Mambo 10 ambayo Simba SC inapaswa Kujifunza Kutoka Yanga SC

demigod

JF-Expert Member
Jan 2, 2015
8,250
15,116
Kwanza, ni muhimu kuelewa kuwa kila timu ina changamoto zake na hakuna njia moja ya kufikia mafanikio. Hata hivyo, hapa kuna mambo kumi ambayo Simba SC wanaweza kuyafanya ili kufikia kiwango na ubora wa Yanga SC hivi sasa:-

1. Kuwa na uongozi thabiti na waaminifu ambao unaweza kuendesha timu kwa ufanisi na uwazi.

Uongozi ni pamoja na wabeba maono na malengo yenye uhalisia. Mfano:- Murtaza Mangungu aliwapa ahadi kuwa kama akiingia madarakani basi atahakikisha Klabu ya simba inaifunga Yanga. Huyu sio aina bora ya kiongozi.

2. Kuwekeza katika vifaa bora vya mafunzo na ujenzi wa miundombinu ya kisasa kwa ajili ya timu.

Aina ya vifaa ambavyo Yanga wanatumia mazoezini ni mfano wa kuigwa kwa kuwa sijawahi kuviona ktk viwanja vya mazozi vya Simba. Vile vile wanapaswa kutafuta kambi nzuri ambayo inafanana na Avic Town. Kule mbweni hakuna utulivu wa kutosha maana kila wakati vigoma vya urigwai vinapita.

3. Kuajiri makocha bora na wenye uzoefu ambao wanaweza kuendesha mafunzo ya kiwango cha juu na kuendeleza vipaji vya wachezaji.

Kocha bora ni yule mwenye CV ambayo inaonyesha kuwa aliwahi kufanya jambo fulani huko nyuma. CV ya Robertinho haionyeshi kuwa kama amewahi kishinda kombe lolote lile barani afrika. Simba wanapaswa kutafuta kocha mpya ambaye aliwahi kushinda hata kombe lolote la CAF.

4. Kuimarisha mfumo wa usajili wa wachezaji kwa kufanya tathmini ya kina na kuchagua wachezaji wenye ujuzi na talanta za kipekee.

Kama kuna klabu inaongoza upigani basi, Simba ni namba moja nchini. Jamaa wameajiri Scout ambaye hapo awali alihusika kumleta SAWADOGO klabuni kwao. Inashangaza mno.

Inafaa waige kutoka Yanga, ukiona mchezaji mzuri unamfuata hadi kwa mama yake na wala sio kutuma watu. Mfano Eng Hersi alimfuata mama yake Aziz Ki.

5. Kuhakikisha kuwa wachezaji wanapata mafunzo ya kutosha kuhusu mbinu na uwezo wa kucheza kwa pamoja kama timu.

Mafunzo na mbinu yanatokana na kocha mzuri ambaye anayeweza kuongoza kwa mfano ili wachezaji waweze kuelewa vyema. Sasa mginda kwa unene ule anawezaje kumuonyesha Kibu Denia namna ya kuwa na Pace? Simba inabidi ijitafakari ktk eneo hili

6. Kutoa motisha kwa wachezaji kwa njia ya malipo mazuri, mikataba mizuri na fursa za kujitokeza katika mechi za kimataifa.

Inasemekana kuwa Mo Dewji ni tajiri bahiri kuwahi kutokea ktk historia ya soka hapa Tanzania. Jamaa anapaswa kujifunza kutoka kwa Mr Ghalib. Uwezi kushindwa kuwalipa bonus wachezaji ili hali kila siku wanabeba ndoo za sabuni na matangazo ya juisi. Kama hawezi aiache timu ili waje wengine wenye nia njema.

7. Kujenga uhusiano mzuri na mashabiki na kuhakikisha kuwa wanahisi sehemu ya timu na wanapewa huduma bora.

Mashabiki wa simba wanaipenda timu yao lkn timu haiwapendi, haiwezekani mpaka sasa hakuna shabiki wa simba mwenye kadi ya kielektroniki kama mashabiki wenzao wa Yanga. Kadi za uanachama zinajenga mahusiano baina ta Klabu na mashabiki.

Yaani sasa hivi mashabiki wa simba wanaishabikia simba kwasababu tu waliipenda wao wenyewe na hawana uwezo wa kuhamia timu nyingine kwasababu soka sio kama dini. Vinginevyo wengi wangekuwa wamehamia Namungo na Singida BS.

8. Kuwa na mkakati wa masoko ambao unaweza kufikia watazamaji wengi na kushiriki katika matukio mbalimbali ya kijamii.

Matukio mbalimbali ni kama kushiriki kutoa misaada mbalimbali kwa wale wasio jiweza. Yanga wamekuwa wakifanya hivi tangu mwaka 2021. Simba walifanya mara moja tu tena walitoa zawadi zisizo zidi elfu 50.

9. Kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya habari na kutoa taarifa za kina kuhusu timu, wachezaji na matukio mbalimbali.

