MAMA YANGU ADUI YANGU - 7-
ILIPOISHIA;
SIKU zilizidi kukatika bila kupata taarifa za mume wangu yupo wapi.
Mama alinieleza niendelee na maisha yangu ikibidi hata kutafuta mwanaume kwa wakati ule wa kuniliwaza wakati namsubiri mume wangu.
SASA ENDELEA...
Japokuwa kulikuwa na wanaume wengi walionimezea mate lakini sikuwa tayari kujidhalilisha. Niliiheshimu ndoa yangu pia mwenyewe nilijiheshimu, sikutaka kuwa na sifa mbaya kama dada zangu. Siku nazo zilikatika bila kupata taarifa za mume wangu.
Sikuchoka kwenda kuuliza kwao na kijiweni kwake labda kulikuwa kuna mtu ana taarifa zake. Kila nilipouliza majibu yalikuwa yaleyale, hawakuwa na taarifa zozote.
Nilijikuta nikianza kuzoea taratibu maisha ya peke yangu na kuamua kujichanganya kama zamani huku moyoni nikiwa na swali lisilo na jibu, mume wangu amekwenda wapi?
Hata kama angekuwa amekwenda kutafuta maisha bado alitakiwa kuniaga kwa vile mimi ndiye nilikuwa mkewe na mtu wake wa karibu. Miezi minane ilikatika bila kujua mume wangu yupo wapi huku nikizidi kuwa katika mtihani wa wanaume walionitaka kimapenzi huku mama na dada zangu wakitumika kunikuwadia.
Kuna mwanaume mmoja aliahidi kama nikimkubali basi angeninunulia gari. Najua angekuwa mtu mwingine angekubali kwa vile hakuwa na mawasiliano na mumewe aliyeondoka bila kuaga.
Lakini kwangu sikuwa hivyo labda ningepata taarifa ya kifo cha mume wangu tena niwe na kithibitisho, hapo ndipo naweza kubadili mawazo na kwa mwanaume muoaji si wa kunichezea kwa vile ana fedha zake mwisho kila mwenye fedha kuugeuza mwili wangu kama dekio.
Baada ya kukaa muda mrefu nilipata wazo la kutafuta kazi. Wazo langu nilimueleza dada ambaye alinieleza atamwambia bwana yake mmoja aliyekuwa na cheo kwenye kampuni moja mjini.
Baada ya kumweleza, alimwuliza nilikuwa nina ujuzi gani, kwa kweli sikuwa na ujuzo wowote zaidi ya elimu ya kidato cha nne tena niliyefeli. Lakini alikubali kunipatia kazi katika duka moja la Supermarket ambalo aliniahidi kunipa jibu baada ya wiki.
Nilimuomba Mungu nipate kazi ili niwe bize nisiwe na wazo baya la kujiingiza katika umalaya wa kuugawa mwili wangu kama pipi. Siku moja tukiwa sebuleni na mama pamoja na dada zangu tukiangalia na kusikiliza muziki wa taarab kwenye video, zikiwa siku nne kabla ya kupata jibu la kuanza kazi, tulisikia sauti ya gari likisimama nje ya nyumba.
Hakuna aliyekuwa na mawazo nalo kwa kujua kama mgeni wetu atapiga honi au kugonga mlango kwa vile marafiki za dada zangu wengi walikuwa wenyeji pale.
Niliwaona kina dada wakitazamana, nilijua kila mmoja alikuwa akijiuliza labda ni mgeni wake, kwa vile hawakuwa na bwana wa siku zote, aliyewahi ndiye aliyepata nafasi ya kuwa na mmoja wa dada zangu.
Mara mlango uligongwa, wote tuliondoa macho kwenye video na kuangalia mlangoni.
"Karibu," dada mkubwa alikaribisha.
Tukiwa tunaangalia mlangoni, sikuamini kumuona mume wangu Beka akiingia. Jamani hata nilivyoamka sijui, nilijikuta nikimkumbatia kwa nguvu na kufanya wote tuanguke chini.
"Yoyooo mume wangu."
Ajabu nyingine baada ya mume wangu kuingia, mama alipata mshtuko na kudondoka toka juu ya kochi mpaka chini. Kwa kweli sikuelewa ule ulikuwa mshtuko wa nini.
Niliamini kabisa huenda mama naye hakutegemea kumuona mkwewe ambaye alikuwa amempoteza zaidi ya miezi minane ameonekana tena akiwa katika hali nzuri. Ilibidi tuingie kwenye kazi ya kumhudumia mama aliyekuwa amepoteza fahamu.
