Manchester United (Red Devils) | Special Thread

faida kubwa ya jamiiforums ni kwamba kila member ana uhuru wa kutoa mawazo yake bila ya kubughudhiwa ila nimesikitishwa na baadhi ya mawazo ya wachangiaji.
Inasikitisha kuona baadhi ya wadau wa manchester united kumdharau mourinho na kufika mtu kusema mourinho ni mwalimu mbovu na hafai kuwepo manchester.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyeileta fc Porto kwenye ramani ya soka la ulaya na aliifunga manchester united kwenye robo final mwaka 2004.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyeipa mafanikio makubwa Chelsea na kuipa utambulisho kwenye soka la ushindani duniani.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyerudisha soka la ushindani nchini italy na kuipa mafanikio Inter Milan iliyoundwa na wachezaji wa kawaida kama cambiasso,lucio,stankovic n.k
Ni mourinho huyu huyu tena ndiye aliyekwenda kuondoa utawala wa wasio shindika wa guardiola isala nchini hispania na haya mafanikio ya ancelloti na zidane ni msingi uliojengwa na mourinho. Kumtukana mourinho kwa sababu anampenda Lingard ni makosa makubwa kwa mtazamo wangu kwa sababu lingard hakupandishwa timu kubwa na mourinho ila yeye alimkuta tu.
Wakati moyes anarithi nafasi ya big boss aliamua kumtoa lingard kwa mkopo na baada ya kufanya vizuri van gaal aliamua kumrudisha kwenye kikosi na nakumbuka mechi ya kwanza ya ligi dhidi ya swansea lingard alianza kikosi cha kwanza(3 -5-2)na bahati mbaya aliumia na akakaa nje kipindi kirefu.
Msimu wa pili wa van gaal aliwauza van persie,dimaria,kagawa,rafael n.k lakini alishindwa kumuuza lingard na aliendelea kumpa nafasi lakini hatukulalamika.
Kwanini awe mourinho wa kulaumiwa?
Siamini kama tumefungwa kwa sababu ya lingard ila naamini tulifungwa kwa sababu tulishindwa kumdhibiti Isco alacron ambaye ndiye mchezaji bora wa real madrid kwa miezi sita amekuwa kwenye ubora.
Kama mourinho aliweza kusikia kilio changu na akafanikiwa kutafuta dawa ya eden hazard basi naamini jose mourinho ataitafuta dawa ya kutibu ugonjwa hatari wa Isco.
Kama mourinho aliweza kutafuta dawa ya kutibu ugonjwa hatari wa xavi na iniesta na mimi naamini jose atafanikiwa kutafuta chanjo ya kutibu ugonjwa hatari wa Isco mwanadamu aliyewafanya juventus kipindi cha pili waonekane kama walikunywa togwa kwenye final ya uefa.
Kwa mpira niliouona jana kipindi cha pili mimi ningependelea kwenye ligi kuu tunapocheza na timu kama west ham tusitumie viungo watatu kwa sababu kasi yetu inakuwa ni ndogo sana na pia huwa hatutengenezi nafasi nyingi.
Kati ya pogba au herrera kwa mtazamo wangu mechi ya ligi kuu mmoja wapo anapaswa akae benchi ili mbele tuweke utatu mtakatifu (mkhitaryan +mata+martial) utakaomuwezesha lukaku kufunga mabao 3 na nitafurahi kama mourinho atakuwa na mawazo kama yangu.
Nitoe shukrani zangu za dhati kwa uongozi mzima wa chelsea kwa kukubali kupokea million 40 kwa ajili ya mauzo ya Matic ila kwenye kipengele cha mauzo walishindwa kuweka kipengele cha kutaka tuwalipe kila mechi atakayocheza matic na hili ni kosa kubwa sana kwa sababu matic ana uwezo wa kucheza hadi miaka 40 bila ya kuchoka.
Pia nimkumbushe muafrika mwenzangu ngolo kante ajiandae kisaikolojia kurudisha ile tunzo ya mchezaji bora wa ligi kuu na wala hapaswi kuipeleka FA ila anatakiwa amkabidhi fundi Mkhitryan kabla ya jumamosi hata kama ligi haijaanza, njia pekee ya kumzuia mkhitaryan asibebe tunzo msimu huu ni kumkata mguu wake.
Mimi naamini kwa timu yetu ilivyo hata kama tutakuwa kundi moja na timu kama real madrid, munich na psg basi sisi tutatokea nafasi ya pili na nafsi ya kwanza watajuwana wenyewe kwa sababu tuna mwalim anayejua kuzitumia mechi mbili za home and away na ndio maana msimu uliopita niliamini timu ilihitaji zaidi kombe la europa kuliko nafasi ya nne japo mashabiki wengi waliamini bado ni mapema.
majirani zetu wenye kelele waanze kujiandaa kisaikolojia kabla ya jumamosi haijafika.
chelsea,arsenal,liverpool hawa wote ni majirani zetu na si wapinzani kama wanavyojidai kwa sababu thamani ya manchester united unaweza kuzinunua timu mbili unazozipenda kati ya chelsea,man city,liverpool na arsenal
 
