Mama yangu adui yangu

Mama yangu adui yangu

Cdhani kama unamtendea haki mwandish wa stori hii,maana unachofanya ni kuihamisha kutoka gazeti la risasi la shigongo
 
Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili na jamaa na mayatima na masikini na jirani wa karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wanao jifakhiri, [4:36]
 
MAMA YANGU ADUI YANGU - 7-



ILIPOISHIA;
SIKU zilizidi kukatika bila kupata taarifa za mume wangu yupo wapi.
Mama alinieleza niendelee na maisha yangu ikibidi hata kutafuta mwanaume kwa wakati ule wa kuniliwaza wakati namsubiri mume wangu.
SASA ENDELEA...
Japokuwa kulikuwa na wanaume wengi walionimezea mate lakini sikuwa tayari kujidhalilisha. Niliiheshimu ndoa yangu pia mwenyewe nilijiheshimu, sikutaka kuwa na sifa mbaya kama dada zangu. Siku nazo zilikatika bila kupata taarifa za mume wangu.
Sikuchoka kwenda kuuliza kwao na kijiweni kwake labda kulikuwa kuna mtu ana taarifa zake. Kila nilipouliza majibu yalikuwa yaleyale, hawakuwa na taarifa zozote.
Nilijikuta nikianza kuzoea taratibu maisha ya peke yangu na kuamua kujichanganya kama zamani huku moyoni nikiwa na swali lisilo na jibu, mume wangu amekwenda wapi?
Hata kama angekuwa amekwenda kutafuta maisha bado alitakiwa kuniaga kwa vile mimi ndiye nilikuwa mkewe na mtu wake wa karibu. Miezi minane ilikatika bila kujua mume wangu yupo wapi huku nikizidi kuwa katika mtihani wa wanaume walionitaka kimapenzi huku mama na dada zangu wakitumika kunikuwadia.
Kuna mwanaume mmoja aliahidi kama nikimkubali basi angeninunulia gari. Najua angekuwa mtu mwingine angekubali kwa vile hakuwa na mawasiliano na mumewe aliyeondoka bila kuaga.
Lakini kwangu sikuwa hivyo labda ningepata taarifa ya kifo cha mume wangu tena niwe na kithibitisho, hapo ndipo naweza kubadili mawazo na kwa mwanaume muoaji si wa kunichezea kwa vile ana fedha zake mwisho kila mwenye fedha kuugeuza mwili wangu kama dekio.
Baada ya kukaa muda mrefu nilipata wazo la kutafuta kazi. Wazo langu nilimueleza dada ambaye alinieleza atamwambia bwana yake mmoja aliyekuwa na cheo kwenye kampuni moja mjini.
Baada ya kumweleza, alimwuliza nilikuwa nina ujuzi gani, kwa kweli sikuwa na ujuzo wowote zaidi ya elimu ya kidato cha nne tena niliyefeli. Lakini alikubali kunipatia kazi katika duka moja la Supermarket ambalo aliniahidi kunipa jibu baada ya wiki.
Nilimuomba Mungu nipate kazi ili niwe bize nisiwe na wazo baya la kujiingiza katika umalaya wa kuugawa mwili wangu kama pipi. Siku moja tukiwa sebuleni na mama pamoja na dada zangu tukiangalia na kusikiliza muziki wa taarab kwenye video, zikiwa siku nne kabla ya kupata jibu la kuanza kazi, tulisikia sauti ya gari likisimama nje ya nyumba.
Hakuna aliyekuwa na mawazo nalo kwa kujua kama mgeni wetu atapiga honi au kugonga mlango kwa vile marafiki za dada zangu wengi walikuwa wenyeji pale.
Niliwaona kina dada wakitazamana, nilijua kila mmoja alikuwa akijiuliza labda ni mgeni wake, kwa vile hawakuwa na bwana wa siku zote, aliyewahi ndiye aliyepata nafasi ya kuwa na mmoja wa dada zangu.
Mara mlango uligongwa, wote tuliondoa macho kwenye video na kuangalia mlangoni.
"Karibu," dada mkubwa alikaribisha.
Tukiwa tunaangalia mlangoni, sikuamini kumuona mume wangu Beka akiingia. Jamani hata nilivyoamka sijui, nilijikuta nikimkumbatia kwa nguvu na kufanya wote tuanguke chini.
"Yoyooo mume wangu."
Ajabu nyingine baada ya mume wangu kuingia, mama alipata mshtuko na kudondoka toka juu ya kochi mpaka chini. Kwa kweli sikuelewa ule ulikuwa mshtuko wa nini.
