Mamlaka ya Mapato (TRA) waongeze nguvu katika vituo vya kula chakula barabarani kipindi cha safari

SuchNoble

Member
Apr 13, 2014
13
11
Nafikiri kwa msafiri yoyote anayesafiri kwa kutumia either mabasi ya abiria au usafiri binafsi atakubaliana na mimi kuwa vyakula katika hoteli za njiani (stop overs) vinauzwa at a very premium prices.

Sasa hoja yangu sio bei ya kuuzwa kwa vyakula hivyo, hoja yangu kubwa ni je, Serikali inapata inachostahili kupata katika bei hizo ambazo raia wake tunaziingia?

Jana nilikuwa natoka Arusha naenda Dar es Salaam nikasimama kituo kimoja cha chakula hapo katikati ya Korogwe na Segera, baada ya kuhudumiwa kama kawaida huwa napenda kudai risiti kwasababu mimi ni mdau mzuri wa kulipa kodi. Nafurahia kuona pia wenzangu wanalipa kodi zao kwa maendeleo ya nchi.

Kilichonishangaza ni kuwa mtoa risiti alitafutwa zaidi ya dakika kumi kana kwamba nihairishe kudai risiti ili basi lisiniache, kwa bahati nzuri nilikuwa na private kwahiyo nilimsubiri hadi alipoamua kutoka alipojificha, na kwa muda wote niliokuwa nimesimama hapo watu walikuwa wakihudumiwa na kuondoka.

Sasa kwa mstakabali huu najiuliza, zile nguvu kazi zilizowekwa kwenye maduka na masoko kwanini zisisambae kwenye barabara hizi watu walipe kodi? Kwasababu ukweli ni kwamba, nchi inapoteza bilions of money monthly kwa uzembe huu kwakuwa sio kila msafiri ana uelewa wa kudai risiti.

Mwisho nitoe wito kwa wafanyabiashara, tutoe risiti hata kama tunaibiwa na wanasiasa, sisi tutimize wajibu wetu ili utakapofika muda wa kuwawajibisha tuwawajibishe kwa usahihi.
 
Sio siri kwa ujinga, upumbavu na ufisadi unaoendelea serikalini, mimi binafsi ninakwepa kodi Kila ninapopata nafasi hiyo na natamani raia wote waache kulipa kodi kama mimi serikali ikale ilipopeleka mboga.

Na natabiri huu uzi wako utashambuliwa na watu kama mimi. Sioni sababu ya kulipa kodi wakati pesa zinaishia kwenye kulipana Per Diem zisizo na kichwa wala miguu. Juzi dreamliner lilijaza nyomi la wahuni wameandamana na raisi kwenda India kutumbua kodi zetu bado unanishauri nilipe kodi?,

Kama sio mojawapo wa wanufaika wa hizi kodi unazopambania hapa basi una asili ya unoko. Ndo wale madingi hamtakagi mtoto aangalie TV, asijifunze kuendesha gari au asiende kusoma nje ya nchi kisa atakuwa mhuni. Nasisitiza mtanzania popote ulipo ukiweza kukwepa kodi fanya hivyo kwa manufaa ya familia yako na tumbo lako kama ilivyo kwa waliopo serikalini. Twende sawa tu.
 
Msile njiani

Siku zote vyakula vya njiani huuzwa ghali

Tokea enzi hizo tunakula comfort Iringa hapo bei ilikuwa ghali

Mkisafiri kuleni karanga biskuti korosho shushieni na maji

Ova
 
Inasikitisha lakini wakwepa kodi wengi,wana hoja zao,mfano ufisadi mkubwa unaofanyika kwenye miradi ya serikali,halafu wahusika baadhi hawawajibishwi ipasavyo,unadhani wananchi wanafurahi?

Mbali na hiyo,mwananchi analipa kodi,halafu hizo kodi zinaenda kuwalipa wafanyakazi wa vyombo vya ulinzi na usalama kama mishahara na posho,watimize wajibu wao kwa raia,halafu unashangaa kusikia askari ambaye ni mnufaika wa kodi ya mwananchi,anampiga na kimuonea raia,unadhani raia huyo atakua na morali ya kulipa kodi kwa hiyari?

Ukiachana na hayo yote,ajira mfano za TRA zimetoka,halafu tangazo linataka wanaojitolea humo maofisini(TRA),wapewe kipaumbele,unadhani baba au mama wa kijana msaka ajira tajwa,atakua na morali ya kulipa kodi,ilhali anajua kuna utaratibu wa hovyo wa baadhi ya taasisi katika utoaji wa ajira,tena ambazo kodi za wananchi,ndiyo zitatumika kuwalipa mishahara na posho nene watakaopangiwa,thubutu....
Anyway,tuendelee kulipa kodi.
 
Nafikiri kwa msafiri yoyote anayesafiri kwa kutumia either mabasi ya abiria au usafiri binafsi atakubaliana na mimi kuwa vyakula katika hoteli za njiani (stop overs) vinauzwa at a very premium prices.

