Mambo 6 wasiyoyapenda wanaume kutoka kwa wenza wao

Ukiona mwanaume anapenda kushirikishwa kwenye umbea au anapenda kujua jua mambo ya wanawake/kike: Huyo si mwanaume kamili na anatutia aibu s#*!,,

Mshindwe kutiwa aibu na mashoga mtiwe aibu na watu wanaopiga story pyeeeeeeeee
 
Haya niliyapata kutoka kwa mshauri wa masuala ya mahusiano, ndoa na vijana Frederick Kyara. Hizi ni baadhi tu nakuwekea hapa japo kuna vitu pia wanawake hawavipendi kutoka kwa wenzi wao wanaume.

Nayo ni haya hapa, ungana nami kujadili jambo hili ambalo kwangu nimeona ni changamoto au niseme sikujua.

1. Wanaume hawapendi kuambiwa cha kufanya na wenzi wao

Mwanamke unapotaka mwanaume afanye jambo usimwambie alifanye bali fanya kama una mpa ushauri. Kwamba John hivi kwa nini tusiweke balbu hapa kwenye korido maana kuna giza kweli. Badala ya hivi wewe John huoni hapa kwenye korido kuna giza balbu imeungua mwezi sasa hujabadilisha kwa nini? Weka balbu bwana. Atafanya au asifanye kabisa kwa sababu umemwambia cha kufanya.

2. Wanaume hawapendi mwenzi mwenye makelele, mlalamishi

Yeye ni kulalamika kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. Japo wanawake nao wanasema kuna wanaume walalamishii balaaa. Na wenye gubu wanasusa kula mpaka kuongea wanawanunia wake zao mmmmh!

3. Wanaume hawapendi mwenzi mchafu

Mchafu wa mwili wake na hata nyumbani kwenye suala la kutunza nyumba wanayoishi. Uchafu hufanya mwanamke apoteze mvuto.

4. Wanaume hawapendi mwenzi mbishi

Japo na wanawake wanasema wanaume ndio wabishi zaidi. Utampa mwanaume ushauri lakini haufanyii kazi ubishi mwingi.

5. Wanaume hawapendi kuamrishwa na mwenzi wao

Mwenzi mbabe anaetoa amri na kumtawala hawataki.

6. Wanaume hawapendi kuhisiwa hisiwa na kusachiwa sachiwa

Kumpekua kwenye simu, mifuko ya suruali kwamba unamulika mwizi. Hawapendi, tena pengine hawajafanya jambo la kuwafanya wahisiwe vibaya.
Nimeyapitia vizuri sana maandishi yako, ningependa sana kuchangia, lakini hoja hizo zote hakuna msingi wowote ambapo zimejengwa kwazo, mwanasaikolojia fulani kwenye kitabu fulani na utafiti uliofanywa mwaka fulani ndiyo uliothibisha maelezo haya, Mimi mawazo haya nayaona kuwa yamejengwa ktk hisia na uzoefu wa mtu binafsi tu. Jambo hili mimi huwa sishadadii sana, nawaachia wenye ngazi hiyo waendee.
 
Kuna wengine wana tabia "baby utanioa lini, au ikifika July nitatoa tamko alafu ukipiga pozi la kutafakari way forward anakuja bay nataka tuzae"
 
Back
Top Bottom