Niliamini kabisa huenda mama naye hakutegemea kumuona mkwewe ambaye alikuwa amempoteza zaidi ya miezi minane ameonekana tena akiwa katika hali nzuri. Ilibidi tuingie kwenye kazi ya kumhudumia mama aliyekuwa amepoteza fahamu.
Baada ya kuzinduka aliomba tumuingize chumbani kwake, tulifanya vile mara moja. Baada ya dakika chache, niliwaacha dada zangu nikatoka kwenda kwa mume wangu aliyerudi kama maji jangwani.
Kabla sijazungumza lolote dada zangu nao walitoka, tulijikuta mimi na dada zangu tukiwa na hamu ya kuzungumza na mume wangu.
"Jamani shemeji za siku?" dada yangu alimuuliza.
"Nzuri tu."
"Mmh! Naona mambo si mabaya."
"Kiasi."
"Jamani basi niacheni nizungumze kwanza na mume wangu," niliingilia kati baada ya kuona wananizuia hamu yangu kwa mume wangu.
Dada zangu walinipisha, lakini kabla ya kuondoka walimpiga mzinga shemeji yao.
"Shem makoo makavu," wakimaanisha wanataka kunywa.
Mume wangu bila kusema kitu aliingiza mkono kwenye mfuko wa juu wa shati na kutoa elfu kumi na kuwapatia.
"Mambo si hayo," walishukuru na kuondoka na kuniacha nikiwa na shauku ya kuzungumza na mume wangu. Nilimwangalia kama ndiyo siku ya kwanza ya ndoa yetu.
"Jamani mume wangu karibu," nilimkaribisha na kumshika kwa kumuogopa.
"Asante," alijibu kwa sauti ya chini.
"Jamani Beka mbona sauti ya chini unaumwa?"
"Hapana."
"Uchovu wa safari?'
"Wala, nipo sawa."
"Sasa tatizo nini?"
"Basi tu, sasa Mwaija naomba tuzungumze nje kwa vile mi si mkaaji."
"Kwa nini tusizungumzie chumbani kwetu."
"Hakuna tatizo."
Tulitoka hadi nje ya nyumba kubwa na kuelekea kwenye chumba changu kilichokuwa banda la uani. Tuliingia chumbani kwetu ambako nilikuwa nimepatengeneza kama nilikuwa naishi na mtu, muda wote chumba changu kilikuwa kwenye hali ya usafi.
"Karibu mume wangu," nilimkaribisha kwa heshima zote.
"Asante," bado asante yake haikuwa na uchangamfu.
"Mume wangu mbona huoneshi furaha kuwa karibu yangu, au hujanikumbuka?"
"Kwa kweli najitahidi lakini inashindikana."
"Nini?"
"Najua hata nikikueleza huwezi kunielewa, lakini ipo siku Mungu akijalia tukionana nitakueleza na utanielewa."
"Kitu gani mume wangu?"
"Nina mambo mengi lakini siwezi kukueleza ila naomba nitakachokifanya ukipokee."
"Kitu gani mume wangu."
"Mwaija nakupenda sana na naamini mpaka nakufa sitampata mwanamke aliyenipenda kama wewe."
"Mume wangu mbona unasema aliyekupenda kwani mi nimekufa si nipo?" kauli yake ilinishtua.
"Ndiyo maana nikasema kila nitakachokisema itakuwa vigumu kunielewa."
"Beka mbona leo sikuelewi?"
"Najua hutanielewa ila elewa sina jinsi lazima iwe hivyo."
"Beka! Una nini?"
"Narudia tena katika maisha yangu mpaka naingia kaburini sitapata tena mwanamke kama wewe."
"Beka au umesikia nimeolewa?"
"Hapana, sijasikia chochote kibaya kwako ndiyo maana nasema sitapata mwanamke mzuri na mwenye heshima kama wewe katika maisha yangu."
"Kwa hiyo unarudi ulipokuwa na kuniacha nyumbani?"
"Hapana, nina imani unayajua maisha yetu yalivyokuwa?"
"Ndiyo mume wangu."
"Kilichotokea mpaka kutengana unakijua?"
"Ndiyo mume wangu, baada ya maisha yetu kubadilika na kuwa magumu."
"Unajua baada ya miezi sita mimi ningekuwa wapi?"
"Mume wangu mi nitajuaje wewe ungekuwa wapi?"
"Unajua sababu ya mama yako kuanguka nilipoingia?"
"Hata sijui."
"Basi kama tungekuwa pamoja leo hii ningebakia jina."
"Ungebakia jina? Una maana gani?"
"Mwaija naomba nikueleze kilichonileta kwenu."
"Kipi mume wangu?"
"Nimeamua kuachana na wewe."
"Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
"Leo nimekuletea talaka yako."
"Talaka yangu! Kivipi?" nilishtuka na kushindwa kumuelewa mume wangu alikuwa anamaanisha nini.
"Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitakayokupa ni usalama wa maisha yangu."


