Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tetesi
MAN UTD WANAMTAKA KINDA WA WHITECAPS


Manchester United wamemwalika kinda wa Vancouver Whitecaps Alphonso Davies kufanya majaribio Januari kwa mujibu wa CTV Edmonton .
Kinda huyo wa miaka 17 ambaye amekuwa mchezaji mdogo zaidi kuichezea timu ya taifa ya Canada majira ya joto, anasubiri kupata kibali kutoka kwenye klabu yake kutua United.
 
Tetesi
ROMERO ANAFIKIRIA KUONDOKA MAN UTD


Sergio Romero anafikiria kuondoka Manchester United dirisha la uhamisho wa Januari kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia majira ya joto, kwa mujibu wa Daily Mail .
Romero ameendelea kuwa mlinda mlango chaguo la kwanza kwa Argentina, licha ya kucheza kama kipa nambari mbili United nyuma ya David de Gea.
 
Tetesi
MAN UTD BADO WANAMTAKA PERISIC


Manchester United bado wanaitamani huduma ya Ivan Perisic baada ya kumkosa winga huyo wa Inter uhamisho wa majira ya joto, kwa mujibu wa The Sun .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia alisaini mkataba mpya kubaki Italia, lakini mchakato huo ulifanyika kutunza thamani yake ila anaweza kupatikana Januari kwa dau la £45 milioni.
 
Tetesi
UTD YATENGA £95M KUMPATA NYOTA WA LAZIO


Manchester United wanataka kuvunja rekodi yao ya usajili kwa kuinasa saini ya nyota wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic kwa dau la £95m, kwa mujibu wa The Express .
Kiungo huyo yumo kwenye rada za miamba wa Serie A Juventus, lakini Jose Mourinho amemfanya kuwa shabaha kuu kwa bodi ya Old Trafford.
 
Tetesi
MAN UTD YATENGA DAU KUMSAJILI ASENSIO


Manchester United itafanya mchakato kumsajili kiungo wa Real Madrid Marco Asensio dirisha la uhamisho la Januari baada ya kuachana na mpango wa kumsajili Gareth Bale, kwa mujibu wa Don Balon .
Mashetani Wekundu wanajiamini watafanikiwa kumsajili mchezaji huyo wa miaka 21 kwani ameshindwa kupata nafasi ya kudumu Santiago Bernabeu.
 
Tetesi
MAN UTD KUMUUZA SHAW & DARMIAN


Manchester United wapo tayari kusikiliza ofa kuwauza mabeki wao Luke Shaw na Matteo Darmian, kwa mujibu wa The Daily Record .
Shaw ambaye amesumbuliwa na majeraha amepewa nafasi kujiunga na klabu nyingi za Uingereza wakati Muitaliano Darmian hatakiwi kwenye kikosi cha Jose Mourinho.
United wanataka kutunisha mfuko wao ili kuwasajili beki wa kushoto Alex Sandro na Danny Rose majira ya baridi.
 
Tetesi
MAN UTD WANATAKA KUMSAJILI ALEX SANDRO


Jose Mourinho amemfanya Alex Sandro wa Juventus kuwa shabaha nambari moja kutua Manchester United kucheza nafasi ya beki wa kushoto kwa mujibu wa Daily Record .
 
City ndo bingwa wa epl ilo halipingiki ila tunafurahi kulikua na kauli kua hatujawahi fungwa uwanja wetu mara cc ndo tutamsimamisha huyu mtu mara sisi ndo tunagombea nae ubingwa hahahaaa jana mtt kalale kwa jilani na "fyatu" vyake

Hapo kuna utoafaut wa mashabik wa timu ndogo na kubwa nyie tayar mshasanda sisi hatujazoea kukata tamaa kama nyie mashabik wa vitimu vidigo bingwa hutangazwa may sio december Mpira ni bahat shukran ziende kwa striker wangu lukaku tu ila wale mliokuwa mkiwataja hawakuonekana pale.
 
Mourihno anakosa nn mpaka anakua na approach mbovu hv dhidi ya timu kubwa?
Alikuwa na kikosi finyu jana, Wachezaji wanne muhimu hawakuwa uwanjani, City ni timu nzuri lazima ucheze nayo kwa tahadhari, kufungwa ni matokeo na mpira ni mchezo wa makosa, ukiangalia jana tulicheza vizuri zaidi ila bahati haikuwa yetu.

City hawakucheza mpira wao, uliona dakika 10 za mwisho City ndio walicheza mpira wao.

All in All tunapokutana na timu kubwa kuna aina flan ya Wachezaji tunawakosa kuufanya Mfumo wetu kucheza, Hatuna winger wa uhakika zaidi ya Martial, timu haina mbadala wa Pogba.

Imagine tungekuwa na Perisic yule wa Inter kama namba 7, afu Martial 11 kati kukawa na Lukaku na Rashford.

Ule ndio Mpira wa Man United hata tulipokuwa na Ferguson tatizo tulikosa Wachezaji muhimu.


Sikuumia kwa kuwa tuliitendea haki Match.
 
Unajenga timu mwaka wa ngapi huu?Guardiola kaja lini? Unanunua wachezaji kwa record ya dunia unaishia kupaki basi!!

Pep hakuikuta city mbovu wewe Kdb,silva,aguero,company,fernandinho,sterling hao wanamsaidia sana yeye kanunua bek tu
 

Nimekupata mkuu
 
babu fegi alikua na timu ya kawaida sana ila ilikua inapambana hatari ila kuna baadhi ya mechi tulibebwa na bahati na si soka la uwanjani....hao city rejea mechi zao 2 za nyuma na soton na westham ndio utajua nini nachokiongelea
 
na hawa jamaa kwa bahati tu wamejaliwa kwa kweli
 
hii ngoma mpaka christmas tulikua tunaongoza sie ligi lakini kilichokuja kutokea sasa kwanin usiseme ni bahati ilichangia kwa 100%
 
kwangu ni bora aje dyabala kulko huyo perisic
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…