Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Chicharito goli alilowafunga chelsea kwa pua ananikumbusha Giovanni Elber wa Bayern Munich mwezi wa 4 ktk nusu final 2001 pale santiago bernebeu kati ya real madrid vs bayern munich,real alilala kwake moja bila chini ya kocha wake Del Bosque akipambana na kocha Ottmar Hitzfeld wa Bayern enzi hizo(kamfunga tena spain vs swiss world cup 2010)Real Madrid ikiundwa na mastaa kina Figo,R Carlos,Hierro libero,Raul,McManaman,Solari,Ivan Helguera,Salgado,Karanka na Casillas alifungwa bao dk inakimbilia 75 la ugoko na Elber,sitosahau Bayern ilikuwa ya ukweli na Real ilikuwa really,kwanza robo final Man Utd kafungwa na Bayern home and away Paulo Sergio old trafford dk 85 1-0,na akafungwa 2-1 Munich,Elber na Sergio tena,Man alifunga Giggs 2nd half ht walikuwa 2-0 tayari,semi Real akala nae 1-0 kwao Madrid,Elber kawaua,na akaenda kula 2-1 nakumbuka Jens Jeremies alilipiza kisasi cha kujifunga msimu ulioisha semi final 2000 vs Real pale bernebeu walipochapwa 2-0 na Anelka alifunga kwa Real marudiano japo walishinda Bayern 2-1 Anelka aliwafungia Real bao pekee na wakapita kwa 3-2 jumla na kuingia final vs valencia wakashinda 3-0 na kubeba ubingwa Real Madrid, maana ktk makundi Real alipigwa 4-1 Munich,4-2 Madrid kabla,na kupita wote Real akaja kumchapa Man Utd 3-2 kwao trafford baada 0-0 bernebeu,sasa safari hiyo 2001 ktk semi bayern akalipa kisasi kwanza kwa man utd ile 1999,halafu akaja real nae akala 1-0,2-1 Figo aliwafungia bao la kufitia machozi kule Munich,final wakamfunga valencia kwa penati,valencia enzi hizo gaidzka mendieta zabala,pablo aimar,zlatko zahovic,john carew,reuben baraja,alberda,miguel angelo angulo,joseph angloma,santiago canizales golini,kily gonzalez na kina claudio lopez alienda lazio yeye na ortega akaenda parma,gerard lopez akaenda barca,barca ilichezea 4-1 ktkt nusu final 2000 pale mestalla kina Figo,Luis Enrique,Rivaldo,Dani Garcia Lara,Kluivert,Pep Guardiola,Xavi enzi hizo chipukizi chini ya kocha wao Louis Van Gaal(kocha wa Bayern sasa)wanashangaa,ulimwengu ulistaajabu maana barca alitoka kumchapa chelsea 5-1 nou camp baada ya kuchapwa 3-1 darajani,Rivaldo akaapa chelsea licha ya kushinda kwao wakiwatoa anaacha kucheza mpira,nimemkumbuka pia Mario Jardel de Almeida Ribeiro,huyu nae ni mbrazil ambae anakumbukwa kule ureno kwa kuweka rekodi ya kufunga mabao mengi akiwa na FC Porto alivunja rekodi ya kuwa mfungaji bora kule Ureno na ulaya kwa ujumla kwa kuunganisha ligi zote kwa miaka 3 mfululizo,aliemfuatia kwa magoli kule ureno yani wa pili aliachwa kwa tofauti ya magoli 20,yeye nadhani +-35,kisha anakuekuja 17,akaenda Galatasaray akabeba nao super cup kwa kumfunga Real Madrid,wao walikuwa mabingwa wa uefa cup1999-2000,Real walikuwa mabingwa champions ligi 1999-2000,ila yeye Jardel hakuwepo msimu wanabeba Galatasaray uefa cup 1999-2000 alikuwa bado yupo Porto,alipoenda Galatasaray mwezi june 2000,akakutana na kina Hakan Sukur,Umit Davala,Popescu,Hasan Sas,Emre Asik,Georghe Hagi na Emre (alienda Inter na Newcastle baadae)
Arsenal walifungwa na hawa kwa penati ktk uefa cup 1999-2000 kule Copenhagen,Denmark katika fainali,Vieira alipoteza penati ya mwisho.
 
Mapumziko tunaongoza kwa goli moja kutoka kwa Vidic. Hii bado ni open game.
 
to be fair to man u, kosa ni la kipa wa spurs gomez, refa hakuwa amepiga filimbi ya faulo,so mpira ulikuwa bado live (open play) sasa yeye ndiye mwenye makosa, hata kama utamlaumu refa kwa kutotoa faulo ya nani kuushika mpira lakini na yeye labda hakuwa ameliona tukio hilo na kwa kuwa hakupiga filimbi then gomez was punished, he was supposed to play with the referree's whistle and not his own judgement

a perspective from an arsenal fan

ila kiukweli man u they still far awy from being the team that used to be, Naona kudra za Mungu bado zinawasaidia
 

Poleni sana Man Utd. Naona leo wamewaandama sana ... ...




Are you kidding me? Tell me that you're joking?





Who has got the last laugh?






Msijali vijana nyie chezeni mpira tu huu mpunga niliopewa na Glazers

sio mchezo ni balaa tutaona kama Abraham O vich

anaweza ku-mech dau ... ..




Msinifuate fuate bana hamfahamu kuna recession?

Wacheni ngebe zenu!








Balaa lote hili alienzisha ni huyu dogo Vidic ... .... ati

wanamuita Ne-manje manje!

Ooops Nemanja phew!








Toto tukutu lilikuwepo linakula mpunga tu .... .... .






Soga haziishi tu?




 
Hongereni wakuu lakini hilo goli lenu la pili marefa wamechanganya habari kinoma lol.

Gomez ni mpuuzi, refa hakupiga filimbi kuashiria Nani kashika na kuwa faul, wala asst refa naye hakunyoosha kibendera kuashiria hivyo maana walijua kuwa ile ilikuwa ni penalt na waliiminya kuwapa Spurs advantage. Gomez kachukua mpira kauweka chini kuna tofauti gani kati ya kudaka na kutema halafu mchezaji anauweka kimiani?.
 
poa spurs wanawasubiri wawachape chelsea,maana hawana rekodi nzuri kwa arsenal na man utd,mara ya mwisho kushinda uwanja wa old trafford ni 1993,na kumfunga man utd ilikuwa 2000-2001 pale white hart lane 3-1 enzi za kina David Ginola,walishaongoza 3-0 white hart lane msimu wa 2001-02 mwezi wa 9 mwaka 2001 hadi half time,2nd half wakala 5,ikawa 5-3 walifunga,msimu wa 2008-2009,waliongoza 2-0 half time wakapigwa 5-2 pale old trafford
 


nimekugongea thanks mkuu kwa hiyo flashback...i loved it:smile-big:
 
Najua wengi wenu masikio yako kwenye matokeo ya uchaguzi ila ndio hivyo tumejipatia ushindi 3 - 0 dhidi ya Bursaspor.
 
Najua wengi wenu masikio yako kwenye matokeo ya uchaguzi ila ndio hivyo tumejipatia ushindi 3 - 0 dhidi ya Bursaspor.

Yaani hawa vibonde mmewafunga hizo tu? Kweli Manure hamnazo mwaka huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…