Itaendelea

MAMA YANGU ADUI YANGU - 8

ILIPOISHIA;
SIKU zilizidi kukatika bila kupata taarifa za mume wangu yupo wapi.
Mama alinieleza niendelee na maisha yangu ikibidi hata kutafuta mwanaume kwa wakati ule wa kuniliwaza wakati namsubiri mume wangu.
SASA ENDELEA...
Japokuwa kulikuwa na wanaume wengi walionimezea mate lakini sikuwa tayari kujidhalilisha. Niliiheshimu ndoa yangu pia mwenyewe nilijiheshimu, sikutaka kuwa na sifa mbaya kama dada zangu. Siku nazo zilikatika bila kupata taarifa za mume wangu.
Sikuchoka kwenda kuuliza kwao na kijiweni kwake labda kulikuwa kuna mtu ana taarifa zake. Kila nilipouliza majibu yalikuwa yaleyale, hawakuwa na taarifa zozote.
Nilijikuta nikianza kuzoea taratibu maisha ya peke yangu na kuamua kujichanganya kama zamani huku moyoni nikiwa na swali lisilo na jibu, mume wangu amekwenda wapi?
Hata kama angekuwa amekwenda kutafuta maisha bado alitakiwa kuniaga kwa vile mimi ndiye nilikuwa mkewe na mtu wake wa karibu. Miezi minane ilikatika bila kujua mume wangu yupo wapi huku nikizidi kuwa katika mtihani wa wanaume walionitaka kimapenzi huku mama na dada zangu wakitumika kunikuwadia.
Kuna mwanaume mmoja aliahidi kama nikimkubali basi angeninunulia gari. Najua angekuwa mtu mwingine angekubali kwa vile hakuwa na mawasiliano na mumewe aliyeondoka bila kuaga.
Lakini kwangu sikuwa hivyo labda ningepata taarifa ya kifo cha mume wangu tena niwe na kithibitisho, hapo ndipo naweza kubadili mawazo na kwa mwanaume muoaji si wa kunichezea kwa vile ana fedha zake mwisho kila mwenye fedha kuugeuza mwili wangu kama dekio.
Baada ya kukaa muda mrefu nilipata wazo la kutafuta kazi. Wazo langu nilimueleza dada ambaye alinieleza atamwambia bwana yake mmoja aliyekuwa na cheo kwenye kampuni moja mjini.
Baada ya kumweleza, alimwuliza nilikuwa nina ujuzi gani, kwa kweli sikuwa na ujuzo wowote zaidi ya elimu ya kidato cha nne tena niliyefeli. Lakini alikubali kunipatia kazi katika duka moja la Supermarket ambalo aliniahidi kunipa jibu baada ya wiki.
Nilimuomba Mungu nipate kazi ili niwe bize nisiwe na wazo baya la kujiingiza katika umalaya wa kuugawa mwili wangu kama pipi. Siku moja tukiwa sebuleni na mama pamoja na dada zangu tukiangalia na kusikiliza muziki wa taarab kwenye video, zikiwa siku nne kabla ya kupata jibu la kuanza kazi, tulisikia sauti ya gari likisimama nje ya nyumba.
Hakuna aliyekuwa na mawazo nalo kwa kujua kama mgeni wetu atapiga honi au kugonga mlango kwa vile marafiki za dada zangu wengi walikuwa wenyeji pale.
Niliwaona kina dada wakitazamana, nilijua kila mmoja alikuwa akijiuliza labda ni mgeni wake, kwa vile hawakuwa na bwana wa siku zote, aliyewahi ndiye aliyepata nafasi ya kuwa na mmoja wa dada zangu.
Mara mlango uligongwa, wote tuliondoa macho kwenye video na kuangalia mlangoni.
"Karibu," dada mkubwa alikaribisha.
Tukiwa tunaangalia mlangoni, sikuamini kumuona mume wangu Beka akiingia. Jamani hata nilivyoamka sijui, nilijikuta nikimkumbatia kwa nguvu na kufanya wote tuanguke chini.
"Yoyooo mume wangu."
Ajabu nyingine baada ya mume wangu kuingia, mama alipata mshtuko na kudondoka toka juu ya kochi mpaka chini. Kwa kweli sikuelewa ule ulikuwa mshtuko wa nini.
Niliamini kabisa huenda mama naye hakutegemea kumuona mkwewe ambaye alikuwa amempoteza zaidi ya miezi minane ameonekana tena akiwa katika hali nzuri. Ilibidi tuingie kwenye kazi ya kumhudumia mama aliyekuwa amepoteza fahamu.
