TRA: Wauzaji/Wananunuzi wasiotoa au kuwa na risiti watatozwa Faini ya asilimia 20% ya thamani ya Mzigo

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,048
49,731
Naunga mkono haya mabadiliko ya Sheria ila nasema Bado Kuna haja ya kuwepo na kikosi kazi Cha TRA.

Kwa nini jambo la Kodi linaonekana ni hiari hapa Tanzania? Mathalani sijadai Risiti Kwa makubaliano na muuzaji akanipunguzia TRA watanikamatia wapi ikiwa vikosi kazi vimefutwa?

Serikali acheni siasa kwenye mambo ya msingi,hakuna anaependa kulipa Kodi eti Kwa hiari ili iwaje?

Tumefika mahala Kwa Sasa ukionekana unadai Risiti dukani Watu au muuzaji anakushangaa,unauliza Risiti ya nini? Nani akukmate Sasa kama huu ndio utaratibu wa Kuendesha Nchi basi tunaelekea kubaya.

Mwisho kama imeshindikana kuwafanya watu watoe na kudai Risiti basi Kodi zitozwe na mzalishaji Ili kusiwepo na kudai Risiti huku Kwa mnunuzi wa mwisho.

===
WAUZAJI WASIOTOA RISITI KUTOZWA 20% YA THAMANI YA MZIGO

Mamlaka ya mapato nchini TRA imewataka wananchi kuendelea na desturi ya kutoa na kudai risiti licha ya sheria kupunguza adhabu ya faini kwani serikali ina uwezo wa kubadilisha pia.

Akizungumza baada ya kukutana na washauri wa kodi, Chamaz Siriwa ambaye ni afisa usimamizi wa kodi msaidizi TRA amesema mabadiliko ya sheria imetoa nafuu kwa muuzaji na mnunuzi ambaye hatatoa na kudai risiti.

Amesema kutokana na kubadilishwa kwa sheria 15 za kodi na kuna maeneo ambayo mambo ni mapya hivyo washauri hao wanapaswa kufahamu ili wakaelimishe wafanyabiashara.

Aidha kwa kwa upande wa adhabu kwa wale ambao Hawatoi risiti Sasa sheria inaelekeza atozwe asilimia 20 ya thamani ya mzigo au Milioni 1.5 na kwa asiyedai risiti atozwe asilimia 20 ya kodi iliyokwepwa
 
Ni utaratibu wa kipumbavu sn, kodi ilipwe kwa lazima ili nchi ipate maendeleo badala ya watu binafsi kujinufaisha pekee
Naunga mkono hoja, Duniani kote Kodi ni lazima huu upuuzi wa kubembelesana Kwa mara ya kwanza nauona Tanzania.

Ndio sababu Watumishi wananyanyaswa sana Nchi hii harafu wafanyabiashara wao wanakula Neema.

I bet hapa Kuna mazingira ya kunufaisha vigogo
 
Ni jambo lakini kuna maduka kupata risiti inachukua nusu saa kwa mashine kuweza kutoa risiti. Kwa mtindo huu hakuna mnunuzi atakayekubali kupoteza huo muda akisubiri karatasi tu hali mzigo alishapewa.

Risit za efd zinafutika mapema sana kitu ambacho kinafanya tushindwe hata kuitumia kama ushahidi kuwa bidhaa hiyo tulinunua wenyewe pale mtu anapotuhumiwa kuiba kitu cha mtu mfano solar panel tu.

Hayo yafanyiwe kazi vinginevyo watu wengi wataendelea kuchukua zile za mkono au kutokuchukua kabisa na kuifanya sirikali kupoteza mapato.

Sirikali ipeleke huduma muhimu kwa watu kama kodi ni kwa maendeleo ya nchi kweli vinginevyo hamna haja kudai wala kutoa risiti kama tu maji,umeme, barabara, vituo vya afya n hawapelekewi walipa kodi yaani wananchi
 
Kwamba wewe unateseka walipopunguza adhabu ya kimangungo.

Kwanini na wewe usifanye biashara uwaite dukani kwako waone unavyochakarika kutoa receipt..
Biashara ninayo,sijakataa kupunguza Faini na nimeunga mkono ila kufanya swala la kutoa Risiti kuwa hiari hapana.

Umefuta kikosi kazi na Risiti sijatoa utanikamataje Sasa?
 
Naunga mkono haya mabadiliko ya Sheria ila nasema Bado Kuna haja ya kuwepo na kikosi kazi Cha TRA.

Kwa nini jambo la Kodi linaonekana ni hiari hapa Tanzania? Mathalani sijadai Risiti Kwa makubaliano na muuzaji akanipunguzia TRA watanikamatia wapi ikiwa vikosi kazi vimefutwa?

Serikali acheni siasa kwenye mambo ya msingi,hakuna anaependa kulipa Kodi eti Kwa hiari ili iwaje?

Tumefika mahala Kwa Sasa ukionekana unadai Risiti dukani Watu au muuzaji anakushangaa,unauliza Risiti ya nini? Nani akukmate Sasa kama huu ndio utaratibu wa Kuendesha Nchi basi tunaelekea kubaya.

Mwisho kama imeshindikana kuwafanya watu watoe na kudai Risiti basi Kodi zitozwe na mzalishaji Ili kusiwepo na kudai Risiti huku Kwa mnunuzi wa mwisho.

Shida sio kulipa kodi, Shida ni pale wajanja wanapoenda kujishtaki wenyewe ICSD halafu wanaipeleka ndege sehemu wanayoitaka na kuikamata hadi tulipe fidia kwa kesi ya kujitengenezea halafu wanagawana pesa, inauma sana
 
Ni jambo lakini kuna maduka kupata risiti inachukua nusu saa kwa mashine kuweza kutoa risiti. Kwa mtindo huu hakuna mnunuzi atakayekubali kupoteza huo muda akisubiri karatasi tu hali mzigo alishapewa.

Risit za efd zinafutika mapema sana kitu ambacho kinafanya tushindwe hata kuitumia kama ushahidi kuwa bidhaa hiyo tulinunua wenyewe pale mtu anapotuhumiwa kuiba kitu cha mtu mfano solar panel tu.

Hayo yafanyiwe kazi vinginevyo watu wengi wataendelea kuchukua zile za mkono au kutokuchukua kabisa na kuifanya sirikali kupoteza mapato.

Sirikali ipeleke huduma muhimu kwa watu kama kodi ni kwa maendeleo ya nchi kweli vinginevyo hamna haja kudai wala kutoa risiti kama tu maji,umeme, barabara, vituo vya afya n hawapelekewi walipa kodi yaani wananchi
Mashine ziboreshwe maisha yaendelee watu walipe kodi na kudia risiti, pia kodi zitumike vizuri na siyo hizi anasa za viongozi
 
Back
Top Bottom