Baada ya kuzinduka aliomba tumuingize chumbani kwake, tulifanya vile mara moja. Baada ya dakika chache, niliwaacha dada zangu nikatoka kwenda kwa mume wangu aliyerudi kama maji jangwani.
Kabla sijazungumza lolote dada zangu nao walitoka, tulijikuta mimi na dada zangu tukiwa na hamu ya kuzungumza na mume wangu.
"Jamani shemeji za siku?" dada yangu alimuuliza.
"Nzuri tu."
"Mmh! Naona mambo si mabaya."
"Kiasi."
"Jamani basi niacheni nizungumze kwanza na mume wangu," niliingilia kati baada ya kuona wananizuia hamu yangu kwa mume wangu.
Dada zangu walinipisha, lakini kabla ya kuondoka walimpiga mzinga shemeji yao.
"Shem makoo makavu," wakimaanisha wanataka kunywa.
Mume wangu bila kusema kitu aliingiza mkono kwenye mfuko wa juu wa shati na kutoa elfu kumi na kuwapatia.
"Mambo si hayo," walishukuru na kuondoka na kuniacha nikiwa na shauku ya kuzungumza na mume wangu. Nilimwangalia kama ndiyo siku ya kwanza ya ndoa yetu.
"Jamani mume wangu karibu," nilimkaribisha na kumshika kwa kumuogopa.
"Asante," alijibu kwa sauti ya chini.
"Jamani Beka mbona sauti ya chini unaumwa?"
"Hapana."
"Uchovu wa safari?'
"Wala, nipo sawa."
"Sasa tatizo nini?"
"Basi tu, sasa Mwaija naomba tuzungumze nje kwa vile mi si mkaaji."
"Kwa nini tusizungumzie chumbani kwetu."
"Hakuna tatizo."
Tulitoka hadi nje ya nyumba kubwa na kuelekea kwenye chumba changu kilichokuwa banda la uani. Tuliingia chumbani kwetu ambako nilikuwa nimepatengeneza kama nilikuwa naishi na mtu, muda wote chumba changu kilikuwa kwenye hali ya usafi.
"Karibu mume wangu," nilimkaribisha kwa heshima zote.
"Asante," bado asante yake haikuwa na uchangamfu.
"Mume wangu mbona huoneshi furaha kuwa karibu yangu, au hujanikumbuka?"
"Kwa kweli najitahidi lakini inashindikana."
"Nini?"
"Najua hata nikikueleza huwezi kunielewa, lakini ipo siku Mungu akijalia tukionana nitakueleza na utanielewa."
"Kitu gani mume wangu?"
"Nina mambo mengi lakini siwezi kukueleza ila naomba nitakachokifanya ukipokee."
"Kitu gani mume wangu."
"Mwaija nakupenda sana na naamini mpaka nakufa sitampata mwanamke aliyenipenda kama wewe."
"Mume wangu mbona unasema aliyekupenda kwani mi nimekufa si nipo?" kauli yake ilinishtua.
"Ndiyo maana nikasema kila nitakachokisema itakuwa vigumu kunielewa."
"Beka mbona leo sikuelewi?"
"Najua hutanielewa ila elewa sina jinsi lazima iwe hivyo."
"Beka! Una nini?"
"Narudia tena katika maisha yangu mpaka naingia kaburini sitapata tena mwanamke kama wewe."
"Beka au umesikia nimeolewa?"
"Hapana, sijasikia chochote kibaya kwako ndiyo maana nasema sitapata mwanamke mzuri na mwenye heshima kama wewe katika maisha yangu."
"Kwa hiyo unarudi ulipokuwa na kuniacha nyumbani?"
"Hapana, nina imani unayajua maisha yetu yalivyokuwa?"
"Ndiyo mume wangu."
"Kilichotokea mpaka kutengana unakijua?"
"Ndiyo mume wangu, baada ya maisha yetu kubadilika na kuwa magumu."
"Unajua baada ya miezi sita mimi ningekuwa wapi?"
"Mume wangu mi nitajuaje wewe ungekuwa wapi?"
"Unajua sababu ya mama yako kuanguka nilipoingia?"
"Hata sijui."
"Basi kama tungekuwa pamoja leo hii ningebakia jina."
"Ungebakia jina? Una maana gani?"
"Mwaija naomba nikueleze kilichonileta kwenu."
"Kipi mume wangu?"
"Nimeamua kuachana na wewe."
"Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
"Leo nimekuletea talaka yako."
"Talaka yangu! Kivipi?" nilishtuka na kushindwa kumuelewa mume wangu alikuwa anamaanisha nini.
"Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitakayokupa ni usalama wa maisha yangu."
