Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hii khofu sijui inatoka wapi! pana shabiki mmoja kanasibisha hili la lukaku na moyes kuwa bwana David aliitengeneza vizuri toffes kwa wachezaji wa pesa kidogo tukaona akiwa na fungu zuri atafanya makubwa matokeo tuliyaona. Lukaku wapishi walikuwa sio mahiri kama ambao anakutana nao OT sasa hapo tena ni kupasia nyavu tu ndio lililobaki jamaa hana anachokijua zaidi ya kufunga na ndio tulipungukiwa hicho.
 
Huyu kijana huwa nakosa la kusema tambo analo zuri tu sasa sijui hata nisemaje !
 
Kwakweli nimekuwa na wikiendi ya kushangaa watu ambao wanakuwa na wasiwasi kwa lukaku ambaye aliweza kutupia vyuma akiwa kama kuku wa kienyeji (anajitafutia chakula chake mwenyewe) sasa yupo na walishaji mahiri kabisa na chanjo anapewa kweli atashindwa kufanya bora zaidi?

I BET LUKAKU NDIO TOP GOAL SCORER WA MSIMU WA 2017/2018
Mark my words, kacnia
 
Hilo nalitegemea na tuanze na EPL watu hawajui ndio pana mechi nyingi na nzugwe kubwa nina imani atatupatia mabao mengi akiisha elewana na wapishi pale zile volley za kina Pogba na penetration za mata na herera burdan.
 
Hata mimi nina uhakika na hilo hawezi kuwa na mpinzani
 
Hata mimi nina uhakika na hilo hawezi kuwa na mpinzani
Unajua watu wanashindwa kutofautisha ugumu wa timu zinazosadikika kuwa ndogo epl na zile za la liga! Epl ni ngumu inahitaji mtu mwenye uzoefu na ligi ili kuwa na msimu wa mafanikio zaidi (lukaku) sasa wanaposema eti hawana imani na lukaku ambaye amekuwa na msimu wa mafanikio zaidi akiwa na everton nakuwa napata kigugumizi kuwaelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…