Mkoroshokigoli
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 14,593
- 5,582
Mama Tibaijuka anatafutwa na wapiga kura wake wa Jimbo la Muleba,leo asbui kwenye kipindi cha Super Mix baadhi ya wapiga kura wake ambao walikua wakihojiwa na Kituo cha redio cha East Africa walisema kuwa tangu wamchague mbunge wao kuna maeneo hajapita kabisa,hasa maeneo ya vijijini,wanadai amewasahau na amehamia Dar es Salaam huku akionesha hana mpango nao.
Wapiga kura wa Mama Tibaijuka wakaenda mbali zaid na kusema,huduma muhim kama vile dawa kwenye zahanat wanakosa,ingawa wanaona magar yanashusha dawa lakin waendapo hospitalini au kwenye vituo vya afya husishia kuambiwa wakanunue kwani dawa hakuna.
Kuna mpiga kura wake mmoja alisema kuwa wakunga wanapata tabu sana kuwazalisha wake zao maana hata gloves hakuna,wao wanasema wanamhitaj mama Tibaijuka aende akawatembelee hasa huko vijijin ili wamueleze kero zao na azifanyie kazi,pia walilalamika kuwa hawashirikishwi kwenye kubuni miradi....
Hata hivyo mtangazaji alisema alipompigia sim mama Tibaijuka,simu haikupokelewa,sasa mimi kwakua niliisikia hii via redio nimeona bora niilete hapa,maana najua mama Tibaijuka ni memba wa JF kwa siku za karibuni.
Kwa sababu nilimskia Mtangazaji Zembwela akisema 'MAMA TIBAIJUKA POPOTE ULIPO KAMA UNATUSIKIA TUNAOMBA UJIBU HOJA ZA WAPIGA KURA WAKO.'
NAWASILISHA
EID NJEMA WADAU
Wapiga kura wa Mama Tibaijuka wakaenda mbali zaid na kusema,huduma muhim kama vile dawa kwenye zahanat wanakosa,ingawa wanaona magar yanashusha dawa lakin waendapo hospitalini au kwenye vituo vya afya husishia kuambiwa wakanunue kwani dawa hakuna.
Kuna mpiga kura wake mmoja alisema kuwa wakunga wanapata tabu sana kuwazalisha wake zao maana hata gloves hakuna,wao wanasema wanamhitaj mama Tibaijuka aende akawatembelee hasa huko vijijin ili wamueleze kero zao na azifanyie kazi,pia walilalamika kuwa hawashirikishwi kwenye kubuni miradi....
Hata hivyo mtangazaji alisema alipompigia sim mama Tibaijuka,simu haikupokelewa,sasa mimi kwakua niliisikia hii via redio nimeona bora niilete hapa,maana najua mama Tibaijuka ni memba wa JF kwa siku za karibuni.
Kwa sababu nilimskia Mtangazaji Zembwela akisema 'MAMA TIBAIJUKA POPOTE ULIPO KAMA UNATUSIKIA TUNAOMBA UJIBU HOJA ZA WAPIGA KURA WAKO.'
NAWASILISHA
EID NJEMA WADAU