Baada ya kuzinduka aliomba tumuingize chumbani kwake, tulifanya vile mara moja. Baada ya dakika chache, niliwaacha dada zangu nikatoka kwenda kwa mume wangu aliyerudi kama maji jangwani.
Kabla sijazungumza lolote dada zangu nao walitoka, tulijikuta mimi na dada zangu tukiwa na hamu ya kuzungumza na mume wangu.
"Jamani shemeji za siku?" dada yangu alimuuliza.
"Nzuri tu."
"Mmh! Naona mambo si mabaya."
"Kiasi."
"Jamani basi niacheni nizungumze kwanza na mume wangu," niliingilia kati baada ya kuona wananizuia hamu yangu kwa mume wangu.
Dada zangu walinipisha, lakini kabla ya kuondoka walimpiga mzinga shemeji yao.
"Shem makoo makavu," wakimaanisha wanataka kunywa.
Mume wangu bila kusema kitu aliingiza mkono kwenye mfuko wa juu wa shati na kutoa elfu kumi na kuwapatia.
"Mambo si hayo," walishukuru na kuondoka na kuniacha nikiwa na shauku ya kuzungumza na mume wangu. Nilimwangalia kama ndiyo siku ya kwanza ya ndoa yetu.
"Jamani mume wangu karibu," nilimkaribisha na kumshika kwa kumuogopa.
"Asante," alijibu kwa sauti ya chini.
"Jamani Beka mbona sauti ya chini unaumwa?"
"Hapana."
"Uchovu wa safari?'
"Wala, nipo sawa."
"Sasa tatizo nini?"
"Basi tu, sasa Mwaija naomba tuzungumze nje kwa vile mi si mkaaji."
"Kwa nini tusizungumzie chumbani kwetu."
"Hakuna tatizo."
Tulitoka hadi nje ya nyumba kubwa na kuelekea kwenye chumba changu kilichokuwa banda la uani. Tuliingia chumbani kwetu ambako nilikuwa nimepatengeneza kama nilikuwa naishi na mtu, muda wote chumba changu kilikuwa kwenye hali ya usafi.
"Karibu mume wangu," nilimkaribisha kwa heshima zote.
"Asante," bado asante yake haikuwa na uchangamfu.
"Mume wangu mbona huoneshi furaha kuwa karibu yangu, au hujanikumbuka?"
"Kwa kweli najitahidi lakini inashindikana."
"Nini?"
"Najua hata nikikueleza huwezi kunielewa, lakini ipo siku Mungu akijalia tukionana nitakueleza na utanielewa."
"Kitu gani mume wangu?"
"Nina mambo mengi lakini siwezi kukueleza ila naomba nitakachokifanya ukipokee."
"Kitu gani mume wangu."
"Mwaija nakupenda sana na naamini mpaka nakufa sitampata mwanamke aliyenipenda kama wewe."
"Mume wangu mbona unasema aliyekupenda kwani mi nimekufa si nipo?" kauli yake ilinishtua.
"Ndiyo maana nikasema kila nitakachokisema itakuwa vigumu kunielewa."
"Beka mbona leo sikuelewi?"
"Najua hutanielewa ila elewa sina jinsi lazima iwe hivyo."
"Beka! Una nini?"
"Narudia tena katika maisha yangu mpaka naingia kaburini sitapata tena mwanamke kama wewe."
"Beka au umesikia nimeolewa?"
"Hapana, sijasikia chochote kibaya kwako ndiyo maana nasema sitapata mwanamke mzuri na mwenye heshima kama wewe katika maisha yangu."
"Kwa hiyo unarudi ulipokuwa na kuniacha nyumbani?"
"Hapana, nina imani unayajua maisha yetu yalivyokuwa?"
"Ndiyo mume wangu."
"Kilichotokea mpaka kutengana unakijua?"
"Ndiyo mume wangu, baada ya maisha yetu kubadilika na kuwa magumu."
"Unajua baada ya miezi sita mimi ningekuwa wapi?"
"Mume wangu mi nitajuaje wewe ungekuwa wapi?"
"Unajua sababu ya mama yako kuanguka nilipoingia?"
"Hata sijui."
"Basi kama tungekuwa pamoja leo hii ningebakia jina."
"Ungebakia jina? Una maana gani?"
"Mwaija naomba nikueleze kilichonileta kwenu."
"Kipi mume wangu?"
"Nimeamua kuachana na wewe."
"Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
"Leo nimekuletea talaka yako."
"Talaka yangu! Kivipi?" nilishtuka na kushindwa kumuelewa mume wangu alikuwa anamaanisha nini.
"Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitakayokupa ni usalama wa maisha yangu."


