Manchester United (Red Devils) | Special Thread



Mkuu herrera kwanza ni lazima ufahamu kipa ni sehemu ya wachezaji so David de Gea ni mchezaji wa Man Utd.Pili unatakiwa ukubali mchango wa Van Gaal wa kumbakiza de Gea kikosi wakati Real walipokuwa wanamyemelea kwa kasi ya ajabu.Pili fahamu ni Van aliyecheza karata ya kumsignisha mkataba mrefu ambao kama Real watamtaka itabidi wavunje kibubu.

So far Man imebakiza mechi mbili ambazo tukishinda zote tuna uhakika na nafasi ya nne (it's within our reach) na usisahau FA Cup tuna nafasi kubwa pia.

Nakubaliana na wewe msimu huu tumefunga goli chahche sana,lakini tunasahau msimu uliopita mashabiki wengi walikuwa wakipiga kelele Rooney aongoze safu ya ushambuliaji bahati mbaya kiwango chake msimu huu kilitetereka sana na pai kuumia hilo si kosa la kocha bali hiyo ni sehemu ya mpira wakati mwingine unawaza hivi matokeo yanakuwa tofauti.

Tukubaliane majeruhi wengi walichangia timu kutetereka sana,bahati mbaya hilo halisemwi sana hasa na vyombo vya habari vya UK ambao ajenda yao kubwa ilikuwa ni ku attack mikakati yote ya Van Gaal.Mfano vyombo vingi vya habari vya UK vimekuwa mstari wa mbele kumponda Van Gaal katumia 250 million lakini havisemi kauza wachezaji wangapi ?.Ni kwanini hawasemi 250 less wachezaji aliwauza na wengine waliondolewa kwenye payroll ?Fedha kiasi gani zilipatika kwa mauzo ya Di Maria,Fletcher,Chicharito,Rafael,Nani,Kagawa,Evans,Welbeck & Cleverley.

Mashabiki wa Mourinho wanasahau mafanikio yote aliyopata Chelsea yalitengenezwa na Ranieri ambaye kaonyesha kipaji cha hali ya juu kwa kuchukua ubingwa kwa bajeti ndogo sana.Nauliza Mourinho alipokuwa Spain alitawala ligi ya kule alichukua vikombe mara ngapi ?.
 
Mkuu labda tuzungumzie kuhusu kuwatoa wachezaji kwenye payroll, lakini suala la transfer market tupo hovyo sana, tunanunua wachezaji kwa bei mbaya na kuwauza kwa hela ya nyanya,

Tumetumia £250+ mill ila tuliowauza haizidi £35 mill

Nani 4 mill
Rvp 3.85
Rafael 2.10
Cleverly free
Fletcher free n.k hizo ndio bei tunazouzia,

Kuhusu mou kwamba mafanikio aliyoyapata Chelsea timu ilijengwa na ranier it might be true, but vipi kuhusu timu zingine anazofundisha?

Katika misimu mitatu ya Madrid, Madrid ya mou iliongoza kwa magoli dhidi ya barca kwa misimu miwili mfululizo, msimu wake wa kwanza alipigwa tano na barca nou camp, alipoteza nusu final, ila alichukua CDR mbele ya barca,

Msimu wa pili walichukua la liga ila walipoteza CDR, wakati wanachukua la liga waliweka record ya kuchukua ubingwa kwa point nyingi, hata Chelsea yake ilifanya hivo. Chelsea msimu uliopita iliitandika Swansea goli tano, sina kumbukumbu kama kuna mechi timu ya van gaal ilimpiga mtu hizo goli.

Mou kachukua ubingwa Mara 8, katika vilabu na nchi 4 tofauti ndani ya miaka 13 iliyopita, unaikumbuka inter yake iliyochukua treble? Kwenye CL iliitandika barca ya pep, ikaitandika na bayern, ana champions league 2 na dozen ya makombe mengine ya mbuzi, kuharibu kwa mou miezi sita sidhani kama ni guarantee ya kusahau CV yake Mkuu.
 

Mkuu herrera fedha za Di Maria haijaziweka ni maksudi au bahati mbaya ?.
 
I have my motto "Tutafika tu"......."bado mechi mbili UCL tutafika tu"........ahhhhhhh hiii misimu mitatu cha moto tumekiona!!!......Eee tunashukuru kwa yote tunasonga mbele.
Kwa sasa usi-aim too higher...hii team haitatengamaa kwa siku moja au.mbili...
 


