwa mpaka saiz mchezaji pekee wa kikosi cha kwanza kwenye nafasi ya ushambuliaji aliyerudi ni Alexis Sanchez.
Sijui wewe umetoka na tafsiri gani hapo.
Mkuu kwahyo wewe ulivyolewa hayo maneno ni kuwa " Mchezaji wa kikosi cha kwanza alierudi ni sanchezi tu"



Hahahahahaha Elimu yetu inahitaji mapinduzi mazito ya Kiufundi.


Kwahiyo hujaona neno "poor sanchez".... Hebu Tafuta English dictionary ya Cambridge uangalie maana ya neno Poor halafu uje hapa Kutoa comment yako tena.



 
Yaani hata sentensi yangu inaonekana hujaisoma yote. Na usitake kuniambia amemaanisha poor ya masikini (fukara) maana utakuwa unachekesha. Au kwa kuondoa mzozo toa tafsiri yako kwa sentensi hiyo.
Hasira zisikutie upofu.
 
Last edited:
Marekebisho kidogo Toure ashatemwa pale city
 
Maneno aliyo yaongea kwa ujumla wa hiyo sentensi ni haya. Sio unakuta ka line kamoja na wewe unachukua neno moja. Eti poor Sanchez ndio una kasimamia hako hako. Hasira zako kwa Mou zisikutie upofu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…