Ndugu wan Jf.nawasalimu nyote.Kwa kuchangia tu kwenye maada hii,mm binafsi ningeomba mtoa maada alipoleta maada angeikamilisha vizuri kwa kubainisha ni zahanati zipi na vijiji gani vinavyomtafuta mh.prof.tibaijuka.Kwanza kasema Mama Tibaijuka anatafutwa jimboni,kule vijijini Muleba,angebainisha vijiji vile kwa majina ni vijiji gani M.T.hajawahai kuvitembelea.Kwa faida ya wengi Takwimu zinaonyesha kuwa Wilaya ya Muleba inavyo vijiji 167,ambapo kwa jimbo la Muleba Kusini,onavyo vojiji 112,kati ya 167.Ni Ukweli usiopingika kuwa M.T.amekuwa akifanya mikutano kwenye Kata yaan Makao makuu ya kata zote 25.za Jimbo zima.Ukweli wenyewe sio rahisi kuvifikia vijiji vyote kwan hata wakati wa kampeni mikitano ya Wabunge hufanyika Makao makuu ya kata. Pili Ndugu yangu mleta maada,anaposema zahanati hazina madawa,ingekuwa vema akabainisha pia ni zahanati zipi kwa majina.Ninavyojua wakati Mh.Prof.Tibajuka,amekuja,11.june.2013,kwa Ndege ya Serikali,alitembelea hospitali zote za Wilaya ya Muleba pamoja na zahanati lakini tatizo la madawa halikusikika kwa wananchi.Hospitali zilizotembelewa ni pamoja na Hosp.Teule ya Wilaya (Rubya hospital),Kagondo hispitalna Ndolage Hospital.Kwa upande wa zahanati,alifika Kaigara iliyopo Muleba Mjini,Kimeya Tarafa ya Kimwani,Rwantege tarafa ya Nshamba.Wagonjwa wenyewe ndio walikuwa shahidi kwa vinywa vyao kuwa Madawa yalikuwepo ya kutosha. Kama hiyo haitoshi,ni Juzi Mh.T.wakati wa Ziara ya Raisi alitembelea wananchi wa Rulanda ambao wanajenga zahanat na Mh.Raisi akawachangia Milion.3,akawambia kuwa atampa Mbunge wenu azilete.Hivyohivyo Kasindaga kata ya Kyebitembe wanajenga Zahanati,Raisi alichangia Mil.2.Habari njema zaidi Kasindaga Halmashauri wanaendelea na ujenzi wa zahanati ile kwa 26.Milioni.Kote huko hakuna mahali walilia madawa.Ndo nasema hivi huyu mleta maada ingekuwa vema akabainisha ni vijiji gani na zahanati gani walipolalamikia upungufu wa madawa?,Nasema hivyo Mh.Tibaijuka ametoka Muleba Jimboni na Mh.Raisi hilo tatizo hakuna mahali lilipotajwa.Ni vema mtandao huu ukatumika kusema ukweli,kwani itaweza kuisaidia kufuatilia na kutafuta ufumbuzi wa tatizo kama habari ni ya kweli.Lakini ieleweke pia hata kusema Uongo ni ufisadi. * Kwa nyongeza pale Kata ya Biirabo,kuna mradi wa ujenzi wa Zahanati chini ya Halmashauri ambapo Mh.Tibaijuka alichangia bati zote,lakini Halmashauri wakaamua kumalizia kila kitu,mpaka sasa imeishaezkwa.Kule Buhangaza hivyohivyo. * kuhusu hoja ya bus stand hii imejengwa tangu 2003,kutoka eneo ilipokua zamani.mpaka sasa standi hii ipo na imekamilika mabasi makubwa na madogo yanatua,pale bila tatizo,huduma za msingi zipo zote maduka ya uhakika na vyoo vya uhakika vimejengwa pale.kwa kufanya ulinganisho na standi zote zilizo katika mkoa wa kagera wala huwezi amini hoja yako,mtoa maada. * kitu muhimu kinachopaswa kueleweka kwa watu wote na hasa wale wanaopost news,kwenye mtandao wetu mtukufu,tujaribu kuheshimu usomi wetu,ambapo kusema ukweli ni zaidi ya yote. Mwisho ningeomba kama inawezekana tunapokuwa na thread nzuri na zenye uhakika basi tujitahidi kuzitoa kwa kuweka wazi majina yetu wazi na sio yale ya bandia,na niombe samahani kwa punctuation kwani niko vijijin na natumia blackbery,mniwie radhu kwa hilo. Denis, ktb/m.tibaijuka muleba.