Ladies & gents Salaam,
Nimeoa mwaka wa pili sasa. Changamoto za ugonjwa zimepelekea tukae na mama mkwe nyumbani tumuuguze. Yapata miezi miwili sasa anatazamia afya yake hapa kwetu. Age yake haizidi 50 and I'm early 30s.
Issues:
1. Ananiheshimu imefikia hatua ananiita baba kwa adabu mpaka naogopa.
2. Hawezi kukaa na mimi hata kupiga stori zaidi ya salaam tu. Yaani hata namkuta anaagalia tv nikiingia tuu kutoka job anaingia chumbani mda huo huo.
3. Ikibidi tupishane koridoni huwa anageuza njia kabisa.
4. She keeps telling her daughter chakula lazima nianze kupewa mimi kwanza tena kile kizuri na kingi.
5. Huwa haniangalii usoni kabisa (japo hii inaweza isiwe adabu).
6. Ole mke wangu aniache sebuleni peke yangu lazima amtimue aje aongee na baba.
Kwakweli yako mengi huyu mama anayafanya mpaka nimuone ana adabu iliyopitiliza.
Imefikia kipindi imebidi nibadili lifestyle. No more loud music no more think pombe at home. Halafu sasa mimi ni muongeaji kishenzi so nilixpect mama mkwe akija hadi idadi ya wa kupiganao story itaongezeka.
Japo mi mama bora ila mwenzenu ananikwaza kwa kweli.
Sent using
Jamii Forums mobile app