Mama yangu adui yangu

Mama yangu adui yangu

jamaa mzizi mkavu@ sijui anakwama wapi amesahau kuwa kuna majukwaa mengi humu
watu tupo huku tunasubili, tunakuwa tunasahau sasa
ntakuwa naiacha mpaka iishe ndo nifuatilie kwa mtindo huu inatia uvuvi mzee😱hwell:!!
 
MziziMkavu umenipa kibarua kipevu cha kutembelea page hii karibuni kila siku ... hebu tupe mambo basi
 
MAMA YANGU ADUI YANGU - 14...

ILIPOISHIA;
Baada ya maumivu niliyopewa na Beka nilikubaliana na mama kuwa hakukuwa na faida ya kuishi maisha ya ndoa au kuwa mwaminifu kwa mwanaume asiyekuwa mwaminifu.
SASA ENDELEA...

Baada ya kuwaza sana huku nikiendelea kuwatazama dada zangu waliokuwa wakifurahia maisha.
Waliponiona waliniita ili nikaungane nao kupunguza mawazo.
“Njoo mdogo wangu, kunywa kidogo upunguze mawazo.”

Nilijisogeza karibu na kupewa glasi iliyokuwa na bia nusu. Niliichukua na kuipeleka mdomoni na kuinywa kama maji. Ilikuwa chungu kiasi nilifumba macho na kuipitisha kooni kwa shida. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilianza kunywa bia kwani niliamini humpunguzia mtu mawazo. Nilijikuta nikipingana na mawazo yangu ya awali kuwa pombe ni uhuni.


Dada zangu walifurahia kitendo changu cha kujaribu bia. Waliniongezea kwenye glasi kila nilipomaliza, japokuwa sikuwahi kunywa lakini haikuwa mbaya sana.


Nilijilazimisha kuinywa mpaka nikamaliza bia moja. Dada aliniongezea nyingine ambayo niliendelea kunywa bila kujua kipi kitafuata.


Nilijikuta nikihisi kizunguzungu, dada aliendelea kunilazimisha nimalize bia nyingine, kitu kilichonifanya nilewe na kulala pale nilipokuwa nimekaa.

Nilishtuka siku ya pili na kujikuta nimelala kitandani kwangu nikiwa nimejisaidia haja ndogo bila kujua huku nikisikia njaa kali. Nilinyanyuka na kwenda kuoga na kufanya usafi kisha nikaanza kutafuta supu.
***
Nilijikuta nikijiingiza katika ulevi ili kupunguza mawazo, pamoja na kufanya yote bado sikuwa tayari kuutoa mwili wangu kama asusa kwa wanaume kwa kuhofia maradhi.
Japokuwa dada zangu walinikuwadia kwa wanaume ikiwa pamoja na kuniletea fedha walizopewa, lakini sikuwa tayari kujiingiza kwenye ukahaba.

Niliamua kujiingiza kwenye ulevi kama mfariji wangu kwa kipindi kile kilichokuwa kigumu sana kwangu, kwa vile mpaka muda ule bado sikujua sababu ya kupewa talaka ambayo ilionekana kuwa na siri nzito ambayo sikuwa nikiijua.

Lakini kulikuwa na tatizo lililokuwa likinisumbua mpaka mama akanikataza kunywa pombe kwa kuwa ilikuwa ikinishinda.

Kila nilipokuwa nikinywa pombe na kuanza kulewa, niliangua kilio kumlilia mume wangu.

Kwa wenzangu ilikuwa ni karaha na kuonekana kama nilikuwa nikiwapigia makelele wakati awali tulilizungumza na kukubaliana. Nilijitahidi kumsahau mume wangu mtu ambaye nilimzoea na kuamini kifo ndicho kingetutenganisha, lakini talaka ilikuwa pigo na kovu kubwa maishani mwangu.