Sasa hoja yangu sio bei ya kuuzwa kwa vyakula hivyo, hoja yangu kubwa ni je, Serikali inapata inachostahili kupata katika bei hizo ambazo raia wake tunaziingia?

Jana nilikuwa natoka Arusha naenda Dar es Salaam nikasimama kituo kimoja cha chakula hapo katikati ya Korogwe na Segera, baada ya kuhudumiwa kama kawaida huwa napenda kudai risiti kwasababu mimi ni mdau mzuri wa kulipa kodi. Nafurahia kuona pia wenzangu wanalipa kodi zao kwa maendeleo ya nchi.

Kilichonishangaza ni kuwa mtoa risiti alitafutwa zaidi ya dakika kumi kana kwamba nihairishe kudai risiti ili basi lisiniache, kwa bahati nzuri nilikuwa na private kwahiyo nilimsubiri hadi alipoamua kutoka alipojificha, na kwa muda wote niliokuwa nimesimama hapo watu walikuwa wakihudumiwa na kuondoka.

Sasa kwa mstakabali huu najiuliza, zile nguvu kazi zilizowekwa kwenye maduka na masoko kwanini zisisambae kwenye barabara hizi watu walipe kodi? Kwasababu ukweli ni kwamba, nchi inapoteza bilions of money monthly kwa uzembe huu kwakuwa sio kila msafiri ana uelewa wa kudai risiti.

Mwisho nitoe wito kwa wafanyabiashara, tutoe risiti hata kama tunaibiwa na wanasiasa, sisi tutimize wajibu wetu ili utakapofika muda wa kuwawajibisha tuwawajibishe kwa usahihi.
Wakifanya unachotaka, hutaweza kumudu hiko chakula, trust me
 
Nafikiri kwa msafiri yoyote anayesafiri kwa kutumia either mabasi ya abiria au usafiri binafsi atakubaliana na mimi kuwa vyakula katika hoteli za njiani (stop overs) vinauzwa at a very premium prices.

Sasa hoja yangu sio bei ya kuuzwa kwa vyakula hivyo, hoja yangu kubwa ni je, Serikali inapata inachostahili kupata katika bei hizo ambazo raia wake tunaziingia?

Jana nilikuwa natoka Arusha naenda Dar es Salaam nikasimama kituo kimoja cha chakula hapo katikati ya Korogwe na Segera, baada ya kuhudumiwa kama kawaida huwa napenda kudai risiti kwasababu mimi ni mdau mzuri wa kulipa kodi. Nafurahia kuona pia wenzangu wanalipa kodi zao kwa maendeleo ya nchi.

Kilichonishangaza ni kuwa mtoa risiti alitafutwa zaidi ya dakika kumi kana kwamba nihairishe kudai risiti ili basi lisiniache, kwa bahati nzuri nilikuwa na private kwahiyo nilimsubiri hadi alipoamua kutoka alipojificha, na kwa muda wote niliokuwa nimesimama hapo watu walikuwa wakihudumiwa na kuondoka.

Sasa kwa mstakabali huu najiuliza, zile nguvu kazi zilizowekwa kwenye maduka na masoko kwanini zisisambae kwenye barabara hizi watu walipe kodi? Kwasababu ukweli ni kwamba, nchi inapoteza bilions of money monthly kwa uzembe huu kwakuwa sio kila msafiri ana uelewa wa kudai risiti.

Mwisho nitoe wito kwa wafanyabiashara, tutoe risiti hata kama tunaibiwa na wanasiasa, sisi tutimize wajibu wetu ili utakapofika muda wa kuwawajibisha tuwawajibishe kwa usahihi.
Tunapenda kukushukuru kwa mrejesho huu na kuonyesha ni jinsi gani umekuwa mzalendo katika kuhakikisha kodi inakusanywa na serikali inapata Mapato yake kwa maendeleo ya nchi yetu.Tumechukua huu ushauri na kuhakikisha tunaufanyia kazi mapema. Mwisho tutatoa rai kwa wananchi kuomba risiti kwa Maendeleo ya Nchi yetu na kama kutakuwa na changamoto ya aina yoyote basi mawasiliano yetu ya bure kwa kupiga 0800780078,0800750075,0800110016 au whatsApp 0744 233 333.
 
Inasikitisha lakini wakwepa kodi wengi,wana hoja zao,mfano ufisadi mkubwa unaofanyika kwenye miradi ya serikali,halafu wahusika baadhi hawawajibishwi ipasavyo,unadhani wananchi wanafurahi?
Mbali na hiyo,mwananchi analipa kodi,halafu hizo kodi zinaenda kuwalipa wafanyakazi wa vyombo vya ulinzi na usalama kama mishahara na posho,watimize wajibu wao kwa raia,halafu unashangaa kusikia askari ambaye ni mnufaika wa kodi ya mwananchi,anampiga na kimuonea raia,unadhani raia huyo atakua na morali ya kulipa kodi kwa hiyari?
Ukiachana na hayo yote,ajira mfano za TRA zimetoka,halafu tangazo linataka wanaojitolea humo maofisini(TRA),wapewe kipaumbele,unadhani baba au mama wa kijana msaka ajira tajwa,atakua na morali ya kulipa kodi,ilhali anajua kuna utaratibu wa hovyo wa baadhi ya taasisi katika utoaji wa ajira,tena ambazo kodi za wananchi,ndiyo zitatumika kuwalipa mishahara na posho nene watakaopangiwa,thubutu....
Anyway,tuendelee kulipa kodi.
Kupona ni mchakato wa muda mrefu, kama ambavyo uharibifu umekuwa ni mchakato wa muda mrefu, tukiendelea kususia kila kitu hatutapona kama nchi. My point of view.
 
