Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ni kweli lkn nyie hampigwi nyie sare ndio zinawaghalimu.

Na ukiingalia Utd jinsi ilivyo kwa sasa baba Mou january anatakiwa aingie sokoni kununua Ata wachezaji watatu hivi ktk nafasi tatu hivi. Back line, middle na ushambuliaji.
Ntunzu hali ya timu inayotafuta matokeo inaonekana mapema game ya kwanza liver alitupiga 4 lakini game iliisha 4-3 man walituongoza 1 but dakika ya 89 ilikua 1-1

Nikizungumzia liver hawako nyuma toka kwa viongozi man city pia

Chelsea waliongozwa goli na man city ila uliisha 3-1

Kuna hali ya kutaka matokeo ambayo sijaona hiyo kitu kwa mourinho yeye poa tu yote sawa

Sasa kwa hli hiyo ni sawa we unafikiri nani atakubali kwenda man u kuarbu cV?
 
Hapo ndio tunapo pishana na wewe, kila kinacho endelea now, kocha lazima aingie kwenye lawama, anaweza asiwe kocha pekee
Ila namba 1, ni yeye.

Mnamkubali wap, mmefukuza mara 2 , mbona hamkukaa naye mwaka jana!!. Au mnamkubali kwa anacho fanya now
Hebu nikuombe unitajie ni kwa namna gani kocha anaingia ktk lawama? Hebu nitajie sbbu kadhaa Wa kadhaa.

Kufukuzwa Chelsea kuna sbbu nyingi sn lkn si kwamba alifukuzwa kwamba hawezi Bali alitolewa angalau kuinusuru timu ktk hali zote maana ilikua wazi tatizo la Chelsea kuharibu ni ule uwepo wake na si kwamba alikua kocha mbovu. Sijui unanielewa?

Karibu Iceman 3D
 
According to statistics tatizo kubwa la United msimu huu ni kushindwa kufunga magoli compared na nafasi wanazotengeneza but kwenye maeneo mengine timu imeimprove ukilinganisha enzi za Moyes na LVG
Belo timu yenu iko vzr na kocha mnae sahihi dirisha dogo najua ataingia sokoni kutafuta wachezaji anaowahitaji kwa kz maalumu ambao kwa sasa hana. Kwa mfano ktk sehemu inayomsumbua sn Mou nu Ma DM hapo kwa Utd ukimtoa Carrick na uzee wake wengine bado hawajafika ktk kiwango akitakacho Mou. Hilo ndio tatizo LA Utd. Alafu unakuja huko kwenye kutupia ndio kuko poor.
 

1.Sasa mkuu data za hao si u google tuu, hata wikipedia utaziona mi nimesema walifanya vyema kama hawakufanya vema wewe ndio kazi yako kuleta data ili uni prove wrong.
2. Tuchel aliikuta timu kwejye hali mbaya kuliko Mou, Zidane alikuta morali iko chini sanaa, ancelotti pia alikuta kuna hali mbaya ki morali. hilo tusiende mbali LVG ali ikuta timu ina hali mbayaaaa, ila alijitutumua.
Hivi mourinho amekuta timu ina hali mbaya kias gani mpaka ana ishusha kutoka alipo ikuta!?

3. Kumbuka tume mpokea Mou aliye acha timu ina karibia kushuka daraja, my concern is that, ubingwa alio chukua sina shida nao kabisa na nakubali kuwa alibeba. Ila namna aliyo ishia chelsea ndio namna hiyo hiyo alo anzia utd

Nawish Mou angefanya vzuri, lakini sioni kama ana fanya vizuri, sioni kabisa kama ata fanya vizuri hapo baadaye (japo inawezekana akabadilika).
 
Jamaa unajua kupulizia hahaha
 
Tuchel kapewa timu msimu uliopita, unajua saiz ni wangapi?
Alimaliza wa pili mwaka jana, hata ndio kashuka but hafanyi vibaya kama Mou.
Na ukizingatia ni kocha wa Calibre ya kawaida kabisa, he is good.
 
Sio sahihi mkuu. Utd inapambana sn... Tena Mourinho na wachezaji wake hawataki kabisa kupoteza au kupata matokeo mabaya. Unaweza kuzisoma Ata nyuso zao. Sometimes jaribuni kua Ata wataalam Wa body examine.... All Utd team and technical bench they are not happy with the results which they have been going through.
 

Basi na wewe huwezi kufananisha ubovu alio achiwa van gaal na ubovu alo achiwa mourinho.

Niliulizwa kocha gani alofanya vizuri ndani ya miez mitatu, sasa ndio nikajibu hao, na sijadanganya.

Zidane aliachiwa timu ya tatu, mou kaachiwa timu ya tano.
Zidane kasogea 1,
Mou karudi 6.

Sasa sijajua namuoneaje Mou
 

Sijaelewa swali kaka
 
Sawa Ntunzu wewe unamuelewa mourinho lakini sio kwa ligi ile emb apewe vilago atafute pakutulia pale England pamesha mshinda
 
Jamaa unajua kupulizia hahaha
Sio kujua kupuriza Utd hawana ma DM hiyo ndio shida kubwa. Viungo wote wameshindwa kuleta ufanisi anaoutaka Mourinho ndio maana back line inaonekana legelege na huko mbele kunasuasua.
 

Tatizo kubwa Mourinho unamfanyia assessment baada ya mechi 14 hao wengine unawafanyia assement baada ya msimu mmoja.Nimekuomba ulete statistics za hao makocha walichofanya ndani ya miezi 3 unaniambia ni-google
 
Khaaa!!
Alo kwambia nani kuwa zina strugle!?
Chelsea ana 34
Arsenal 31
Liva 30
Man city 30.

Sasa hilo gap mbona la kawaida na la ligi kabisa.

Man utd.... 21- hiii sasa ndio ina struggle

Kutoa sare siyo kugain point moja ni kupoteza point mbili, na man utd hawawez wakajiteta et kwa kuwa wana toka sare.
 
Alimaliza wa pili mwaka jana, hata ndio kashuka but hafanyi vibaya kama Mou.
Na ukizingatia ni kocha wa Calibre ya kawaida kabisa, he is good.

Mbona hawa makocha wengine wakishuka unasema ni sawa but Mourinho sio sawa ?
 
Matatizo yaliyokua kwa Chelsea yalikua sio kocha Bali ni wachezaji na mtandao Wa hujuma Wa waingereza dhidi ya Mourinho maana mpira hauna ushindani uwanjani tu Ata huko nje kuna ushindani na interest za watu kibao tu. Ukilijua hilo halitokusumbua. Hii hali ilimkumba sn Mourinho akiwa Chelsea lkn kwa sasa akiwa Utd imeanza kupoa kidogo.
 
Khaaa!!!
Nimeangalia mechi za Swansea city na Hull city huwa wanafungwa na wana sikitika kweli, kigezo cha wachezaji kusikitika hakiwezo kutuambia kuwa hii timu iko vizuro kaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…