Umesahau kitu kimoja kuwa hata Neymar angekuwa Liverpool asingefikisha hayo magoli na assist.
 
Umesahau kitu kimoja kuwa hata Neymar angekuwa Liverpool asingefikisha hayo magoli na assist.

Neymar Kaanza Kucheza Na Kufunga Magoli Ya Kutosha Toka Akiwa Ligi Ya Kwao Brazil Na Timu Ya Taifa Achana Na Hiyo Kitu
 
Umeanza vizur ukamalizia na pumba.. matic n kiungo mzito sana.... kama hujui... yupo slow.. na anachoka haraka especially second half... team ikiwa inashambuliwa matic huwa anapotea.. kama ulimfuatilia vizur Chelsea ngolo kante aliteseka sana pind akicheza na matic.. I stand to be corrected...

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Hii Kamba Sasa
 
Matic ni kiungo mzito ??? Sijui kama unamfaham matic vizuri

Sent From My Nokia Ya Tochi
 
Manchester United have started talks over a new deal to bring back striker Zlatan Ibrahimovic, according to Sky in Italy.

The 35-year-old Swede is a free agent following his release from Old Trafford at the end of last season and is battling back to fitness after suffering a cruciate knee ligament injury in April.

His rehabilitation has continued at the club's Carrington training complex, with Jose Mourinho saying in July that he could resume at United despite Romelu Lukaku's arrival. "Why not wait for such a good player that gave us so much?" he said.
 
Matic ni kiungo mzito ??? Sijui kama unamfaham matic vizuri

Sent From My Nokia Ya Tochi

Matic ni kiungo kizuri, lakini unatakiwa wachezaji wa midfield kama Pogba, Mkhitaryan, Lingard, Herrera, Mata, Fellaini na Carrick wawe wanaweza kufunga magoli mengi kila mwaka kama Paul scholes, David Beckham, Ryan Giggs au Roy keane. Wote walikuwa wanafunga kama zaidi ya 10 goals kila mwaka. Lakini hawa wa sasa hivi hawawezi kufanya hivyo. Hili ni tatizo Kubwa.
 
Hayo ni masihara zaidi. Hivi mbona Mourinho anabadili utamaduni wa Man U wa 'hakuna mchezaji Mkubwa kuliko klabu'? Zlatan alikuwa hivyo kule PSG, sasa naona hilo linataka kuja kwetu. Klabu ishatangaza kumuacha lakini inampa option ya kusaini tena au kuondoka manake nini, kwa kipi alichonacho yule mzee? Kiukweli naamini Ibra wa Jana c Ibra wa Leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakin mbna Antonio contee
Anasema kwamba kauzwa matic bila ridhaa yake ? Anadai kwamba hata kumleta bakayo haikuwa na lengo matic aondoke bali ilikua kuongeza nguvu tu...ww unamdiss ...frsh lakin n mtazamo wako
 
Sidhani kama umewahi kumuona Matic akicheza.Ulimuona jana alivyocheza against Casemiro,Kroos & Mondric ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…