Kuna kipindi pale Arsenal tulikua tunataka Stan Kroenke aachie timu agewe mtu mwingine. Miongoni mwa watu walioitaka Arsenal alikua Dangote na mmiliki wa Spotify.
Kroenke akagoma kuuza. Dangote akarudi kukomaa na viwanda vyake na jamaa wa Spotify akaenda kupambana kuimiliki Barcelona.
Kipindi hicho ilikua Arsenal tunaweza kosa mchezaji kwakua anauzwa 45M au 50M. Arteta ilibidi afanye kazi na aliowakuta, wakina Mustafi, Guendouzi, Ceballos na Odegaard kwa mkopo, Sokratis, Bellerin aliyetoka majeruhi, Xhaka asiyejiamini, Cech n.k.
Kroenke akawa anagoma kutumia pesa akidai kwamba anataka timu ijiendeshe, itumie inachozalisha. Mashabiki tukaona anaongea upuuzi kwakua katika timu yake nyingine anayoimiliki ilikua haijiendeshi kwa mode hii. Kwanini akomae Arsenal tu ndiyo ijiendeshe hivyo?
Mashabiki wakaanza riots.
Tuje kwa United, wana wamiliki ambao ikatokea mchezaji anaongozwa na pesa na siyo ile kutaka kucheza timu fulani pesa hua inatoka. Kwa uzoefu wangu na observation mchezaji ambaye alifocus na pesa aliletwa United bila shida, Pogba, Martial, Fernandes, Amad, Mbeumo, Cunha, Sesko, Dorgu, Onana, Ugarte, Casemiro, Mazraoui, De Ligt, Sancho, Yoro, Heaven, Martinez, Malacia, Van De Beek, Antony, Chido n.k.
Hao ni wachezaji ambao kocha alipoint na wakaletwa. Ronaldo alirudi siyo kwa mapenzi ya kocha ila alirudi baada ya mashabiki wenyewe kuentertain hilo swala online.
Mtu anasema bora aje mmiliki mwarabu, ndiyo atafanya nini cha tofauti kwa anachotakiwa kufanya mmiliki? Kwani Newcastle mnajua inamilikiwa na nani? Wanaspend kama wapumbavu ila wako wapi? Mnahisi mmiliki atasababisha timu ikabe? Atasababisha wachezaji wageane pasi kwa wakati?
Chelsea walimleta Tuchel na alipofika tu alisema anachotaka. Akacheza back three akaondoka na CL, akiwa na wachezaji ambao Lampard alisema hawa na ubingwa ni maji na mafuta.
Amorim amefika United anacheza back three, mtu wa Hayloto Mbulu anasema huyu kocha hajui kitu back three bila wachezaji wa kufit mfumo itakutesa. Na yeye akapita na hilo gap. Kwakua it doesn't matter mchezaji kama una LB huyo ni LWB una RB huyo ni RWB so huwezi sema huna wachezaji wa kufit mfumo.
Mashabiki wa United hawajui mpira, hayo ni maneno ya Pogba, unashuhudia hayo kwa wanavyomhukumu kocha na wamiliki. Peronally kocha mtengeneza nidhamu namhofia kwakua once ukicheza na timu ipo disciplined wewe kuondoka na matokeo haiwezi kua easy.
Na Amorim alikua anafanya hili kwa bidii, sasa kwakua hamjui mpira mnahisi shida ni Amorim, kaondoka. Shida ni mmiliki? How? Mnasema kocha hapewi full authority? Ipi? Ronaldo aliwekwa benchi na kocha hakuhojiwa, a club legend. Bench. Na kocha hakuhojiwa.
Kocha analilia wachezaji aliowatumia Uholanzi, kaletewa. Kisha hawatumii na hajaulizwa. Unanunua starters wa Bayern, PSG na Atalanta na hauwatumii na haulizwi. Wewe mkazi wa Kinyanambo C unataka mmiliki afanye nini sasa?
Umelilia Amorim afukuzwe ili ucheze back four kafukuzwa umecheza back four na umenyooshwa unataka mmiliki aondoke. Kwa ishu ipi sasa?
Safari bado ndefu hadi mjue mlimhitaji Amorim na mlitakiwa mumpe muda awanyooshe hao viazi ambao kaka zao hawaamini kua wanatakiwa kukaa bench wajue kupambana.
Ndugu yangu, ze dudu, anakuambia anaona nafasi pale juu. Kimahesabu Wolves pia anaweza kumaliza ndani ya top four. Arsenal tulihitaji ushindi dhidi ya Brighton ili kuingia international games tukasuluhu. Hatukwenda.
Tulihitaji points 3 kwenye mechi zaidi ya nne ili kwenda CL au Europa na hatukwenda. So mahesabu yasikutie majaribuni ukajipa matarajio makubwa.
Muwe mnatumia akili