Itaendelea
 
[h=1]MAMA YANGU ADUI YANGU - 9[/h]
ILIPOISHIA;
"Nimeamua kuachana na wewe."
"Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
"Leo nimekuletea talaka yako."
"Talaka yangu! Kivipi?" nilishtuka na kushindwa kumuelewa mume wangu alikuwa anamaanisha nini.
"Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitakayokupa ni usalama wa maisha yangu."
SASA ENDELEA...

"Beeka, nilitaka kukuua?"
"Walaa!"
"Sasa usalama upi?"
"Kwa leo hutanielewa."
"Nieleze nitakuelewa tu mume wangu."
"Ipo siku lakini siyo leo."
"Sasa unaniacha ili iweje?"
"Kila kitu mama yako anajua."
"Mama anajua nini?" jibu la mume wangu lilinishtua sana.
"Mwaija mama yako anajua kila kitu juu ya talaka hii."
"Anaijua kivipi?"
" We kamuulize."
"Ndiye aliyesema unipe?"
"Nikiondoka muulize mama yako atakujibu kila kitu tena kwa kirefu."
"Beka mbona sikuelewi, mara kujua kilichomuangusha mama, mara nimuulize mama kuhusu talaka yangu mbona sikuelewi?"
"Majibu ya maswali yote anayo mama yako, ila kila kilichopo hapa ni mali yako na sehemu ya kiwanja cha Charambe nitakiuza na kukupa haki yako. Siwezi kukudhulumu hata senti tano kwa vile ni haki yako."
"Beka umesikia maneno gani mabaya juu yangu? Au umeambiwa na mimi nilijiunga na dada zangu kufanya mchezo mchafu?" nilijikuta nikijitahidi kubashiri sababu ya kupewa talaka.
"Wala sivyo unavyodhania, hujafanya na nina amini huwezi kufanya."
"Umesikia nina mwanaume?"
"Hapana."
"Sasa kosa langu nini mpaka unaniacha mume wangu?"
"Huna kosa ila mama yako anajua kila kitu."
"Beka kwa nini aniambie mama yangu wakati wewe upo? Kama kuna kosa niweke wazi mume wangu, japokuwa naamini sina kosa kwako."
"Nimekwambia siku yoyote tukionana nitakueleza sababu ya talaka, naamini hutakasirika na utakubaliana nami kwa uamuzi wangu huu."
"Beka nimekaa muda gani kukusubiri? Nimejitunza kwa ajili ya ndoa yetu, nimevumilia mangapi leo hii nakuona mume wangu furaha yangu unaigeuza kilio? Beka umepata mwanamke mwingine? Nipo tayari kuishi uke wenza lakini siyo kuniacha Beka, bado nakuhitaji katika maisha yangu," nilimpigia magoti mume wangu ili abadili uamuzi.
"Hata mimi nakuhitaji tena sana."
"Sasa kwa nini unaniacha mume wangu, kama kuna kosa niambie ili nami nijitetee."
"Mwaija huna kosa."
"Jamani! Kama sina kosa, kwa nini unaniacha? Beka ni unyama gani unaonifanyia? Nimekusubiri kwa muda mrefu huku kila siku nikikuombea kwa Mungu ufanikiwe. Leo nimekuona kicheko changu kimegeuka kilio?
"Beka mume wangu nionee huruma, nimeteseka kwa miezi minane sijui upo wapi, unatokea na kunipa talaka, hii ni haki? Beka mume wangu hebu rudisha moyo nyuma. Naomba usijifikirie wewe peke yako, nifikirie na mimi mume wangu," niliendelea kupiga magoti mbele ya Beka ambaye naye alikuwa akitokwa na machozi huku mishipa ya kichwa ikiwa imemsimama.
Beka aliinama na kulia kilio cha kwikwi, kitu kilichonifanya ninyamaze na kumnyamazisha mume wangu.
"Beka usilie mume wangu, niambie tatizo nini, kama kuna uwezekano tulitatue."
"Mwaija," aliniita huku akinitazama, macho yakiwa mekundu.
"Naam mume wangu."
"Mwaija nakupenda zaidi ya sana, lakini lazima nikuache ili pawepo na usalama wa maisha yetu."
"Usalama upi? Mbona sikuelewi?"
"Kwa leo hutanielewa, naomba nikuachie mzigo wako mi niondoke."
"Mzigo gani Beka?"
"Talaka yako."
"Beka unasema kweli au unatania?"
"Sijawahi kukutania," Beka alisema huku akiingiza mkono kwenye mfuko wa shati na kunipa karatasi.
Niliipokea nikiwa siamini, niliifungua na kuisoma, kweli ilikuwa talaka moja. Nilipatwa na mshtuko na kuanguka chini.
***
Nilipozinduka nilijikuta nipo chini nimelazwa, pembeni walikuwepo dada zangu.
"Vipi Mwaija?"
"Beka yupo wapi?" niliwauliza kwanza mume wangu.
"Amekuja kutuita na kutueleza umepatwa na mshtuko, tumeingia ndani na kukuta umepoteza fahamu, baada ya huduma ya kwanza umezinduka."
"Beka yupo wapi?" niliendelea kumuulizia mume wangu.
Itaendelea Alkhamisi ijayo....................
 
mhhh endelea please kesho naisubiri mungu akipenda unakatisha natamani nisome mpaka mwisho please usisahau
 
jamani naomba uendelee na hadithi hii ni nzuri sana na inafundisha, big up SANA.
 
jamani naomba uendelee na hadithi hii ni nzuri sana na inafundisha, big up SANA.
Kweli inafundisha ujinga mtupu.

Toka lini mama yako akawa adui yako!

Yani mwanaume wako anaamua kukuwacha sababu ya mama yako!


KWANINI MME WAKO ASIWE ADUI YAKO, mana anakuwacha kwa sababu ya watu, mimi namuona mtoa thread hii anatafuta tu vita na mama yake.
 
Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili na jamaa na mayatima na masikini na jirani wa karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wanao jifakhiri, [4:36]

jazzakallahu khair!
 
Kweli inafundisha ujinga mtupu.

Toka lini mama yako akawa adui yako!

Yani mwanaume wako anaamua kukuwacha sababu ya mama yako!

sio lazima


KWANINI MME WAKO ASIWE ADUI YAKO, mana anakuwacha kwa sababu ya watu, mimi namuona mtoa thread hii anatafuta tu vita na mama yake.
inafundisha kwani wewe huwezi kujifunza chochote hapo? au ndo kusema kuwa mambo kama hayo hayapo katika jamii yetu! haya mambo yapo sana tu, sio kwamba inafundisha kuchukia mama zetu hapana ila ni kuwa makini na tabia kama hizo za mama kwenda kwa mwanae kila siku, anafuata nini kwa mwanae kama sio kuharibu ndoa yao, mbona mwanae au wewe unaona alivyokuwa anamshauri binti yake asiolewe ni vizuri, soma vizuri utailewa, angalia tabia za dada zake na binti je ni nzuri?
 
