Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Pole sana karibu Liverpool
 
Kwa muda Ferguson alioondoka timu ingeweza kua na identity mpya.

Hizi lawama unapeleka kusiko
 
Nasikia lawama sasa hivi zimeanza kupelekwa kwa Casemiro
 
M
Malalamiko fc...
 
Ngongo Natoa ushauri kwako. Kwa kuwa wewe sio mtu wa kuvumilia mapito magumu nakushauri uamie Man City sababu kule kuna raha.
Bakumbuka ulipohama toka Arsenal ulitoa sababu kama 5 hivi. Na ni muda mrefu sasa umepita. We huoni kama huko United unaweza kupata magonjwa ya moyo? Pressure, kiharusi, kikosa furaha nk?
Natoa ushauri nenda city au liverpool.
 
Kwa muda Ferguson alioondoka timu ingeweza kua na identity mpya.

Hizi lawama unapeleka kusiko
Babu anaondoka katuachia mfumo wa 442 lawama zangu hapa alipaswa kubadilika kiuchezaji kama mwenzie wenga toka pale game ya wembley aliyotetemeshwa

Hivi unajua kipindi kile aseno tulikuwa tunamfunga kiujanjaujanja tu na sio soka la uwanjani maana walikua wanacheza mpira wa pasi na unaovutia mno ambao ndio msingi wa soka la leo na ndio maana kuna mechi tulichezesha mabeki saba........wenga aliibadilisha aseno kutoka soka la ovyo mpaka hili soka tamu unaloliona leo.....tunamfunga aseno ila ukiangalia umiliki wa mpira baada ya full time unachoka😃😃😃
Yule mzee huu mpira wa leo hakuuona kwenye maono yake na ndio unaotupa tabu mpaka leo kuucheza tunaishia fukuza makocha tu
 
Kocha wa maana anahitaji msimu Moja tu kujua anacheza vipi na wachezaji gani kitendo Cha kutaka kuhamisha timu ya ajax ije united ni tatizo Moja wapo anakusanya wachezaji wake wa zamani kibao wasio na maana ni dalili ya mtu kuishiwa.
Haiwezekani msimu wa 3 huu tunaruka ruka tu uwanjani halafu mseme Fergie, huu msimu kipara Hana pa kujificha kashaletewa karibia 50% ya ma x zake wa ajax atuoneshe sasa umwamba wa vijana wake uwanjani.
 
Kama nakumbuka vizuri Arsenal imekua na infield technical nzuri kabla hata ya Wenger.

Graham alileta mapinduzi ndani na nje ya uwanja kwa Arsenal. Ferguson hana kosa
 
Kama nakumbuka vizuri Arsenal imekua na infield technical nzuri kabla hata ya Wenger.

Graham alileta mapinduzi ndani na nje ya uwanja kwa Arsenal. Ferguson hana kosa
Kweli kabisa huwezi kumlaum Fergie miaka mingi sasa watu wanapewa kazi wanazingua.
 
Karibu The Gunners kwetu soka ni burudani,hakuna butuabutuaaa ni kheiri tusishinde ila pass zipigwe mpaka ndani ya 16 na hatuna stress 😬
 
Man u kocha tu ndio kiazi, sio babu Wala mifumo sijui, maana kizazi chababu hakuna pale.

Sisi arsenal pila linapigwa sema vile tunambwela mwishoni.

Sent from my itel P32 using JamiiForums mobile app
 
Wew umeijua Siri karibu
 
Kwenye goli la pili Casemiro anapoteza mpira, anadondoka, ila nyuma yake kuna wachezaji 5 wa nyumbu. Liva inaingia kwenye boksi ikiwa na wachezaje 3 dhidi ya 5 wa nyumbu

Wanashindwa kuzuia linafungwa goli.

Shabiki anamlaumu Casemiro.

Sikumbuki mara ya mwisho ni lini kuanzia 2021 Arsenal kafungwa goli la ndani ya box huku ana wachezaji 5 kwenye boksi na siyo kona wala faulo. Na siyo Arsenal pekee, timu nyingi huwezi kuzifunga ikiwa ni 3 against 5

Erik kichwa ngumu siyo kocha.
 
Sawa, sasa tunamsubri INEOS hao ndio maboss sio wewe.
Ana makombe ambayo sio kivuli chake lakini inahitaji tathimini nzuri kabla ya kumfukuza.
Swali: arteta akimaliza trophless msimu huu wewe unapendekeza Nini?? Abaki au afukuzwe?
 
Sawa, sasa tunamsubri INEOS hao ndio maboss sio wewe.
Ana makombe ambayo sio kivuli chake lakini inahitaji tathimini nzuri kabla ya kumfukuza.
Swali: arteta akimaliza trophless msimu huu wewe unapendekeza Nini?? Abaki au afukuzwe?
Kwa Uingereza Erik ana makombe gani?

Arteta ana makombe gani?

Sioni kama Arsenal tunatakiwa kuja kumshika shati Arteta kisa makombe. He is beaten by Pep, money and arm twisting tactics
 
Kwa Uingereza Erik ana makombe gani?

Arteta ana makombe gani?

Sioni kama Arsenal tunatakiwa kuja kumshika shati Arteta kisa makombe. He is beaten by Pep, money and arm twisting tactics
Mna visingizio sana linapokuja suala la kumtetea Arteta. Wakisema uweke wazi ushahidi wa haya madai yako nina imani utaishia matamshi ya kukisia tu.
Kidogo nilianza kukuunga mkono uliposema ameshindwa na Pep (kwa kigezo cha ubora) ila ulivyochomekea suala la pesa (utadhani ninyi mnasajili bure) na match fixing nikajua unaongelea ushabiki zaidi.

Ifike mahali tukubali kwa umoja wetu kuwa Pep ameset standard kubwa ya alama ili uweze kuwa bingwa wa EPL. Kwa alama zenu za misimu miwili iliyopita bila uwepo wake, Arsenal mngalikuwa back to back champions ila ndio hivyo jamaa anatunyanyasa collectively.

Hadi sasa bado hakuna kocha EPL wa kumchallenge Pep convincingly, tunabahatisha tu, Ngoja tumpe Slot muda ila sio arteta wenu wala Ten hag wetu.
 
Madrid walimtaka Haaland akatua City. Hakuna anayejua signing bonus ya jamaa, mshahara wa wiki wala performance bonus.

Mimi nimeandika ninachojua kwa kila nilichowahi kusoma. Kama kuna sehemu una taarifa kunizidi ni sawa kwakua taarifa zinatoka sehemu mbalimbali.
 
we
we bado hujaama timu tulia dawa iingie ....hakuna kitu kigumu kama kuhama timu moyo uliyo chagua hapo akili inakuambia ushahamia Liverpool ila roho bado ipo unyumbuni na hili jambo lipo kwa man utd fans haupo peke yako

utakuta tu wapo wana shabikia na mpaka kuwa na jezi za timu nyingine mfano city arsenal Chelsea lakini kipimo cha kuwa bado timu ipo rohoni inapozidi kufanya vibaya una umia mno ilihali upo timu nyingine na pia inapofanya vizuri unajikuta unatembea kifua mbele hata kugombana na mtu anaye taka kuchukulia poa progress ya timu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…