Nimecheka sana asee....Eti unasema? uko uvunguni na Livescore?
 
Nasubiria nisikie Mourinho katangazwa kuwa kocha ili nika renew membership card yangu ili nianze tena kwenda uwanjani..
Kiukweli tunahitaji kushinda kombe kubwa ili kurudi Kwneye hadhi yetu.
 
LVG: Points before a party

"Tuesday we have to play against an opponent who says goodbye to the stadium. So they won't want to lose in their own stadium.
They have already lost to Man United in the FA Cup match. That is also history. That is not good for us. And West Ham United is a very good
team.
We have a lot of respect for West Ham. I think it is a historical big club in England and so we don't want to spoil their party but we need the three points and that is different."
 
Dah Woodward unazengua Hummels uliishia tetesi tu Renato Sanches dogo wa Benefica ukatuaminisha end of season sasa naona Bayern waishajibebea tu wachezaji wote...hivi MUFC itakua timu ya kupoint wachezaji mpk lini
 
Babu anatakiwa kuondoka haraka sana mara baada ya msimu huu kumalizika.

No matter what, kachukua FA au kaingiza timu UCL, Hatufai amesha-prove uwezo wake mdogo ktk ufundishaji kwa miaka ya leo. Kitu kibaya kwa kizazi cha sasa hakitaki historia, ndiomaana Arsene anapigiwa kelele pale Emirates bila kujali kikosi chake cha Invisible huko nyuma. Historia imeshindwa kumbeba Mou pale Darajani mpaka kuondolewa licha ya mafanikio makubwa aliyoyapata huko nyuma yaliyomfanya kuimbwa na Mashabiki na wachezaji wa timu hiyo.

Timu ya sasa ya United inamtaka kocha kama Mou angalau kwa misimu mitatu. Timu imejaa wachezaji wavivu na goigoi wasiojua thamani yano na Timu uwanjani. Falsafa Mourinho ktk kufundisha soka haitofautiani sana na SAF ingawaje babu alikuwa akipenda kwenda na washambuliaji wawili ilhali Mou anacheza na mshambuliaji mmoja. Lakini ukija kwenye hamasa ya Timu, Usiriasi na Management hawa watu hawatofautiani.

Ktk miaka yake 26 pale OT hakuna mchezaji aliyewahi kujiona yuko juu ya SAF au Timu. Kila mmoja alitimiza wajibu wake itakiwavyo. Asiyetaka kuendana na Timu au kocha alifurushwa...!!! Hivyo ndivyo alivyo Mou. Tatizo moja tu lililoko bayana kwa Mou, ni kushindwa kulea Vipaji vinavyotengenezwa na Timu, yeye anataka wachezaji ambao wako tayari kwa Mapambano. Lakini sisi hatumtaki Mou kama kocha wa Kudumu, hapana. Sisi tunamtaka yeye ili kuturudishia heshima iliyopotea kwa miaka minne sasa inaenda tangu kustaafu kwa Babu pale OT. Tunaamini kwa nguvu zote kazi hii Mou anaiweza

Tumpe nafasi.

BACK TANGANYIKA
 
sie tunasajiligi kwa tetesi tushazoea

yani hovyo kabisa dirisha lilikaribia kufungwa ndo tunakimbilia michezaji ya hovyo halafu saiv man utd itapata tabu sana kusajili mana wanajua tunataka wachezaji wa viwango bei zao zitakuwa kali sana huyo renato man alikuwa anamtaka tukatajiwa euro 45 had 50 wakat bavaria wamempata kwa 28 nakumbuka vidal ilikuwa hivyo hivyo bavaria wakampata kiurahis sana hata kiuhalisia bei ya martial ilikuwa kali sna ile ilikuwa ni risk ila bahat nzur kafanikiwa tuombe mungu aendelee ni hii fom yake
 
Timu ya sasa ya United inamtaka kocha kama Mou angalau kwa misimu mitatu.

BACK TANGANYIKA
Sasa braza, baada ya misimu hiyo mitatu, what next? Kama unataka kusema kwamba baada ya misimu mitatu timu itakaa imara (baada ya kushinda makombe chini ya mpiga domo), una uhakika gani na hilo? Kwanini timu isitafute mchezaji anayeweza kukaa na timu kwa muda mrefu na kujenga filosofia yake?
Pengine nieleweshe, yaani unataka mpiga domo aje kuipa makombe United kisha aondoke zake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…