Vitu kama hizi za kurndelea mara part II mara Part III sizipendiiii si kwa vibaya lakini MziziMkavu maliza story mara moja bana.Kama nakukwaza Im deeply sory

eeeh ni kama unaenda uani, unakata gogo kidogo humalizi , halafu unarudi unakatena, na tena na tena badala ya kushusha mzigo wote pwaaa...............!:becky:
 
MAMA YANGU ADUI YANGU - 10-11

  • ILIPOISHIA;
    "Kwa leo hutanielewa, naomba nikuachie mzigo wako mi niondoke."
    "Mzigo gani Beka?"
    "Talaka yako."
    "Beka unasema kweli au unatania?"
    "Sijawahi kukutania," Beka alisema huku akiingiza mkono kwenye mfuko wa shati na kunipa karatasi.
    Niliipokea nikiwa siamini, niliifungua na kuisoma kweli ilikuwa talaka moja. Nilipatwa na mshtuko na kuanguka chini.
    ***
    Nilipozinduka nilijikuta nimelazwa chini, pembeni walikuwepo dada zangu.
    "Vipi Mwaija?" dada mkubwa aliniuliza kwa sauti ya upole.
    "Beka yupo wapi?" niliwauliza kwanza mume wangu.
    "Amekuja kutuita na kutueleza umepatwa na mshtuko, tumeingia ndani na kukuta umepoteza fahamu na baada ya kupewa huduma ya kwanza umezinduka."
    "Beka yupo wapi?" niliendelea kumuulizia mume wangu.
    SASA ENDELEA...


    "Baada ya kutuita tulijua tutakuwa naye ndani, lakini kumbe yeye ameondoka. Beka ni mwanaume muuaji mkubwa sikutegemea," alisema dada mkubwa kwa hasira.
    Macho yangu yalitua kwenye mkono wa dada na kumuona ameshikilia karatasi, nilinyanyuka na kumpokonya ile karatasi na kuisoma, nilikuta kweli ni talaka yangu.
    "Jamani kosa langu nini mpaka nipewe talaka?" niliuliza huku nikiangua kilio.
    "Sasa unatuuliza sisi wakati mlikuwa wenyewe ndani?" dada alionesha kunishangaa.
    "Dada kwani kawaambia sababu ya kunipa talaka?"
    "Hajatuambia kitu zaidi ya kutuita na kutueleza kuwa umeanguka. Lazima wewe unajua sababu ya kupewa talaka."
    "Dada zangu hata sijui chochote, basi ameamua tu, yaani kujizuia siku zote kwa ajili yake, matokeo yake kunipa talaka. Kweli hii ni halali?" niliuliza kwa uchungu huku nikiendelea kulia.
    "Sasa mdogo wangu sisi tutajuaje? Wewe ndiye uliyetakiwa kutuambia sababu."
    "Najua ninyi ndiyo mmeniponza na kuonekana nami nina wanaume wa nje," niliwalaumu dada zangu.
    "Koma weee, upuuzi wako na mtalaka wako isikufanye utuvunjie adabu," dada zangu walinijia juu.
    "Laki.." nilikatwa kauli.
    "Funga domo lako, alikuja akakufumania?"
    "Hapana."
    "Sasa kwa nini utulaumu, kwani wakati anakuoa na sasa, kipi kimebadilika hapa kwetu?"
    Niliona hakuna msaada wowote kwa dada zangu, niliendelea kulia mpaka mama alipokuja na kunikemea.
    "We mtoto mbona unaleta uchuro?"
    "Mama inauma, kosa langu nini la kupewa talaka?"
    "Wewe Mwaija kipi cha ajabu kwani wewe ni wa kwanza kuachwa. Kipi kimepungua kwako toka aondoke huyo mwana haramu wako, hukulala na njaa wala kulala nje."
    "Mama inauma mtu nimsubiri siku zote atokee na kunipa talaka, hii ni halali kweli? Si bure kuna kitu tu mama," nilimlalamikia mama huku nikiendelea kulia.
    "Kama unajua huna kosa achana naye, huenda keshaoa huko alipokwenda. Amekuja kuachana na wewe. Unajuaje pengine mwanamke aliyempata alimdanganya hajaoa."
    "Lakini mama mbona mume wangu kaniambia eti wewe ndiye unayejua sababu ya talaka yangu?"
    "Nini! Mimi niijue talaka yako?" kauli yangu ilionesha kumshtua sana mama.
    "Ndiyo mama."
    "Sasa haya makubwa! Yaani mimi nijue sababu ya talaka yako wakati mnapeana mimi sikuwepo?"
    "Hapana, ila mume wangu kasema wewe unajua sababu ya mimi kupewa talaka."
    "Mumeo ndiyo kakwambia hivyo?"
    "Ndiyo, kasema nikuulize wewe."
    "Hii ajabu! Mwenye kutoa talaka asikwambie, mimi nitajuaje? Huoni huo ni ukosaji wa adabu anaofanya mumeo? Shukuru Mungu kupewa talaka, ni wazi yule mwanaume alikuwa hakufai na pia hakuwa na mapenzi nawe."
    "Hapana mama, mume wangu namfahamu vizuri kuna kitu mama unakijua ila unanificha, yeye si mwendawazimu kusema hivyo."
    "Nikufiche ili iweje?"
    "Eti, halafu nini kilichokuangusha wakati alipoingia mume wangu mpaka ukapoteza fahamu?"
    "Mwaija! Swali gani hilo?" niliona mama akinibadilikia.
    "Mama kuna ubaya gani kukuuliza?"
    "Ulitaka nife ufurahi?"
    "Mama mi nifurahie kufa kwako?" nilimshangaa mama.
    "Sasa hilo ni swali gani?"
    "Basi mama yamekwisha, lakini bado talaka yangu naamini kuna kitu si bure."
    "Mumeo asituchanganye, upuuzi wake usitugombanishe bure kuwa makini mwanangu."
    "Mmh! Sawa nitajua tu," ilibidi nikubali ili yaishe kwani hapakuwa na ushahidi wa moja kwa moja.
    "Hilo ndilo neno."
    Baada ya kusema vile mama alitoka nje na kuniacha peke yangu, wakati huo dada zangu walikuwa wameshatoka kitambo na kuniacha na mama. Chumba nilikiona kichungu niliitazama upya talaka yangu huku nikitokwa machozi, haikuwa na mabadiliko yoyote zaidi ya kuandikwa nimeachwa kwa talaka moja.
    Siku hiyo nilishinda chumbani kwangu nimejilaza kifudifudi nikiwa nimelalia mto nikiendelea kulia. Nilijitahidi kuvuta kumbukumbu katika maisha yangu ya ndoa kama kuna kosa lolote nililowahi kumkosea mume wangu hata kwa siri kufikia kuamua kunipa talaka.
    Baada ya kutafuta kwa muda, sikubaini kosa nililomtendea mume wangu wala kuliwaza, maneno ya mume wangu yalinirudia kichwani kuhusu sababu ya fumbo la talaka yangu. Maneno yalijirudia kichwani mwangu kama mtu aliyekuwa akisikiliza redio.
    "Unajua baada ya miezi sita mimi ningekuwa wapi?"
    "Mume wangu mi nitajuaje wewe ungekuwa wapi?"
    "Unajua sababu ya mama yako kuanguka nilipoingia?"
    "Hata sijui."
    "Basi kama tungekuwa pamoja mpaka leo hii ningebakia jina."
    "Ungebakia jina? Una maana gani?"
    "Mwaija naomba nikueleze kilichonileta kwenu."
    "Kipi mume wangu?"
    "Nimeamua kuachana na wewe."
    "Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
    "Leo nimekuletea talaka yako."
    "Talaka yangu! Kivipi?" lilikuwa neno lililonishtua sana.
    "Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitayokupa ni usalama wa maisha yangu."
    Nikarudia yale maneno kwa sauti ya chini kama namwambia mtu.
    "Miezi sita mume wangu angekuwa wapi? Na...na sababu ya mama kudondoka! Kudondoka..mama...i..i...naashiria nini? Kwani kuna nini kati ya siri ya talaka na mama? Mmh! Eti kunipa talaka ni usalama wa maisha yake...mmh! Amesikia nimeathirika?... Mungu wangu lazima kuna mtu amekwenda kumpa uongo mume wangu kuwa nimekuwa malaya na kutembea na mtu aliyeathirika. Mmh! La...la...kini mbo...mbo...na ameuliza kuanguka kwa mama? Jamani hii talaka ina nini, sikubali lazima nimtafute Beka anieleze kiundani...aa...au mama alimtaka mume wangu kimapenzi? Jamani mbona sipati jibu, jamani naweza kuwa kichaa bure."
    Nilijikuta nikikosa jibu na kukifanya kichwa kisitulie, kwani kilikuwa kikiniuma kama kidonda kila nilipolazimisha kuwaza kitu kilichokuwa hakina jibu.