Magu pekeyake ndio alikuwa anaweza hiyo michezo.

Kauli yake ilikuwa madhubuti
The best practices ni kuwa na mfumo bora sio mtu bora.
Magu alifanya mengi ila alisahau kuwa mtu kama mtu hufariki na mipango yake kupotea . angeweka mfumo bora mengi yangeendelezwa
 
Tunapenda kukushukuru kwa mrejesho huu na kuonyesha ni jinsi gani umekuwa mzalendo katika kuhakikisha kodi inakusanywa na serikali inapata Mapato yake kwa maendeleo ya nchi yetu.Tumechukua huu ushauri na kuhakikisha tunaufanyia kazi mapema. Mwisho tutatoa rai kwa wananchi kuomba risiti kwa Maendeleo ya Nchi yetu na kama kutakuwa na changamoto ya aina yoyote basi mawasiliano yetu ya bure kwa kupiga 0800780078,0800750075,0800110016 au whatsApp 0744 233 333.
Malalamiko hayo muyachukue pia, mchukue vijana wanaojitolea wasiishie kutumwa vitumbua na kukoroga chai tu, au kusumbua madukani na masokoni wanajifunza kupokea rushwa waajirini. #Kodikwamaendeleo
 
Una hoja..

Kifupi mie si mpenzi saana wankula vyakula vyao, nitagonga yoghurt,nitagonga korosho au karanga. nitagonga apple, nitagonga matunda matunda hasa ndizi. Kati ya hivyo chochote fresh tu
Bado walipe kodi katika hayo pia
 
Nafikiri kwa msafiri yoyote anayesafiri kwa kutumia either mabasi ya abiria au usafiri binafsi atakubaliana na mimi kuwa vyakula katika hoteli za njiani (stop overs) vinauzwa at a very premium prices.

Sasa hoja yangu sio bei ya kuuzwa kwa vyakula hivyo, hoja yangu kubwa ni je, Serikali inapata inachostahili kupata katika bei hizo ambazo raia wake tunaziingia?

Jana nilikuwa natoka Arusha naenda Dar es Salaam nikasimama kituo kimoja cha chakula hapo katikati ya Korogwe na Segera, baada ya kuhudumiwa kama kawaida huwa napenda kudai risiti kwasababu mimi ni mdau mzuri wa kulipa kodi. Nafurahia kuona pia wenzangu wanalipa kodi zao kwa maendeleo ya nchi.

Kilichonishangaza ni kuwa mtoa risiti alitafutwa zaidi ya dakika kumi kana kwamba nihairishe kudai risiti ili basi lisiniache, kwa bahati nzuri nilikuwa na private kwahiyo nilimsubiri hadi alipoamua kutoka alipojificha, na kwa muda wote niliokuwa nimesimama hapo watu walikuwa wakihudumiwa na kuondoka.

Sasa kwa mstakabali huu najiuliza, zile nguvu kazi zilizowekwa kwenye maduka na masoko kwanini zisisambae kwenye barabara hizi watu walipe kodi? Kwasababu ukweli ni kwamba, nchi inapoteza bilions of money monthly kwa uzembe huu kwakuwa sio kila msafiri ana uelewa wa kudai risiti.

Mwisho nitoe wito kwa wafanyabiashara, tutoe risiti hata kama tunaibiwa na wanasiasa, sisi tutimize wajibu wetu ili utakapofika muda wa kuwawajibisha tuwawajibishe kwa usahihi.
Tatizo sana bei juu sana kisoda kidogo 1500
 
Tunapenda kukushukuru kwa mrejesho huu na kuonyesha ni jinsi gani umekuwa mzalendo katika kuhakikisha kodi inakusanywa na serikali inapata Mapato yake kwa maendeleo ya nchi yetu.Tumechukua huu ushauri na kuhakikisha tunaufanyia kazi mapema. Mwisho tutatoa rai kwa wananchi kuomba risiti kwa Maendeleo ya Nchi yetu na kama kutakuwa na changamoto ya aina yoyote basi mawasiliano yetu ya bure kwa kupiga 0800780078,0800750075,0800110016 au whatsApp 0744 233 333.
Punguzeni kula rushwa na kuwakadiria wafanyabiashara kodi za kuwakomoa.
 
Back
Top Bottom