Manchester United (Red Devils) | Special Thread


..khaaa!!!..na weye mtani wangu leo ulikua wapi hii gemu yote?...Manda peke yake ndiye alikua hapa jamvini tukimpiga tafu maana alikua keshaanza kuwatusi wachezaji wa Man U... wengine m'mejitokeza baada ya gemu kuishia draw...tumbo joto!!!...LOL!

..afu pia una kauzalendo flani...eti 'we never die'....mmmhhh???

Leo mumeponea sio siri. Kuna goli mbili za wazi jamaa wamepiga mwamba...ndo hapo nilitaka kuamini mna kamati ya ufundi
kutoka sumbawanga.
 
Mtani nilianza kuangalia mechi kipindi cha pili, jamaa wakanitibua nikabadirisha channel kurudi nikakuta tuko nyuma 2-0 nikawa nimekata tamaa. Ila kumbe jamaa walikuwa na ideas nyingine.
Kusema kweli mapenzi yangu ya soka na man utd yataniua nikiwa kijana maana msimu huu ni kasheshe tupu, ndio maana ata kuingia hapa wakati wa mechi siwezi tena mtu unakuwa na pressure mpaka mechi inaisha lol.

Ila unazi pembeni watani ile spirit waliyoonyesha vijana dakika 15 za mwisho ndio what defined manchester united miaka ya nyuma and to be honest we are lacking that fighting spirit msimu huu.

Kamati yetu ya ufundi ikiamua kufanya kazi inafanya vizuri sana tu hehehe.
 
Sijasema mmebebwa, nilichouliza ni kwanini refa hakumpa kadi Vidic lakini akampa kadi Young kwa kosa linalofanana?! Labda wewe unaweza kueleza ni kwanini?

Refa alikuwa stunned na come back mjomba mpaka akasahau kadi alikoiweka.
 

Lile shuti la macheda lilikuwa la kua mtu zingekuwa nyavu zetu za uswazi lazima mpira ungetoboa nyavu.
 
Acha ushabiki kama umeangalia game yule refa alikuwa anawabeba sana Vila NANI kachezewa rafu mbili za hatari but refa hajatoa kadi,
 
Hii ndio Manchester mbovu tangu nimeanza kushabikia hii timu, CARICK,BROWN,OSHEA hawana chao tena .Hapo kati hasipokuwepo babu SCHOLES timu inakuwa kimeo pamoja na matatizo yote hayo eti anayeongoza ligi amatuzidi point 6
 

Bruh!...acha majungu bana, mlikuwa mnanizodoa au mlikuwa mnanipiga tafu?, be sincere..BTW kwa utumbo wa manure ule wa dakika 80 hata SAF pia najua alikuwa anawamiminia "f" words from benchi, they were real disgusting bana. Pheeeeew!, kiukweli hali yetu si nzuri sana, nashangaa hata hiyo nafasi ya tatu tumeshikaje eti!?
 
Acha ushabiki kama umeangalia game yule refa alikuwa anawabeba sana Vila NANI kachezewa rafu mbili za hatari but refa hajatoa kadi,
Umeongea ukweli,hata Ji sung Park,sitetei 7bu ya Man Utd
 
Manutd yabidi ijirekebishe juu ya hizi sare haswa mechi za ugenini vinginevyo ubingwa watausikia kwenye bomba...............
ligi bado mbichi kaka,hao wanaotoka sare na man utd,utakuta wamewafunga chelsea,arsenal,liverpool au man city,mechi ngumu,aston villa hajapoteza mechi nyumbani msimu huu,man utd ni miaka 15 hajafungwa hapo villa park.
 
Usijali sana, hata mabingwa walipata sare hapo Villa Park.
wakachapwa 0-3 darajani stamford jana j2 na timu inayofundishwa na nahodha wa zamani wa man utd,hadi leo ktk comments zako unaongea lugha mbalimbali umesahau kisambaa tu,muinuke zeze!
 
Hii ndio Manchester mbovu tangu nimeanza kushabikia hii timu, CARICK,BROWN,OSHEA hawana chao tena .Hapo kati hasipokuwepo babu SCHOLES timu inakuwa kimeo pamoja na matatizo yote hayo eti anayeongoza ligi amatuzidi point 6
sio mbovu sema sisi washabiki ndio ugonjwa wa moyo,mbovu haijafungwa toka august mpaka leo ktk michuano yote,na haijaruhusu goli ktk uefa champs ligi ni rekodi hiyo na kumfunga valencia kwao,ya wakati ule watu walikuwa wanasema anaejua chenga ni Giggs tu,Beckham wanasema sio mchezaji hajui chenga,sasa hivi mnasema sijui Fletcher,Carrick,Brown na Oshea wabovu,wapi jamani,mwacheni babu SIR anajua nini anachokifanya.
 
Wanazi wa man ukeli ni kwamba sijawahi kuiona manutd kama hii ya sasa imebidi nilipie Dstv niangalie mpira nyumbani kwenye mabar nashindwa kuvumilia nataniwa mpaka nakasirika natamani nimtwange ngumi Sir alex kwa kushindwa kusajili wachezaji wa kiwango.Tayari nimemsikia akibwabwaja hatakuwa na mpango wa kusajili dirisha dogo ?.

Manchester United inahitaji wachezaji wawili wa kiungo hata kama hawatakuwa na msaada mkubwa msimu huu lakini watazoea mazingira na uchezaji wa man.Evra na Vidic ni mfano mzuri wa wachezaji waliosajiliwa dirisha dogo baadae wakaja kuisaidia sana timu.Kuna baadhi ya wachezaji watatakiwa kuondoka mara moja.John Oshea,Garry Neville,Carrick,Giggys na Barbaflop.Scholes apewe mkataba wa mwaka mmoja wakati replacement akijiandaa kuzoea mazingira.
 
Hii ndio Manchester mbovu tangu nimeanza kushabikia hii timu, CARICK,BROWN,OSHEA hawana chao tena .Hapo kati hasipokuwepo babu SCHOLES timu inakuwa kimeo pamoja na matatizo yote hayo eti anayeongoza ligi amatuzidi point 6

Kwani ulianza lini kushabikia mashetani wekundu? Mlikutana na watoto watukutu tu.


Usijali ndio kabumbu hilo .... .... upo kwenye EPL
 
Msimu wa 98-99 tulikuwa na point 25 baada ya mechi 13, i doubt hii timu itakusanya point 65 katika mechi zilizobakia.

Tatizo liko kwenye midfield, wachezaji kama Carrick na Fletcher hawajarudi kwenye form ya season zilizopita na inconsistence yao inaumiza mabeki na strikers, hatuboss midfield kama season zilizopita. Ili tatizo linafanya strikers wasipate service na hii kitu inasababisha akina berbatov et al kurudi deep kutafuta mipira. Tunatakiwa tupate mtu kama Bastian Shweinsteiger.

Ngongo quality player tutakayemnunua dirisha dogo atatusaidia kwenye ligi ya ndani tuu kwenye cl atakuwa cup tied.
 


Going nowhere ..... ..... .......

''Sir Alex Ferguson has revealed that he is 'in no mood' to retire as Manchester United manager. ... ''
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…