mbalizi1
JF-Expert Member
- Dec 16, 2015
- 22,592
- 45,214
Hawawezi kukuelewa wanachojua wao ni lawama tu.Kabla ya kuandika waraka huu taja mradi mmoja tu umewahi kuendeshwa kwa faida na sisi wazawa? tumefilisi kila kitu na tunajenga vi stand vya bus Billion 5 havina thamani hata ya Million 100 moja. Tutajie shirika moja tumeweza kulikuza zaidi ya kuuwa. Mwendokasi tulikuwa sisi tumefanya nini? Ma bus hakuna na yaliyopo hayatoshi likiharibika ndio basi tena. SGR pale watu wanapiga pesa kwenye tickets hatari hawana hata uchungu wanajali matumbo yao tu. Yaani ni wizi mtupu wewe ukitaka kufilisika mradi wako mpe Mtanzania tu. Nimeona miradi ya barabara imefanywa na kampuni za wazawa ni aibu mashimo tupu mpaka miradi inarudiwa. Badala ya kulaumu tujiangalie sisi tumefanya nini?
SGR ikiendelea kuendeshwa na waajiriwa wazawa chini ya serikali inaenda kufa kifo cha mende.
Watanzania hatuajiriki. Tunaiba, tunahujumu, tunafilisi, tunachakaza, hatujali zaidi ya kujijali. Tu wavivu kuzidi kiumbe chochote kivivu Duniani. Ni waongo, wanafiki, mafisadi, ovyo kwelikweli.
Kazi kubwabwaja midomo pyeeeee!!!pyeeeee!!!!! Utadhani watu, hamna lolote zaidi ya kupiga domo.