Habari zao mara nyingi hawataki kuzivujisha mitandaoni, mara nyingi wanazificha kwenye APP yao. Hii inalwapa shida wachambuzi & waandishi wa habari kupata habari za michezo.

10. Kuendeleza maadili mema kama vile nidhamu, uwajibikaji, uaminifu na umoja kati ya wachezaji, viongozi na mashabiki.

Nidhamu imekuwa tatizo kubwa sana kwao. Hawajipi nafasi ya kujifunza kutoka kwa wenzao Yanga. Wanatabia yakuchukua wachezaji waliochwa na vilabu vingine kwa makosa ya kinidhamu mfano Saido Ntibanzokinza. Vile vile hawana uwezo wa kuwaadhibu wachezaji wanao vuta bangi klabuni mfano Jonas Mkude. We mchezaji anawezaje kumtongoza CEO? Basi Mkude aliweza kufanya hivyo mara kwa mara pale atokapo kuvuta Shisha.

Hayo ni machache wakuu, ila tusichukiane pale tunapo kosoa ili kufanyike mabadiliko.
 
Kwanza, ni muhimu kuelewa kuwa kila timu ina changamoto zake na hakuna njia moja ya kufikia mafanikio. Hata hivyo, hapa kuna mambo kumi ambayo Simba SC wanaweza kuyafanya ili kufikia kiwango na ubora wa Yanga SC hivi sasa:-

1. Kuwa na uongozi thabiti na waaminifu ambao unaweza kuendesha timu kwa ufanisi na uwazi.
Nitarudi Makolokolo wakitulia na kukujibu pasipo mihemuko ya ushabiki maandazi.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
1900fc73-440f-4c99-9f3c-d7b53724b4ad.jpg
 
Yaani badala ya Simba SC ajifunze kutoka kwa wenye makombe Al Ahly, Wydad, E Tunis na T Mazembe ya wakati ule halafu ajifunze kwa Yanga aliyepata mafanikio jana ilhali wenzake alipata tangu miaka 30 iliyopita. Akili Ipo Kweli Ya Kutafakari..!
Mtoto anapo jifunza. Kuttembea ni lazima afuate hatua zote za ukuaji.

Kukaa.
Kusema.
Kutambaa.
Kutembea.

Huwezi kuruka hatua.

Ni lazima.ajifunze kwanza kwa Yanga ndipo aje kujifunza kwa hao wengine.
 
Mtoto anapo jifunza. Kuttembea ni lazima afuate hatua zote za ukuaji.

Kukaa.
Kusema.
Kutambaa.
Kutembea.

Huwezi kuruka hatua.

Ni lazima.ajifunze kwanza kwa Yanga ndipo aje kujifunza kwa hao wengine.
Kwa mafanikio yapi ya Yanga ambayo Simba SC hakuyafikia.?
 
Kwanza, ni muhimu kuelewa kuwa kila timu ina changamoto zake na hakuna njia moja ya kufikia mafanikio. Hata hivyo, hapa kuna mambo kumi ambayo Simba SC wanaweza kuyafanya ili kufikia kiwango na ubora wa Yanga SC hivi sasa:-

1. Kuwa na uongozi thabiti na waaminifu ambao unaweza kuendesha timu kwa ufanisi na uwazi.

Uongozi ni pamoja na wabeba maono na malengo yenye uhalisia. Mfano:- Murtaza Mangungu aliwapa ahadi kuwa kama akiingia madarakani basi atahakikisha Klabu ya simba inaifunga Yanga. Huyu sio aina bora ya kiongozi.

2. Kuwekeza katika vifaa bora vya mafunzo na ujenzi wa miundombinu ya kisasa kwa ajili ya timu.

Aina ya vifaa ambavyo Yanga wanatumia mazoezini ni mfano wa kuigwa kwa kuwa sijawahi kuviona ktk viwanja vya mazozi vya Simba. Vile vile wanapaswa kutafuta kambi nzuri ambayo inafanana na Avic Town. Kule mbweni hakuna utulivu wa kutosha maana kila wakati vigoma vya urigwai vinapita.

3. Kuajiri makocha bora na wenye uzoefu ambao wanaweza kuendesha mafunzo ya kiwango cha juu na kuendeleza vipaji vya wachezaji.

Kocha bora ni yule mwenye CV ambayo inaonyesha kuwa aliwahi kufanya jambo fulani huko nyuma. CV ya Robertinho haionyeshi kuwa kama amewahi kishinda kombe lolote lile barani afrika. Simba wanapaswa kutafuta kocha mpya ambaye aliwahi kushinda hata kombe lolote la CAF.

4. Kuimarisha mfumo wa usajili wa wachezaji kwa kufanya tathmini ya kina na kuchagua wachezaji wenye ujuzi na talanta za kipekee.

Kama kuna klabu inaongoza upigani basi, Simba ni namba moja nchini. Jamaa wameajiri Scout ambaye hapo awali alihusika kumleta SAWADOGO klabuni kwao. Inashangaza mno.