Itaendelea
MAMA YANGU ADUI YANGU - 8
ILIPOISHIA;
SIKU zilizidi kukatika bila kupata taarifa za mume wangu yupo wapi.
Mama alinieleza niendelee na maisha yangu ikibidi hata kutafuta mwanaume kwa wakati ule wa kuniliwaza wakati namsubiri mume wangu.
SASA ENDELEA...
Japokuwa kulikuwa na wanaume wengi walionimezea mate lakini sikuwa tayari kujidhalilisha. Niliiheshimu ndoa yangu pia mwenyewe nilijiheshimu, sikutaka kuwa na sifa mbaya kama dada zangu. Siku nazo zilikatika bila kupata taarifa za mume wangu.
Sikuchoka kwenda kuuliza kwao na kijiweni kwake labda kulikuwa kuna mtu ana taarifa zake. Kila nilipouliza majibu yalikuwa yaleyale, hawakuwa na taarifa zozote.
Nilijikuta nikianza kuzoea taratibu maisha ya peke yangu na kuamua kujichanganya kama zamani huku moyoni nikiwa na swali lisilo na jibu, mume wangu amekwenda wapi?
Hata kama angekuwa amekwenda kutafuta maisha bado alitakiwa kuniaga kwa vile mimi ndiye nilikuwa mkewe na mtu wake wa karibu. Miezi minane ilikatika bila kujua mume wangu yupo wapi huku nikizidi kuwa katika mtihani wa wanaume walionitaka kimapenzi huku mama na dada zangu wakitumika kunikuwadia.
Kuna mwanaume mmoja aliahidi kama nikimkubali basi angeninunulia gari. Najua angekuwa mtu mwingine angekubali kwa vile hakuwa na mawasiliano na mumewe aliyeondoka bila kuaga.
Lakini kwangu sikuwa hivyo labda ningepata taarifa ya kifo cha mume wangu tena niwe na kithibitisho, hapo ndipo naweza kubadili mawazo na kwa mwanaume muoaji si wa kunichezea kwa vile ana fedha zake mwisho kila mwenye fedha kuugeuza mwili wangu kama dekio.
Baada ya kukaa muda mrefu nilipata wazo la kutafuta kazi. Wazo langu nilimueleza dada ambaye alinieleza atamwambia bwana yake mmoja aliyekuwa na cheo kwenye kampuni moja mjini.
Baada ya kumweleza, alimwuliza nilikuwa nina ujuzi gani, kwa kweli sikuwa na ujuzo wowote zaidi ya elimu ya kidato cha nne tena niliyefeli. Lakini alikubali kunipatia kazi katika duka moja la Supermarket ambalo aliniahidi kunipa jibu baada ya wiki.
Nilimuomba Mungu nipate kazi ili niwe bize nisiwe na wazo baya la kujiingiza katika umalaya wa kuugawa mwili wangu kama pipi. Siku moja tukiwa sebuleni na mama pamoja na dada zangu tukiangalia na kusikiliza muziki wa taarab kwenye video, zikiwa siku nne kabla ya kupata jibu la kuanza kazi, tulisikia sauti ya gari likisimama nje ya nyumba.
Hakuna aliyekuwa na mawazo nalo kwa kujua kama mgeni wetu atapiga honi au kugonga mlango kwa vile marafiki za dada zangu wengi walikuwa wenyeji pale.
Niliwaona kina dada wakitazamana, nilijua kila mmoja alikuwa akijiuliza labda ni mgeni wake, kwa vile hawakuwa na bwana wa siku zote, aliyewahi ndiye aliyepata nafasi ya kuwa na mmoja wa dada zangu.
Mara mlango uligongwa, wote tuliondoa macho kwenye video na kuangalia mlangoni.
"Karibu," dada mkubwa alikaribisha.
Tukiwa tunaangalia mlangoni, sikuamini kumuona mume wangu Beka akiingia. Jamani hata nilivyoamka sijui, nilijikuta nikimkumbatia kwa nguvu na kufanya wote tuanguke chini.
"Yoyooo mume wangu."
Ajabu nyingine baada ya mume wangu kuingia, mama alipata mshtuko na kudondoka toka juu ya kochi mpaka chini. Kwa kweli sikuelewa ule ulikuwa mshtuko wa nini.
Niliamini kabisa huenda mama naye hakutegemea kumuona mkwewe ambaye alikuwa amempoteza zaidi ya miezi minane ameonekana tena akiwa katika hali nzuri. Ilibidi tuingie kwenye kazi ya kumhudumia mama aliyekuwa amepoteza fahamu.
Baada ya kuzinduka aliomba tumuingize chumbani kwake, tulifanya vile mara moja. Baada ya dakika chache, niliwaacha dada zangu nikatoka kwenda kwa mume wangu aliyerudi kama maji jangwani.
Kabla sijazungumza lolote dada zangu nao walitoka, tulijikuta mimi na dada zangu tukiwa na hamu ya kuzungumza na mume wangu.
"Jamani shemeji za siku?" dada yangu alimuuliza.
"Nzuri tu."
"Mmh! Naona mambo si mabaya."
"Kiasi."
"Jamani basi niacheni nizungumze kwanza na mume wangu," niliingilia kati baada ya kuona wananizuia hamu yangu kwa mume wangu.
Dada zangu walinipisha, lakini kabla ya kuondoka walimpiga mzinga shemeji yao.
"Shem makoo makavu," wakimaanisha wanataka kunywa.
Mume wangu bila kusema kitu aliingiza mkono kwenye mfuko wa juu wa shati na kutoa elfu kumi na kuwapatia.
"Mambo si hayo," walishukuru na kuondoka na kuniacha nikiwa na shauku ya kuzungumza na mume wangu. Nilimwangalia kama ndiyo siku ya kwanza ya ndoa yetu.
"Jamani mume wangu karibu," nilimkaribisha na kumshika kwa kumuogopa.
"Asante," alijibu kwa sauti ya chini.
"Jamani Beka mbona sauti ya chini unaumwa?"
"Hapana."
"Uchovu wa safari?'
"Wala, nipo sawa."
"Sasa tatizo nini?"
"Basi tu, sasa Mwaija naomba tuzungumze nje kwa vile mi si mkaaji."
"Kwa nini tusizungumzie chumbani kwetu."
"Hakuna tatizo."
Tulitoka hadi nje ya nyumba kubwa na kuelekea kwenye chumba changu kilichokuwa banda la uani. Tuliingia chumbani kwetu ambako nilikuwa nimepatengeneza kama nilikuwa naishi na mtu, muda wote chumba changu kilikuwa kwenye hali ya usafi.
"Karibu mume wangu," nilimkaribisha kwa heshima zote.
"Asante," bado asante yake haikuwa na uchangamfu.
"Mume wangu mbona huoneshi furaha kuwa karibu yangu, au hujanikumbuka?"
"Kwa kweli najitahidi lakini inashindikana."
"Nini?"
"Najua hata nikikueleza huwezi kunielewa, lakini ipo siku Mungu akijalia tukionana nitakueleza na utanielewa."
"Kitu gani mume wangu?"
"Nina mambo mengi lakini siwezi kukueleza ila naomba nitakachokifanya ukipokee."
"Kitu gani mume wangu."
"Mwaija nakupenda sana na naamini mpaka nakufa sitampata mwanamke aliyenipenda kama wewe."
"Mume wangu mbona unasema aliyekupenda kwani mi nimekufa si nipo?" kauli yake ilinishtua.
"Ndiyo maana nikasema kila nitakachokisema itakuwa vigumu kunielewa."
"Beka mbona leo sikuelewi?"
"Najua hutanielewa ila elewa sina jinsi lazima iwe hivyo."
"Beka! Una nini?"
"Narudia tena katika maisha yangu mpaka naingia kaburini sitapata tena mwanamke kama wewe."
"Beka au umesikia nimeolewa?"
"Hapana, sijasikia chochote kibaya kwako ndiyo maana nasema sitapata mwanamke mzuri na mwenye heshima kama wewe katika maisha yangu."
"Kwa hiyo unarudi ulipokuwa na kuniacha nyumbani?"
"Hapana, nina imani unayajua maisha yetu yalivyokuwa?"
"Ndiyo mume wangu."
"Kilichotokea mpaka kutengana unakijua?"
"Ndiyo mume wangu, baada ya maisha yetu kubadilika na kuwa magumu."
"Unajua baada ya miezi sita mimi ningekuwa wapi?"
"Mume wangu mi nitajuaje wewe ungekuwa wapi?"
"Unajua sababu ya mama yako kuanguka nilipoingia?"
"Hata sijui."
"Basi kama tungekuwa pamoja leo hii ningebakia jina."
"Ungebakia jina? Una maana gani?"
"Mwaija naomba nikueleze kilichonileta kwenu."
"Kipi mume wangu?"
"Nimeamua kuachana na wewe."
"Sijakuelewa, kuachana kivipi?"
"Leo nimekuletea talaka yako."
"Talaka yangu! Kivipi?" nilishtuka na kushindwa kumuelewa mume wangu alikuwa anamaanisha nini.
"Mwaija, nakuacha huku nakupenda sana tena sana, lakini talaka nitakayokupa ni usalama wa maisha yangu."
Itaendelea