Kila nilipolia na kukemewa niliwaahidi dada zangu kuwa sitalia tena, pia niliahidi nitaachana na mawazo ya mtalaka wangu aliyeniacha bila sababu za kueleweka. Lakini kila nilipokunywa pombe na kulewa yote yalijirudia na kuanza kulia huku nikitawaliwa na mawazo mabaya ya kunitaka ninywe sumu ili niepukane na aibu ya kuachwa.


Wakati kwangu likiwa pigo mujarabu moyoni mwangu, dada zangu waliotangulia kuachika hawakuteteleka waliendelea na maisha kwa kutumia miili yao kama mitaji ya kuwaweka mjini bila kuhofia hali ya hatari.


Niliamini njia ya kumuondoa mume wangu akilini ni kuwa bize kuliko kuendelea kukaa nyumbani na kujilazimisha kunywa pombe ambayo kila nilipolewa nilimlilia mtalaka wangu.

Niliamini ubize pekee ndiyo ungeweza kunisaidia kuchosha mwili na nikirudi nyumbani mchovu, nitafikia kuoga kula na kulala kuliko kushinda nyumbani kusubiri wanaume.

Mwanaume mmoja wa dada mkubwa alikuwa anafanya kazi serikalini, niliamini anaweza kunisaidia kupata kazi. Nilimweleza dada amweleze anitafutie kazi popote.

Baada ya kumweleza dada amwambie alinihakikishia kunipa jibu ndani ya wiki.
****

Baada ya siku nne dada aliniletea taarifa kuwa kazi imepatikana kwenye super market iliyopo katikati ya jiji. Kwa kweli nilifurahi sana kupata kazi nikiamini kuwa bize kutanifanya niwe mbali na vishawishi vibaya.

Nilielezwa Jumatatu nilitakiwa nianze kazi, bwana wa dada alisema atanipitia asubuhi ya siku hiyo, hivyo nilitakiwa niamke mapema kujiandaa kabla hajafika.

Kwa vile taarifa nilizipata siku tatu kabla, nilijiandaa kwa kutafuta nguo itakayoendana na maeneo husika, japokuwa siku zote sikupenda kuvaa nguo fupi kwani zilininyima uhuru na kujiona nakaa uchi lakini siku hiyo sikuwa na budi kuivaa.

Jumatatu niliamka alfajiri na kujiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini. Saa moja kasoro bwana wa dada Sauda alifika na gari lake na kunichukua kunipeleka kwenye hiyo super market.

Tulikwenda mpaka katikati ya jiji. Tulipofika alipiga simu na nilimsikia akizungumza.

“Haloo..eeh..nimefika.... haya nakuja.”


Usikose kusoma Alkhamisi ijayo......
 
Dah hii hadithi kiboko inakufanya mtu unabaki na kiu isiyotulizwa kwa chochote kiukweli inanifanya nasahau shida zangu.
 
Wee kibabu siku hizi unamatatizo,hebu malizia hii hadith..usilete story za afande na mtoto wa singida.
 
MAMA YANGU ADUI YANGU - 15-

ILIPOISHIA;
Kwa vile taarifa niliipata siku tatu kabla, nilijiandaa kwa kutafuta nguo itakayoendana na maeneo yale, japokuwa siku zote sikupenda kuvaa nguo fupi kwani zilininyima uhuru na kujiona nakuwa mtupu.

Siku ya Jumatatu niliamka alfajiri nikajiandaa na kuelekea kwenye kazi hiyo. Saa moja kasoro bwana wa dada Sauda alifika na gari lake na kunichukua kunipeleka kwenye hiyo super market.


Tulikwenda mpaka kwenye super market iliyokuwa katikati ya jiji. Tulipofika alipiga simu na kumsikia akizungumza.


“Haloo...eeh...nimefika...haya nakuja.”

Baada ya kukata simu aliniambia.
“Twende.”
SASA ENDELEA...

Sikumjibu nilimfuata, tuliingia naye ndani na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi moja iliyokuwa ya vioo vitupu na kuingia ndani.