Inafaa waige kutoka Yanga, ukiona mchezaji mzuri unamfuata hadi kwa mama yake na wala sio kutuma watu. Mfano Eng Hersi alimfuata mama yake Aziz Ki.

5. Kuhakikisha kuwa wachezaji wanapata mafunzo ya kutosha kuhusu mbinu na uwezo wa kucheza kwa pamoja kama timu.

Mafunzo na mbinu yanatokana na kocha mzuri ambaye anayeweza kuongoza kwa mfano ili wachezaji waweze kuelewa vyema. Sasa mginda kwa unene ule anawezaje kumuonyesha Kibu Denia namna ya kuwa na Pace? Simba inabidi ijitafakari ktk eneo hili

6. Kutoa motisha kwa wachezaji kwa njia ya malipo mazuri, mikataba mizuri na fursa za kujitokeza katika mechi za kimataifa.

Inasemekana kuwa Mo Dewji ni tajiri bahiri kuwahi kutokea ktk historia ya soka hapa Tanzania. Jamaa anapaswa kujifunza kutoka kwa Mr Ghalib. Uwezi kushindwa kuwalipa bonus wachezaji ili hali kila siku wanabeba ndoo za sabuni na matangazo ya juisi. Kama hawezi aiache timu ili waje wengine wenye nia njema.

7. Kujenga uhusiano mzuri na mashabiki na kuhakikisha kuwa wanahisi sehemu ya timu na wanapewa huduma bora.

Mashabiki wa simba wanaipenda timu yao lkn timu haiwapendi, haiwezekani mpaka sasa hakuna shabiki wa simba mwenye kadi ya kielektroniki kama mashabiki wenzao wa Yanga. Kadi za uanachama zinajenga mahusiano baina ta Klabu na mashabiki.

Yaani sasa hivi mashabiki wa simba wanaishabikia simba kwasababu tu waliipenda wao wenyewe na hawana uwezo wa kuhamia timu nyingine kwasababu soka sio kama dini. Vinginevyo wengi wangekuwa wamehamia Namungo na Singida BS.

8. Kuwa na mkakati wa masoko ambao unaweza kufikia watazamaji wengi na kushiriki katika matukio mbalimbali ya kijamii.

Matukio mbalimbali ni kama kushiriki kutoa misaada mbalimbali kwa wale wasio jiweza. Yanga wamekuwa wakifanya hivi tangu mwaka 2021. Simba walifanya mara moja tu tena walitoa zawadi zisizo zidi elfu 50.

9. Kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya habari na kutoa taarifa za kina kuhusu timu, wachezaji na matukio mbalimbali.

Habari zao mara nyingi hawataki kuzivujisha mitandaoni, mara nyingi wanazificha kwenye APP yao. Hii inalwapa shida wachambuzi & waandishi wa habari kupata habari za michezo.

10. Kuendeleza maadili mema kama vile nidhamu, uwajibikaji, uaminifu na umoja kati ya wachezaji, viongozi na mashabiki.

Nidhamu imekuwa tatizo kubwa sana kwao. Hawajipi nafasi ya kujifunza kutoka kwa wenzao Yanga. Wanatabia yakuchukua wachezaji waliochwa na vilabu vingine kwa makosa ya kinidhamu mfano Saido Ntibanzokinza. Vile vile hawana uwezo wa kuwaadhibu wachezaji wanao vuta bangi klabuni mfano Jonas Mkude. We mchezaji anawezaje kumtongoza CEO? Basi Mkude aliweza kufanya hivyo mara kwa mara pale atokapo kuvuta Shisha.

Hayo ni machache wakuu, ila tusichukiane pale tunapo kosoa ili kufanyike mabadiliko.
Simba haiwezi jifunza kwa underdogs
 
Unaona hizi akili sasa, ametolea mfano tu, anaweza kwenda kwa mtu wake wa karibu, umeona vile Yanga wamekuta Mtoto wa Nabi ili wafanye mazungumzo mkataba wa Baba
Wachezaji wazuri wafwate Hadi Kwa mama zao? Hata kama mama zao wamekufa kiongozi Bora aende kuongea makaburini ikiwezekana sio?
 
Hiv ni yanga ijifunze kwa simba au simba ijifunze kwa yangaaa?

Kunakitu hakiko sawa hapaaaa
 
Kwenye point ya KAMBI YENYE UTULIVU..ni hoja ya kiufundi sana..inawezekana ndiyo siri kubwa YANGA karibuni..
Kufanyia kambi nje ya nchi ni kuongeza tu pressure kwa wachezaji dhidi ya media na matarajio makubwa..
Naamini ikisukwa defence line viongozi+ kipa them ukawa na viungo shoka- skilled simba inarudi kwa kuwa tayari ina mtaji wa jina..

Natamani yule dada BARBARA angerudi, hata kama sio kwa position ya CEO..ILA alikuwa ni icon..

Simba inahitaji japo figure mpya charismatic
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom