Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nimeisikia pia ila ngoja tuone time will tell.
 
Mkuu unachosema ni ukweli kabisa tumalizane na middlefilders kwanza, tupate beki moja ya kushoto na beki ya kulia. Hapa tunaitaji wachezaji angalau wasiopungua 5.
Wewe full backs gani miaka yote unashindwa kujifunza Cross muda wote ni kubabatiza miguuni pa watu kama sio miguuni ni kupereka mpira sehemu kusiko na wahusika inanikera sana hii.
 
Wewe full backs gani miaka yote unashindwa kujifunza Cross muda wote ni kubabatiza miguuni pa watu kama sio miguuni ni kupereka mpira sehemu kusiko na wahusika inanikera sana hii.
Yaan tuna vituko wengi sana mkuu, kama garter,zirkee sijui mpaka sasa
 
Auziwe mwarabu maana waingereza mabahili mno
 
IGHALO anampa Code Bwana mdogo, sema haya ndio nilikuwa nazungumzia kuhusu Man u na wachezaji tokea Africa kama sijasahau Mwaka wamemaliza Napoli kuchukua kombe Osimhen wamoto saaana Tulikuwa na shida ya Finisher tena mwenye akili timamu, Dogo akawa shida na kocha wake Man u hawakuona firsa ya kumcheck waka Deal na Hodjlund wakamuacha aende Galatasaray niliumia sana.
Hivyo basi kama mwaka huu wanahitaji sticker wa kukupa 16+ Goals kwa msimu na hapo Combo yake na El Magnifico haijawa vizuri sana huyu Jamaa atafaa ila ni Juu yao wataamua.
 
Dogo Yoshua Z ubishoo mwingi mpaka kwenye kumaliza mpira anapiga kijishuti kama cha marehemu Sharo Milionea hizi Assist Records za Bruno alikuwa anazimalizia Yeye ile Game ya Nottingham, Jitu kama Ugarte likiingia tu Baasi Goli zinarudi tena.
Ila shaolin monk 10 hag ametuharibia sana club yetu.
 
Dogo Yoshua Z ubishoo mwingi mpaka kwenye kumaliza mpira anapiga kijishuti kama cha marehemu Sharo Milionea hizi Assist Records za Bruno alikuwa anazimalizia Yeye ile Game ya Nottingham, Jitu kama Ugarte likiingia tu Baasi Goli zinarudi tena.
Ugarte sijui anatokea Uruguay ya wapi! Na sidhani hata kama tulifanya scouting juu yake, kabla ya kumsajili
 
NtYga fuentte baada ya kumsikiliza fabrizio romano niseme tu bodi ya West Ham inahitaji vichwa vyao vikaguliwe kwa uthamini huo wa pauni milioni 85 kwa mateus fernandes baada ya kushushwa daraja.

Kwa sababu westham walimnunua kwa kwa pound 38m, adds on 4 for total package ya 42m. kutoka Southampton iliyoshuka daraja mwaka 2024, Inakuaje watake pound 85m. Hapa nitashanga kama tukitoa hiyo hela, Thamani ya mateus fernandes ni 55m adds on 5 jumla 60m isizidi 65m just take it or leave it.

Bila hivyo tukienda kwa Newcastle tumchukue Lewis hall tutapigwa pound 90m na tukija kwa tonali tutambiwa 100m au juu maana city na arsenal pia wanamtaka. Nipo tayari kukosolewa ila ni bola tukatae kupigwa ijapokua tusipojipanga vizuri msimu ujao tutadhalilika tukiwa na Carrick.
 
Mkuu King faisal umenena jambo jema sana. Westham bado wana dhana ya kwamba Man Utd ni splashers kwenye soko la usajili kama ilivyokuwa zamani. kitendo cha kuwagomea BHA kwa gharama ya pauni 100 kwa Baleba msimu uliopita, kumnunua Dorgu kwa pesa ya kibahili hata kipindi tuko kwenye uhitajiwa mkubwa na wa haraka ni dalili kwamba hatuendi sokoni kuibiwa bali kununua bidhaa kwa thamani sahihi.

Hata sasa huoni tukigonga vichwa vya habari sababu ya wachezaji wakubwa sana ila sajili zetu kiasi zimekuwa kama sapraizi. Ingawa bado naamini utaratibu ule ulikuwa unaongozwa na Amorin ila sijui kuhusu misimamo ya Carrick na staffs wake.

Kumbe tuko wengi ambao bado tuna tahadhali na ujio wa Carrick kama kocha mkuu bila kujali mafanikio ya mwendokasi aliyotupatia msimu ulioisha. Tujipe muda na tuombe FERNANDES awe kwenye form yake mkuu
 
Ni kweli kabisa mkuu, kwa alipotufikisha Carrick ni sehemu nzuri. Lakini bado ni mapema sana kusema tuna kocha bora. Maana msimu ujao tutakua na mechi nyingi sana, mie nipo pamoja na uongozi. Hata kama tutamkosa fernandes,tonall na hall ni sawa tu kuliko kupigwa. Nina imani tukitumia njia ya amorim, tutapata wachezaji wazuri tu watakopigania timu na kutufikisha sehemu nzuri msimu ujao.
 
Euro 85m kwa Mateus ni kubwa Sana kwa ninavyoona Bwana mdogo anayo Thamani ya Euro 55m nikipanda saaaana ni Euro 63m mwisho, Haya maswala ya kutuchukulia Advantage Juu ya uhitaji wetu wa Midfielders watajikuta msimu ujao wanafukuza Sporting Director kama Brighton walichofanya baada ya kukataa Euro 75m za Baleba.


Sando Tonali ninampa Market Price ya Euro 80m mpaka Euro 95m sina sababu za kuvuka hapo Pote ijapokuwa TunaJua Signing ni Gamble Japo Tonali ni Bidhaa inayojiuza na imethibitishwa.

Kuhusu Carrick Ndugu zangu mimi simuamini sana maana hata ukiangalia hizi Game tume Draw nitulihangaika sana ni vile Spirit ya wachezaji tu na Mungu mwenyewe kutuona Kwa jicho la huruma Pia Game ya Nottingham tulikuwa wazi sana Second half mpaka nikawa nahisi tunaenda kupoteza maana kulitokea msako muda flani mpaka nikawaza Kheri twende Europa Tukajenge huu msimu unaofuata.
Maana vita tunayoenda kuipigana ni Madagascar vs Russia.
 
Mkuu unachosema ni kweli, unajua kama ingetokea tungeshinda ile fainali ya Europe dhidi ya Tottenham. Sijui nini kingetukuta msimu huu ulioisha. Baleba msimu huu sijaona akifukuziwa, na Manchester United, pamoja na vilabu vingine ukiacha ile kauli ya wachezaji weusi, itakua hajaperform vizuri EPL msimu huu ulioisha.

Tukija kwa tonali nakubaliana nawew anafit na kutufaa sana, Newcastle wasipotufanyia roho mbaya tumchukue pia Lewis hall. Michael Carrick kwakweli niseme pia simwani lakin siwezi kujudge mapema hivyo time will tell.
 
Kuna muda ninaona kama tunatumia nguvu kubwa sana kwenye hili dirsha na Pesa sio zetu mfano Dirisha la msimu ulioisha kule mbele walitumia Karibu Pauni 200m au 200m na kidogo kulete Mateus Cunha, Bryan Mbeumo na Benjamin Sesko na imetulipa karibu 77%.

Na Tukiangalia Budget yao ya Dirisha hili ni Pauni 300m, hivyo basi Tufanye kujiripua msimu huu pia kwa Kutengeneza haswa ukuta wa kati (Midfielders) Tuchote tena Euro 200m kwenye hiyo Euro 300m, ko kwenye 200m Tushachukua tayari Ederson 35m inabaki Pauni 165m Roughly Chukua TONALI Pauni 95m malizana na Mateus Fernandes Pauni 70m tunakuwa tumemaliza.

Tunabaki na Pauni 100 tukichekecha kabisa hatupati Beki ya kushoto na Stricker ili iwepo Backup ya Sesko na huyu mwenda wazimu Shaw.


NI MAWAZO TU MSINITUKANE😄.
 
Hapo kama rashford,ugarte, na zirkee wakiuzwa, pia nimesikia fernabache wanataka kumnunua mason greenwood na hapo pia kuna share ya Manchester United, hivyo 100m itaongezeka na pia tunaweza kupata angalau beki ya kushoto na stricker.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…