Ndani tulimkuta kaka mmoja mtanashati, baada ya kuingia nilikaribishwa kwenye kiti. Nilikaa na kutulia huku bwana wa dada akisalimiana na yule kaka kisha alisema:

“Sasa bibie mi acha niwahi, kila kitu atamalizia huyu mwenyeji wako.”
“Hakuna tatizo.”

Bwana wa dada alitoka na kuniacha na yule kaka ambaye aliniomba radhi na kutoka. Baada ya muda alirudi na fomu ambazo zilikuwa za kuajiriwa. Baada ya kukaa aliniuliza maswali mawili matatu kisha alinipeleka sehemu, nikapigwa picha.

Baada ya zoezi lile nilirudi ofisini kwa yule kaka aliyekuwa meneja wa duka lile kubwa sana. Alinyanyua simu na kuagiza chai, baada ya muda ililetwa na kunywa kisha alimwita dada mmoja.
Alipofika alimweleza:
“Suzy huyu ni mfanyakazi mpya, naomba umpe ushirikiano wa hali ya juu.”
“Hakuna tatizo bosi.”
“Kampatie sare na aanze kazi.”
“Hakuna tatizo, atakuwa sehemu gani bosi?”
“Mweke kwa keshia.”
“Hakuna tatizo, kitambulisho?”
“Muone Sam nina imani kitakuwa tayari.”
“Haya shem, nina imani Suzy atakusaidia, kazi njema.”
“Asante.”

Nilitoka na Suzy mpaka kwenye chumba kimoja kilichokuwa na sare na kunichagulia inayonitosha kisha tuliongozana mpaka kwenye chumba kingine na kukuta kitambulisho changu kipo tayari.


Nilipewa na kukivaa kisha nilipelekwa sehemu na kuelekezwa kama mtu akishalipia bidhaa aliyonunua namuwekea kwenye mfuko na kuwakaribisha tena.


Haikuwa kazi kubwa sana lakini nilichoka sana kwa vile sikuwa nimezoea kusimama muda mrefu. Jioni bwana wa dada alinipitia. Kabla ya kuondoka da Suzy niliyekuwa nimemzoea kwa haraka, alinieleza muda wa kuingia kazini na umuhimu wa kuwahi.


Nilimshukuru na kumuahidi kuwahi siku ya pili. Niliingia ndani ya gari la shemeji na kurudishwa nyumbani. Njiani shemeji aliniuliza mambo mengi kuhusiana na kazi.


Sikusita kumshukuru kwa msaada wake ambao ulikuwa muhimu kuliko kitu chochote kwa wakati ule.

Tokea siku ile nilianza kazi ya kuuza kwenye super makert na jioni shemeji alinipitia kama kawaida. Siku zote nilirudi nimechoka baada ya kuoga na kula muda mwingi niliutumia kitandani kwangu kupumzika.

Taratibu nilianza kumsahau mtalaka wangu Beka na kuamini kuna maisha mengine baada yake kwa kujua kila linalomtokea mwanadamu lina makusudio yake.


Kazi niliizoea na kuwa maarufu kutokana na ucheshi wangu. Lakini nilikuwa na wakati mgumu kazini kutokana na wanaume wengi wakware kunitaka kimapenzi.


Pamoja na ahadi nyingi nilizopewa kama nitakubali kujitoa kwao kimapenzi, sikuwa tayari kujiingiza katika dunia iliyoniumiza na kufikia hatua ya kuwachukia wanaume, japokuwa sikutakiwa kumhukumu mtu kwa kosa la mwingine.


Moyoni nilipanga baada ya miaka miwili ndipo niufungue moyo wangu. Najua unaweza kushangaa uamuzi wangu lakini kila aliyekumbwa na mkasa wa mapenzi hawezi kunishangaa kwa vile mapenzi yanaumiza sana hasa uachwe na mtu unayempenda tena bila kujua kosa lako.


