Man City na Mpira Pesa.
Manchester City ndio kikosi kilichotengenezwa kwa kiasi kikubwa cha fedha katika Historia ya soka baada ya kutumia kiasi cha Euro Milioni 878 katika soko la usajili, kwa mujibu wa taarifa mpya za matumizi ya fedha.
Orodha iliyochapishwa na CIES Football Observatory inaonyesha kikosi cha Pep Guardiola ambao ni vinara wa Ligi kuu ya Soka ya Uingereza, wametumia kiasi kikubwa cha fedha zaidi ya klabu yoyote ile katika ligi kuu tano bora barani Ulaya, baada ya usajili wa mwezi huu Januari wa Pauni Milioni 57 wa beki Aymeric Laporte.
Uwekezaji wa City , umeupiku ule wa Paris Saint-Germain ambao umegharimu kiasi cha Euro Milioni 805, zaidi ya robo ya matumizi hayo yametumika kumsajili Neymar kwa rekodi ya usajili ya Euro Milioni 222 kutoka Barcelona.
Manchester United wanashika nafasi ya tatu katika orodha hiyo wakiwa wametumia kiasi cha Euro Milioni 747, juu ya Barcelona ambao wametumia Euro Milioni 725, Chelsea Euro Milioni 592 na Real Madrid ni Euro Milioni 497.
Kuna vilabu sita kutoka ligi kuu ya soka ya Uingereza katika orodha ya 20 bora vikiwemo vilabu vya , :
( Liverpool (€461m), Arsenal (€403m), Everton (€365m), Tottenham (€358m), Southampton (€229m) and Crystal Palace (€225m). )
Na wastani wa matumizi wa ligi kuu ya soka ya Uingereza upo kwenye thamani ya Euro Milioni 291, mbele ya Hispania , Euro Milioni 131, Serie A Euro milioni 124, Bundesliga Euro Milioni 113 na Ligi ya Ufaransa Euro Milioni 91.
View attachment 694553