Malizia huu msemo: Ukivuliwa nguo sharti ………….....

Malizia huu msemo: Ukivuliwa nguo sharti ………….....

Binti wa zamani

Platinum Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
11,902
Reaction score
27,646
Nimesikiliza hotuba ya raisi akifungua rasmi bunge la 13 na nimeona ni kama ameanza kuinama na kujisitiri kutokana na yale yaliyotokea.

  1. Je, ili achutame kabisa kiungwana na kuepuka fedheha inabidi afanye nini?

  2. Kwa wenzangu mliosikiliza hotuba: je imewatia moyo au ndiyo imewaongeza hasira?

  3. Gen Z na wote wanaosapoti D9: kuna hoja hata moja imeongelewa ambayo inagusa malalamiko ya maandamano yaliyopita au yale yajayo?

Binafsi kwa niliyoyasikia nimeona ni inawezekana watawala wameona mabavu siyo suluhisho litakalotufikisha mahali pazuri kama taifa. 
Nafikiri haya mambo 5 yameashiria kwamba sauti za watanzania zina nguvu:
  • Kukiri kuhusu mauaji ya siku za uchaguzi na kutoa pole
  • Mchakato wa katiba mpya kurejea ndani ya siku 100 za kwanza
  • Kufuta kesi za uhaini kwa vijana
  • Tume ya kuchunguza mauaji ya Oktoba 29 na maridhiano (japo bado kuna maswali: watu gani wapo kwenye hiyo tume na wamepatikanaje)
  • Kuanzisha wizara maalum ya vijana na ajira mpya sekta za elimu na afya

Mambo mengine niliyoyasikia ni blah blah za kila mwanasiasa - Mikopo, uboreshaji miundombinu , kilimo, utalii, uwezeshaji madini, kuinua uchumi, tehama, mwendokasi, reli, madaraja mapya etc.

Kilichonishangaza: ni wabunge kupiga makofi mengi pale raisi aliposema anywe maji kidogo 😂😂
 
hotuba.jpg


Cc:
Mbaga Jr
 
Nimesikiliza hotuba ya raisi akifungua rasmi bunge la 13 na nimeona ni kama ameanza kuinama na kujisitiri kutokana na yale yaliyotokea.

  1. Je, ili achutame kabisa kiungwana na kuepuka fedheha inabidi afanye nini?

  2. Kwa wenzangu mliosikiliza hotuba: je imewatia moyo au ndiyo imewaongeza hasira?

  3. Gen Z na wote wanaosapoti D9: kuna hoja hata moja imeongelewa ambayo inagusa malalamiko ya maandamano yaliyopita au yale yajayo?

Binafsi kwa niliyoyasikia nimeona ni inawezekana watawala wameona mabavu siyo suluhisho litakalotufikisha mahali pazuri kama taifa. 
Nafikiri haya mambo 5 yameashiria kwamba sauti za watanzania zina nguvu:
  • Kukiri kuhusu mauaji ya siku za uchaguzi na kutoa pole
  • Mchakato wa katiba mpya kurejea ndani ya siku 100 za kwanza
  • Kufuta kesi za uhaini kwa vijana
  • Tume ya kuchunguza mauaji ya Oktoba 29 na maridhiano (japo bado kna maswali:akina nani wapo hiyo tume na wamepatikanej)
  • Kuanzisha wizara maalum ya vijana na ajira mpya sekta za elimu na afya

Mambo mengine niliyoyasikia ni blah blah za kila mwanasiasa - Mikopo, uboreshaji miundombinu , kilimo, utalii, uwezeshaji madini, kuinua uchumi, tehama, mwendokasi, reli, madaraja mapya etc.

Kilichonishangaza: ni wabunge kupiga makofi mengi pale raisi aliposema anywe maji kidogo 😂😂
huyu mama anauwezo mdogo sana wa kubambanua mambo .
 
Hapo alikuwa anajikosha kwa aibu! Nafsi inamsuta kwa mauaji ya kinyama kama yale! Hizo ahadi zote ni nyimbo zile zile za uongo za miaka nenda rudi.
Bado anafikiri Watanzania watasahau wapendwa wao waliokufa!
Harafu anawaza kuwa kwa kuwa tayari ametawazwa kuwa rais ni garantii ya kumaliza miaka 5!
 
Hapo alikuwa anajikosha kwa aibu! Nafsi inamsuta kwa mauaji ya kinyama kama yale! Hizo ahadi zote ni nyimbo zile zile za uongo za miaka nenda rudi.
Bado anafikiri Watanzania watasahau wapendwa wao waliokufa!
Harafu anawaza kuwa kwa kuwa tayari ametawazwa kuwa rais ni garantii ya kumaliza miaka 5!
Sidhani kama anapata usingizi!
 
Hawa jamaa waliniuliza taarifa za maandamano ulikuwa unazipata wapi nikawaambia jf.. ss kitendo Cha kulala na sim zangu wanaweza wakawa washadukua wanaijua I'd yangu. Hapo nadhani ni kuchange I'd tu niwe huru
Fanya hivyo usije kuingia matatani, hao wapuuzi siyo watu wazuri kabisa 🫤😬
 
Back
Top Bottom