    Itaendelea Jumapili
 
Mkuu hututendei haki, kama kuna uwezekano wa kumalizia hii kitu tunakuomba ufanye hivyo, hadi jpili tena duh! Please please, do the needful comrade!
 
MziziMkavu 27th January 2013 23:47
#1 JF Senior Expert Member Array


Join Date : 3rd February 2009
Location : European Union
Posts : 19,499
Rep Power : 16144
Likes Received5928
Likes Given19698


[h=2]
icon1.png
Mama yangu adui yangu[/h]
WASWAHILI wanasena uchungu wa mwana aujuae mzazi, lakini kwa mama yetu ilikuwa kinyume. Sikuamini mama yetu mzazi kuwa chanzo cha matatizo ya familia yetu, pengine hata mimi kushindwa kufikia ndoto zangu za kusoma hadi chuo kikuu na kuishia kidato cha nne huku nikifeli vibaya.

Mwanzo sikuelewa lolote kwa vile nilikuwa na akili za kitoto na kuona kila kitu kiko sawa. Lakini nilikuja kuufahamu ubaya wa mama baada ya kuingia kwenye ndoa ambayo ilighubikwa na utata mkubwa na hapo ndipo nilipoyaona makucha ya mama. Ni mama yangu lakini kama asingekuwa mzazi wangu sijui tungefikishana wapi.

Mambo aliyonitendea mama yangu, kama mzazi aliyenizaa kwa uchungu, hakutakiwa kunifanyia kamwe . Lakini kama sitatanguliza shukurani nitakuwa mwizi wa fadhila. Waswahili wanasema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Kwanza kabisa lazima nitangulize shukurani zangu za dhati kwa mama yangu mzazi, kwa kunizaa na kunilea, pia kunipa elimu aliyonikadiria mwenyewe. Hiyo ni hatua kubwa sana katika maisha ya mwanadamu anayopitia akiwa mikononi mwa wazazi wake. Kabla sijafunguka akili nilimuomba Mungu katika maisha yangu aniwezeshe uwezo wa kulipa hata robo ya yote aliyonifanyia mama yangu, japo nilijua ni kazi kubwa. Toka nikiwa binti mdogo nilijua mama yangu ndiyo kila kitu kwa vile alijitoa kwa ajili yetu.