Siku zilikatika huku nikizidi kuifurahia kazi yangu na maisha yangu mapya ya kuishi kama mdudu wa sikio bila kuwa na mshirika. Mwanzo niliamini maisha yale yangekuwa magumu ya kuishi bila mwanaume, lakini kila kitu ukiamua unaweza nami niliweza kabisa.

Nakumbuka siku moja wakati natoka kazini nikiwa ndani ya gari la shemeji bwana wa dada. Baada ya kutoka kazini tulikwenda mwendo wa dakika tano, alinigeukia na kuniuliza:
“Mwaija una mpango gani?”
“Kuhusu nini shemeji?”
“Si nilisikia umeachana na mumeo?”
“Ndiyo.”
“Sasa una mpango gani baada ya kuachana naye?”
“Mmh! Bado sina mpango wowote nimeamua kupumzika kwanza.”
“Mwaija wewe bado msichana mdogo kwa nini ujifuje?”
“Sijifuji bali nimeamua kupumzika, kilichonikuta Mungu anajua.”
“Mwaija siyo Mungu anajua, mwanaume uliyekuwa naye hakuwa sahihi kwako.”
“Ukisema hivyo sikubaliani na wewe, Beka namjua vizuri kuliko mtu yeyote, kuna kitu tu ambacho kimesababisha aniache.”
“Kitu gani?”
“Wee shemu, tuyaache tu yalishapita hayo,” kwa kweli sikupenda kuzikumbuka habari za mtalaka wangu.
“Kama anatokea leo na kutaka kukurudia utakubali?”
“Naweza kukubali kama atanieleza sababu ya kuniacha na mimi kuikubali.”
“Sasa Mwaija tuachane na hayo kuna kitu nataka kukuambia japokuwa ninacho muda mrefu, lakini naamini leo ni siku muafaka.”
“Kitu gani hicho shemeji yangu?”
“Kuhusu wewe.”
“Mimi! Nimefanya nini?”
“Siyo kwamba umefanya kitu ila kuna jambo nimejifunza kwako kwa muda mrefu.”
“Kipi?”
“Mwaija unatabia tofauti na dada zako.”
“Kivipi?”
“Unajiheshimu pia unajifahamu.”
“Nashukuru kwa kulifahamu hilo.”
“Baada ya kuligundua hilo nilikuwa na ombi moja ambalo nina imani litakuwa na faida kubwa kwako.”
“Ombi gani?”
“Nataka nitabadili maisha yako uweze kumiliki nyumba na gari.”
“Kivipi?”
“Nafikiri unajue mimi na dada yako tukoje?”
“Ndiyo najua.”
“Basi nimeishamfumania na wanaume zaidi ya watatu.”
Shemeji alitulia kuzungumza akasimamisha gari kuwaruhusu watu waliokuwa wakivuka barabara eneo la Chang’ombe Maduka Mawili wavuke. Baada ya watu kuvuka alibadili gea na kukanyaga mafuta kisha alinigeukia na kusema:
“Unajua nilikuwa nina mipango mikubwa na dada yako.”
“Mipango gani?”
“Nimjengee nyumba na kumnunulia gari.”
“Tatizo nini?”
“Hataki nimuoe zaidi ya kupenda maisha anayoishi, wewe ni mdogo lakini una akili sana.”
“Shem, si nasikia umeoa?”
“Ndiyo, lakini angekuwa nyumba yangu ndogo.”
“Mmhu, na mimi unataka kuyabadilisha maisha yangu kivipi?”


Nini kitaendelea? Tukutane tena jumamosi....
 
hehehe!kwa wanaokwazika na simulizi hii inapatikana kwa shigongo globalpubliashers au gazeti la risasi.ila siku tajwa ndio inaendelea!
 
heeee hii hadithi nzuri sana kama natizama series hemu malizia leo please hii ndo jumamosi mwaya
 
Back
Top Bottom