Kusema kuwa CCM imejitakasa sasa ni sawa na kukiri kuwa tatizo la CCM alikuwa Makamba, which is not. Makamba aliingia katika mtandao uliokuwepo kabla yake tena kama wapo walionufaika na huo mtandao makamba si mmoja wao. Kwa hiyo mabadiriko ya kweli bado hayajaonekana labda tusubiri halmashauri kuu ya taifa kama itacheua lolote, so far, gamba liko pale pale.
Kurekebisha muundo na kuifanya sekretarieti kuwa ya watu wasio na majukumu mengine, ni jambo zuri. Jambo baya ni kuwa sekretarieti hii haina meno ya kung'ata. Hii sekretarieti ilitakiwa iwe ndo miwani inayoangalia mambo yanavyoenda serikalini na kuwang'oa wale wote wanaokwenda kinyume na maadili ya chama. Sekretarieti ikiwa na meno hayo halafu ikawa nje ya serikali tunaweza kuamini kuwa itaisadia serikali kuona kile ambacho wananchi wanakiona ila serikali haikioni. Kwa majina yaliyokwisha tajwa kuwa ndo wahusika wa hiyo sekretarieti mpya, hatuioni sekretarieti ikimsaidia rais kuisafisha serikali kwa kuwaondoa wale ambao hawafai.
Kumbuka CCM ilipotea mwelekeo pale ilipoamua kuwa ndani ya serikali na serikali ndani yake. Mambo yalikuwa yakienda kutegemea usafi wa watu fulani tu lakini si kwa kufuata "principles". Sasa wale watu walipoondoka, matatizo ya kukosa principles yakaanza kuwa wazi kuwa sasa chama hakitafika mbali. Sasa hivi kiongozi haondoki madarakani kwa makosa ya kiutendaji au ukosefu wa maadili. Kiongozi anaondoka kwa kuwa walioingia si mtandao wake, hilo ndo tatizo. Ndo maana ufisadi umekuwa ndo "modus operandi" na chama kikishuhudia na kupata kigugumizi kifanye nini.
Sasa kazi kubwa iliyopo mbele ya CCM ni kuipora ajenda ya kupambana na ufisadi na kuifanya ya kwake. Mtanziko au dilemma iliyopo ni je CCM hii inaweza kuifanya kazi hiyo? Wananchi wanauona ufisadi serikalini, kila mahali. CCM iliamua kuwa kupambana na ufisadi ni ajenda ya wapinzani wao haiwahusu kwa sababu hawauoni ufisadi! Hapo ndo tunaposema CCM lazima ife. Kwa sababu haiwezi kupambana na ufisadi bila kuukata uti wa mgongo wa CCM yenyewe kwani iko compromised centre, left and right!!
Hatuna sababu yoyote ya kushangilia kufukuzwa kazi kwa Makamba tu. Mhimili wa maovu (axis of evil) ndani ya serikali bado unapeta na ufisadi utaendelea kuisumbua serikali hii nyuma na mbele! Tusubiri tuone.
Kurekebisha muundo na kuifanya sekretarieti kuwa ya watu wasio na majukumu mengine, ni jambo zuri. Jambo baya ni kuwa sekretarieti hii haina meno ya kung'ata. Hii sekretarieti ilitakiwa iwe ndo miwani inayoangalia mambo yanavyoenda serikalini na kuwang'oa wale wote wanaokwenda kinyume na maadili ya chama. Sekretarieti ikiwa na meno hayo halafu ikawa nje ya serikali tunaweza kuamini kuwa itaisadia serikali kuona kile ambacho wananchi wanakiona ila serikali haikioni. Kwa majina yaliyokwisha tajwa kuwa ndo wahusika wa hiyo sekretarieti mpya, hatuioni sekretarieti ikimsaidia rais kuisafisha serikali kwa kuwaondoa wale ambao hawafai.
Kumbuka CCM ilipotea mwelekeo pale ilipoamua kuwa ndani ya serikali na serikali ndani yake. Mambo yalikuwa yakienda kutegemea usafi wa watu fulani tu lakini si kwa kufuata "principles". Sasa wale watu walipoondoka, matatizo ya kukosa principles yakaanza kuwa wazi kuwa sasa chama hakitafika mbali. Sasa hivi kiongozi haondoki madarakani kwa makosa ya kiutendaji au ukosefu wa maadili. Kiongozi anaondoka kwa kuwa walioingia si mtandao wake, hilo ndo tatizo. Ndo maana ufisadi umekuwa ndo "modus operandi" na chama kikishuhudia na kupata kigugumizi kifanye nini.
Sasa kazi kubwa iliyopo mbele ya CCM ni kuipora ajenda ya kupambana na ufisadi na kuifanya ya kwake. Mtanziko au dilemma iliyopo ni je CCM hii inaweza kuifanya kazi hiyo? Wananchi wanauona ufisadi serikalini, kila mahali. CCM iliamua kuwa kupambana na ufisadi ni ajenda ya wapinzani wao haiwahusu kwa sababu hawauoni ufisadi! Hapo ndo tunaposema CCM lazima ife. Kwa sababu haiwezi kupambana na ufisadi bila kuukata uti wa mgongo wa CCM yenyewe kwani iko compromised centre, left and right!!
Hatuna sababu yoyote ya kushangilia kufukuzwa kazi kwa Makamba tu. Mhimili wa maovu (axis of evil) ndani ya serikali bado unapeta na ufisadi utaendelea kuisumbua serikali hii nyuma na mbele! Tusubiri tuone.