Maisha yote tuliishi na mama yetu, sikubahatika kumuona baba, nilielezwa alifariki mama yangu akiwa na ujauzito wangu wa miezi sita, kwa hiyo sura ya baba yangu niliiona kwenye picha tu. Siku nilipojua siri ya kifo cha baba nilikuwa hoi. Nimeamini nyuma ya mioyo ya watu kuna siri kubwa, ndiyo maana huwezi kujua dhamira ya mtu. Namuomba Mungu asinipe moyo wa mama.

Najua unataka kujua kwa nini mama yetu alituzaa ili ageuke adui yetu namba moja, kwa vile tuko pamoja naomba ungana nami ili siku moja ukubaliane na kauli yangu ili kina mama wenye roho kama ya mama yangu wabadilike.

Naitwa Mwaija mtoto wa mwisho katika familia ya marehemu mzee Salmini. Japokuwa sikubahatika kumuona baba yangu naambiwa nilifanana naye sana. Katika familia ya watoto watano, wa kike wanne na wa kiume mmoja. Baada ya kumaliza elimu yangu ya sekondari kidato cha nne nilipata mchumba wa kunioa.

Ukweli mchumba wangu hakuwa mgeni kwangu, ni mwanaume wangu niliyeanza naye urafiki tangu nilipokuwa kidato cha pili. Mwanzo tulifanya mapenzi ya siri japokuwa kati ya dada zangu, mmoja alimfahamu baada ya siku moja kuniona naye kwa mbali. Aliponiuliza nilijaribu kumficha lakini aliponibana nilimweleza ukweli. Basi ikawa kila siku nikikutana na mpenzi wangu lazima nimpelekee dada zawadi.

Ahadi yetu ilikuwa nikimaliza kidato cha nne tuoane, japokuwa mwanzo nilikuwa na ndoto za kufika chuo kikuu, lakini mazingira ya nyumbani yalinifanya nipoteze mwelekeo wa masomo na kuyabadili mawazo yangu yote kuhamishia kwa mpenzi wangu ambaye muda mwingi baada ya masomo nilikwenda kwake.

Hata matokeo ya kidato cha nne yalipotoka na kuonesha nimefeli vibaya sikushtuka kama wengine waliofikia hatua ya kutaka kujiua. Kwangu ilikuwa sawa kwa vile niliamini kabisa muda ule ulikuwa muafaka kwa mimi kuolewa na Beka.

Baada ya matokeo nilimfuata mwenzangu na kumweleza ule ndiyo ulikuwa muda muafaka wa yeye kuja kujitambulisha rasmi nyumbani.
Siku nilipomtambulisha hakuwa mgeni kwa dada, baada ya kuondoka mpenzi wangu, familia yangu ilitaka kujua anafanya

kazi gani. Niliwaeleza ni dereva wa teksi.
“Teksi yake au ameajiriwa?” mama aliniuliza.
“Ameajiriwa.”
“Sasa akifukuzwa kazi mtakula nini?”
“Mama mbona umekimbilia kufukuzwa kazi kuliko yeye kununua yake?’
“Atawahi! Mwanangu hawa dada zako wamekosa nini hapa nyumbani?”
“Mama wao hawakupenda kukaa nyumbani bali mapenzi ya Mungu.”
“Hata kama kazi ya Mungu, lakini toka warudi nyumbani wana tatizo gani?”
“Hawana matatizo, lakini wao ndiyo hawataki kuolewa tena.”
“Hawataki kuolewa kwa sababu wanaume wasio na uwezo ni mzigo kwa familia tu, kesho akifukuzwa kazi nikulishe mimi?”
“Mama ni kuniombea kwa Mungu nifanikiwe.”
“Kwa kazi kama hiyo nakuomba uachane na wazo hilo,” mama alinikata maini.
“Mama siwezi kuachana na wazo hilo kwa vile nitakayeolewa ni mimi.”
“Kama una uamuzi wako, sawa olewa kwa amri yako.”
“Mama nipo tayari kuishi maisha yoyote ndani ya ndoa, tutaishi hivi mpaka lini tunajazana nyumbani hata heshima hatuna.”
“Kwa hiyo umefanya vibaya kwenye mtihani ili uolewe?”
“Mama uliniambiaje?”
“Nilikuambia nini?”
“Mama si uliniambia huna hela za kunisomesha tena?”
“Ndiyo umefeli kiasi hicho?”


Je Vipi wasomaji mumeipenda hii hadithi? nataka mawazo yenu mukiipenda ıtaendelea hamukuipenda bora niishie hapo mnasemaje?Toeni Mawazo yenu........

Jamani MAMA hata afanye kitu gani kamwe hawezi kuwa Adui yangu, Muda wote huo amekulea unasema Adui yako? Kweli Hiki ni kizazi cha nyoka, Alafu inaonyesha huyo Mwanamke anataka kuolewa ili ajenge jina naye kwamba ameolewa.
 
Back
Top Bottom